1YA jatutujon otro biaje mananagüe gui oriyan tase; ya mandaña guiya güiya dangculo na linajyan taotao, enao mina jumalom gui un batco, ya matachong gui tase; ya todo y linajyan taotao manestaba gui jilo tano gui oriyan tase.
1Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
2Ya jafanagüe sija megae pot acomparasion, ya ilegña nu sija gui finanagüeña.
2Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
3Ecungog: Estagüe y tatanom na jumuyong para ufananom.
3"Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4Ya anae manananom, palo mamodong gui oriyan chalan; ya mato y pajaron y aire ya macano.
4Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5Ya y palo mamodong gui jilo acho, anae ti megae na oda; ya enseguidas mandoco, sa ti tadong gui eda.
5Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6Lao anae cajulo y atdao, sinenggue, sa taejaleñija manmalayo.
6Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7Ya y palo mamodong gui entalo tituca sija; ya mandoco y tituca sija, ya chiniguet, ya ti manogcha.
7Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
8Ya y palo mamodong gui mauleg na tano, ya manmanogcha, ya mangajulo ya manmegae; ya uno manogcha treinta, y otro sesenta, y otro ciento.
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia."
9Ayo nae ilegña nu sija: Y gae talanga para ufanjungog, güiya uecungog.
9Kisha akawaambia, "Mwenye masikio na asikie!"
10¶ Ya anae estaba güe güiyaja, y manestaba gue oriyaña yan y dose, mafaesen güi ni y acomparasion sija.
10Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
11Ya ilegña nu sija: Jamyo manmanae y misterion raenon Yuus; lao y mangaegue gui sumanjiyong, pot acomparasion nae umafatinas todo estesija;
11Naye akawaambia, "Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
12Para y manlilie, jalie ya ti jasiente; ya y manecungog, manmanjungog, lao ti jatungo; sa no sea ufanmabra talo, ya ufanmmaasie ni isaoñija.
12ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe."
13Ya ilegña nu sija: Ti intingo este na acomparasion? Jafa taemano nae, tungonmiyo todo ni acomparasion sija?
13Basi, Yesu akawauliza, "Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
14Y tatanom jatanme y finijo.
14Mpanzi hupanda neno la Mungu.
15Ya este yuje sija y oriyan chalan, anae manmatanme y finijo; lao despues di jajungog, mato si Satanas, enseguidas, ya janajanao y finijo ni matanme gui corasonñija.
15Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
16Parejoja locue yan este sija y manmatanme gui jilo acho; anae majungog y finijo, enseguidas maresibe todo ni y minagofñija;
16Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
17Lao taya jaleñija, ya ti jadura apmam; sa anae cajulo y triniste, pat y pinetsigue pot y finijo, enseguidas maninefende.
17Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
18Ya este yuje sija y manmatanme gui entalo tituca sija; y jumungog y finijo;
18Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
19Lao y inadajen este y tano, yan y dinaguen y güinaja sija, yan y minalago ni guaja gui palo güinaja sija, manjalom ya machiguet y finijo ya jumuyong ti manogcha.
19lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda.
20Ya este yuje sija y manmatanme gui mauleg na tano; y jumungog y finijo ya maresibe, ya manmanogcha, ya uno treinta y otro sesenta, y otro siento.
20Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja."
21¶ Ylegña nu sija locue: Esta machule y candet para umapolo gui papa medida, pat gui papa cama? Ya ti para umapolo gui jilo lamasa?
21Yesu akaendelea kuwaambia, "Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
22Sa taya na manaatog, ti umafatanñaejon; ni gae gui secreto ya ti umababa.
22Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
23Yaguin guaja gaetalanga para ufanjungog, güiya uecungog.
23Mwenye masikio na asikie!"
24Ylegña nu sija locue: Adaje jafa y jiningogmiyo. Y medida anae inmediye sija, ayoja nae infanmamidiye jamyo; ya infanmanae jamyo mas.
24Akawaambia pia, "Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
25Sa y guaja, umanae: ya y taya, esta y güinajaña, unajanao.
25Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa."
26¶ Ya ilegña: Taegüine y raenon Yuus, yaguin un taotao manyute semiya gui jalom oda;
26Yesu akaendelea kusema, "Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
27Ya maego, ya cajulo gui puenge yan jaane, ya semiya mapta ya doco, ti jatungo jafataemano.
27Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
28Sa y tano güiyaja manogcha, finena jagon, enseguidas y espiga, despues y grano bula gui espiga.
28Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
29Ya yaguin y tinegcha dumangculo, enseguidas mapolo y sese para mangoco, sa mato y cosecha.
29Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika."
30¶ Ya ilegña: Jafajit nae tanaparejo y raenon Yuus? pat jafa na acomparasion nae taacompara?
30Tena, Yesu akasema, "Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
31Parejo yan un granon mostasa, ni y anae matanme gui tano, achogja güiya mas diquique gui entalo todo y semiya sija ni y guaja gui jilo y tano.
31Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
32Lao anae matanme, doco, ya güiya mas dangculo qui todo na golae, ya manramas ni mandangculo na ramasña; ya pot este y pajaron y aire siña mañaga gui papa y nijongña.
32Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake."
33¶ Yan megae sija na acomparasion parejo yan este sija, jasangane sija finijo, jaftaemano y siña jajungog.
33Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
34Ya sin acomparasion ti jasangane sija; lao y disipoluña sija anae mañisijaja janaclaruye todo.
34Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
35Ya ilegña nu sija güijija na jaane, anae esta pupuenge: Nije tafanmalofan gui otro banda.
35Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, "Tuvuke ziwa, twende ng'ambo."
36Ya jadingo y linajyan taotao, ya macone güe mañija, anae gaegue güe sui jalom batco. Ya guaja locue palo diquique na batco mañisija.
36Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
37Ya cajulo un dangculon pagyon manglo, ya jinatme ni napo sija y jalom batco, ya ninabula.
37Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
38Ya güiya gaegue gui popa na mamaego gui jilo alunan; ya mayajo, ya ilegñija nu güiya: Maestro, taya unadadaje na infanmatae?
38Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, "Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?"
39Ya cajulo güe, ya jalalatde y manglo, ya ilegña ni tase: Pacaca famatquilo. Ya bumasta y manglo, ya guaja dangculo na catma.
39Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, "Kimya! Tulia!" Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
40Ya ilegña nu sija: Jafa jamyo na gosmanmaañao? Taye jinengguenmiyo trabia?
40Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?"
41Ya mangosmanmaañao, ya ilegñija entre sija: Jaye este, na asta y manglo yan y tase maosgue güe?
41Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, "Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?"