1YA mandaña guiya güiya y Fariseo sija, yan palo gui escriba sija ni manmato guine Jerusalem,
1Baadhi ya Mafarisayo na walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu walikusanyika mbele ya Yesu.
2Ya malie palo gui disipuluña na mañochocho pan yan áplacha na canae, ni comequeilegña na pot ti jafagase.
2Waliona kwamba baadhi ya wanafunzi wake walikula mikate kwa mikono najisi, yaani bila kunawa.
3Sa y Fariseo sija, yan toda y Judio sija, jaadadaje y tradision manamco sija, yaguin megae nae ti jafagase y canaeñija, ti ufañocho.
3Maana Mafarisayo na Wayahudi wengine wote huzingatia mapokeo ya wazee wao: hawali kitu kabla ya kunawa mikono ipasavyo.
4Ya anae manmato guine y metcado, yaguin ti jafagase sija, ti ufañocho; yan megae sija na güinaja rinesibeñija para ujaadaje, parejoja yan mafagase y copa sija, yan y jara sija, yan y bason coble sija.
4Tena hawali kitu chochote kutoka sokoni mpaka wamekiosha kwanza. Kuna pia desturi nyingine walizopokea kama vile namna ya kuosha vikombe, sufuria na vyombo vya shaba.
5Ya mafaesen ni Fariseo sija yan y escriba sija: Jafa y disipulumo sija na ti manmamómocat taemano y tradision manamco sija; mañochochoja pan yan aplacha y canaeñija?
5Basi, Mafarisayo na walimu wa Sheria wakamwuliza Yesu, "Mbona wanafunzi wako hawayajali mapokeo tuliyopokea kwa wazee wetu, bali hula chakula kwa mikono najisi?"
6Ya ilegña nu sija: Hipocrita jamyo; mauleg sinanganña si Isaias, ni y esta matugue: Este sija na taotao y labiosñija nae maonrayo, lao y corasonñija chago guiya guajo.
6Yesu akawajibu, "Wanafiki ninyi! Nabii Isaya alitabiri ukweli juu yenu alipoandika: Watu hawa, asema Mungu, huniheshimu kwa maneno matupu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami.
7Lao taebale jaadorayo, manmamananagüe ni finanagüe ni tinago taotao sija.
7Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu.
8Sa inpelo jamyo y tinago Yuus, ya mantietiene fitme y tradision taotao sija: (ni y mafagase y jara sija, yan y copa sija, yan infatinas megae sija na güinaja parejo yan este.)
8Ninyi mnaiacha amri ya Mungu na kushikilia maagizo ya watu."
9Ya ilegña nu sija: Magajet jamyo yumute y tinago Yuus para inadaje y tradisionmiyo.
9Yesu akaendelea kusema, "Ninyi mnajua kuepa kwa ujanja sheria ya Mungu kwa ajili ya kufuata mapokeo yenu.
10Sa si Moises ilegña: Onra si tatamo yan si nanamo; ya y mumatdise y tata pat y nana, seguro na umatae.
10Maana Mose aliamuru: Waheshimu baba yako na mama yako, na, Anayemlaani baba au mama, lazima afe.
11Lao jamyo ilegmiyo: Yaguin y taotao ilegña ni tataña pat nanaña: Y Cotban (cumequeilegña y ninae) na jago umaprobecha pot guajo, güiya sumaga libre.
11Lakini ninyi mwafundisha, Kama mtu anacho kitu ambacho angeweza kuwasaidia nacho baba au mama yake, lakini akasema kwamba kitu hicho ni Korbani (yaani ni zawadi kwa Mungu),
12Ya inpelo güe na ufatinas taya para si tataña pat si nanaña;
12basi, halazimiki tena kuwasaidia wazazi wake.
13Inrechasa y sinangan Yuus ni ninaenmiyo na tradision; yan megae sija na güinaja finatinasmiyo parejo yan este.
13Hivyo ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa ajili ya mafundisho mnayopokezana. Tena mnafanya mambo mengi ya namna hiyo."
14¶ Ya jaagang talo guiya güiya todo y linajyan taotao ya ilegña: Ecungog jamyo todos, ya intingo.
14Yesu aliuita tena ule umati wa watu, akawaambia, "Nisikilizeni nyote, mkaelewe.
15Taya gui sumanjiyong gui taotao ni y janajalom, siña numataelaye, lao y janajujuyong gui jinalomña, ayo sija munatataelaye y taotao
15Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mtu toka nje ambacho chaweza kumtia mtu najisi. Lakini kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia mtu najisi."
16(Yaguin guaja gaetalanga para ufanjungog, uecungog)
16Mwenye masikio na asikie!
17Ya anae jumalom gui guima, jadingo y linajyan taotao, y disipuluña sija mafaesen güe ni acomparasion.
17Alipouacha umati wa watu na kuingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza maana ya huo mfano.
18Ya ilegña nu sija: Taegüenaja jamyo locue manaetiningo? Ti intingo na todo y guine jiyong ni jumajalom y taotao ti siña ninataelaye?
18Naye akawaambia, "Je, hata ninyi hamwelewi? Je, hamwelewi kwamba kitu kinachomwingia mtu toka nje hakiwezi kumtia unajisi,
19Sa ti jumajalom gui corasonña na y tiyanña ya malolofan gui secreto; taegüenao janagasgas todo y nengcano.
19kwa maana hakimwingii moyoni, ila tumboni, na baadaye hutolewa nje chooni?" (Kwa kusema hivyo, Yesu alivihalalisha vyakula vyote.)
20Yan ilegña: Y jumujuyong gui taotao, ayo munatataelaye y taotao.
20Akaendelea kusema, "Kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia najisi.
21Sa y gui jinalomña gui corason y taotao sija nae, manjujuyong y manaelaye na jinaso sija, y manadulterio, y manábale yan y manpegno,
21Kwa maana kutoka ndani, katika moyo wa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji,
22Y mañaque sija, y manlatga, y manaelaye, y dinague, y inábale, y taelaye na atadog, y chinatfino contra si Yuus, y sobetbio, y bababa:
22uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu.
23Todo este sija na tinaelaye, manguine jalom ya janatataelaye y taotao.
23Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu najisi."
24¶ Ya cajulo güije, mapos para y oriyan Tiro yan Sidon; ya jumalom gui guima, malagoña na taya utiningo; lao ti siña unatog.
24Yesu aliondoka hapo, akaenda hadi wilaya ya Tiro. Huko aliingia katika nyumba moja na hakutaka mtu ajue; lakini hakuweza kujificha.
25Sa jajungog masasangan güe un palaoan na y diquique na jagaña, guaja un áplacha na espiritu, mato ya jatomba güe gui adengña:
25Mwanamke mmoja ambaye binti yake alikuwa na pepo, alisikia habari za Yesu. Basi, akaja akajitupa chini mbele ya miguu yake.
26Ya y palaoan Griega, gui tano Sirofenisa, y tinayuyut güe na uyute juyong gui jagaña y anite.
26Mama huyo alikuwa Mgiriki, mwenyeji wa Sirofoinike. Basi, akamwomba Yesu amtoe binti yake pepo mchafu.
27Lao ilegña nu guiya: Polo finena ya ufanjaspog y famaguon sija; sa ti mauleg machule y pan y famaguon, ya ufanmayotte y galago sija.
27Yesu akamwambia, "Kwanza watoto washibe; kwa maana si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa."
28Ya manope y palaoan, ilegña: Junggan, Señot; lao y galago sija, gui papa lamasa, jacacanoja y andesmoronan y famaguon sija.
28Lakini huyo mama akasema, "Sawa, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto."
29Ayo nae ilegña ni palaoan: Pot este na sinangan, janao y anite jumanao gui jagamo.
29Yesu akamwambia, "Kwa sababu ya neno hilo, nenda. Pepo amemtoka binti yako!"
30Ya anae jumanao para iyasija, jasoda na y jagaña umaason gui jilo cama, ya y anite esta jumanao.
30Basi, akaenda nyumbani kwake, akamkuta mtoto amelala kitandani, na pepo amekwisha mtoka.
31¶ Ya tumalo jumanao gui oriyan Tiro yan malofan guiya Sidon, ya mato gui tasen Galilea; ya malofan gui entalo y oriyan Decapolis.
31Kisha Yesu aliondoka wilayani Tiro, akapitia Sidoni, akafika ziwa Galilaya kwa kupitia nchi ya Dekapoli.
32Ya maconie güe un tanga ya udo, ya matayuyut güe na upolo y canaeña gui jiloña.
32Basi, wakamletea bubu-kiziwi, wakamwomba amwekee mikono.
33Ya janasajnge güe gui linajyan taotao, ya japolo y calolotña gui talangan y tanga, ya tumola ya japacha y jilaña;
33Yesu akamtenga na umati wa watu, akamtia vidole masikioni, akatema mate na kumgusa ulimi.
34Ya jaatan julo y langet sumospiros, ya ilegña: Efatha, cumequeilegña, mababa!
34Kisha akatazama juu mbinguni, akapiga kite, akamwambia, "Efatha," maana yake, "Funguka."
35Ya mababa y talangaña; ya mapula y gumogode y jilaña, ya cumuentos mauleg.
35Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema sawasawa.
36Ya jaencatga sija, na chañija sumangangane ni jaye; lao mientras mas jaencatga, mas manamamto;
36Yesu akawaamuru wasimwambie mtu juu ya jambo hilo. Lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari hiyo.
37Ya ninafangosmanman, ilegñija: Mauleg finatinasña todo: janafanmanjungog y mananga, ya y manudo janafanguentos.
37Watu walishangaa sana, wakasema, "Amefanya yote vyema: amewajalia viziwi kusikia, na bubu kusema!"