1YA ilegña nu sija: Magajet jusangane jamyo, na guaja palo sija ni mangaegue güine na ti ujaguaeya finatae, asta que jalie y raenon Yuus na mato yan ninasiña.
1Yesu akaendelea kuwaambia, "Kweli nawaambieni, wako wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa enzi."
2¶ Anae esta malofan y sais na jaane, si Jesus jacone si Pedro, yan si Santiago, yan si Juan, janafañajnge sijaja gui un taquilo na ogso; ya jaago güe gui menanñija.
2Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane juu ya mlima mrefu peke yao. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao,
3Ya y magaguña manmañila, gosapaca calang niebe, taya ni un fafagas gui tano siña munaapaca taegüine.
3mavazi yake yakang'aa, yakawa meupe sana, jinsi dobi yeyote duniani asingeweza kuyafanya meupe.
4Ya manalie na mato guiya güiya si Elias yan Moises, na manguecuentos yan si Jesus.
4Eliya na Mose wakawatokea, wakazungumza na Yesu.
5Ayo nae manope si Pedro, ilegña as Jesus: Maestro mauleg utafañagajit güine, ya tafanmamatinas tres tabetnáculo; para jago y uno, para si Moises y otro, yan para si Elias y otro.
5Petro akamwambia Yesu, "Mwalimu, ni vizuri sana kwamba tuko hapa. Basi, afadhali tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya."
6Si ti jatungo jafa usangan, sa estaba mangosmaañao.
6Yeye na wenzake waliogopa hata hakujua la kusema.
7Ya mato un mapagajes y manjineme sija, ya un inagang gui mapagajes, ilegña: Este y güinaeyaco na Lajijo, jingog güe.
7Kisha likatokea wingu likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu, "Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni."
8Ya derepente jaatan gui oriyañija, ti manmanlie ni jaye, na si Jesusja yan sija.
8Mara wanafunzi hao wakatazama tena, lakini hawakumwona mtu mwingine, ila Yesu peke yake pamoja nao.
9Ya anae manunog sija guine y egso, jaencatga sija na chañija sumangangane ni jaye ni liniiñija, asta que y Lajin taotao esta cajulo guine entalo y manmatae.
9Walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwakataza wasimwambie mtu yeyote mambo waliyoyaona, mpaka Mwana wa Mtu atakapokuwa amefufuka kutoka wafu.
10Ya sija jaadaje ayo na sinangan guiya sijaja, manafaesen gui entaloñija: Jafa ayo y cajulo guine entalo y manmatae cumequeilegña.
10Basi, wakashika agizo hilo, lakini wakawa wanajadiliana wao kwa wao maana ya kufufuka kutoka wafu.
11Ya mafaesen güe, ilegñija: Y escriba sija ilegñija, si Elias nesesita ufato finenana.
11Wakamwuliza Yesu, "Mbona walimu wa Sheria wanasema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?"
12Güiya manope ilegña nu sija: Si Elias magajet nesesita ufato finenana, ya jafatinas talo todo y güinaja: Jafa esta matugue gui Lajin taotao na upadese megae ya manataya guaelayeña?
12Naye akawajibu, "Naam, Eliya anakuja kwanza kutayarisha yote. Hata hivyo, kwa nini basi imeandikwa katika Maandiko Matakatifu kwamba Mwana wa Mtu atapatwa na mateso mengi na kudharauliwa?
13Lao jusangane jamyo na si Elias esta mato ya esta mafatinas guiya güiya todo y malagoñija, taegüine esta matugue nu güiya.
13Lakini nawaambieni, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtendea walivyotaka kama ilivyoandikwa juu yake."
14¶ Ya anae mato gui disipuluña sija, jalie un dangculon linajyan taotao gui oriyañija, yan y escriba sija ni manafaesen yan sija.
14Walipowafikia wale wanafunzi wengine, waliona umati mkubwa wa watu hapo. Na baadhi ya walimu wa Sheria walikuwa wanajadiliana nao.
15Ya enseguidas todo y linajyan taotao, anae malie güe, ninafangosmanman, ya manmalago guato guiya güiya ya masaluda güe.
15Mara tu ule umati wa watu ulipomwona, wote walishangaa sana, wakamkimbilia wamsalimu.
16Ya jafaesen sija, ilegña! Jafana manafaesen jamyo yan sija?
16Yesu akawauliza, "Mnajadiliana nini nao?"
17Ya manope uno gui linajyan taotao, ilegña: Maestro juconie jao mague na lajijo, na guaja un espiritun udo;
17Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu, "Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
18Ya manoja nae quinene güe, japedadasos; ya bóboan, ya janachechegcheg y nifenña, ya ninayafae; ya jusangane y disipulumo sija, na ujayute juyong, lao ti manasiña.
18Kila mara anapomvamia, humwangusha chini na kumfanya atokwe na povu kinywani, akisaga meno na kuwa mkavu mwili wote. Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo lakini hawakuweza."
19Manope güe, ilegña nu sija: O generasion ni ti manjonggue! asta ngaean nae utafanjijitaja? asta ngaean nae jususungonja jamyo? maelayofan mague.
19Yesu akawaambia, "Enyi kizazi kisicho na imani! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni kwangu."
20Ya maconie guato guiya güiya; ya anae jalie, enseguidas y espiritu manlálaolao güe; ya güiya podong gui jilo oda gumagalileg ya bóboan.
20Wakampeleka. Mara tu huyo pepo alipomwona Yesu, alimtia mtoto kifafa, naye mtoto akaanguka chini, akagaagaa na kutoka povu kinywani. Yesu akamwuliza baba yake huyo mtoto,
21Ya jafaesen y tataña; cuanto tiempo esta desde qui mato este guiya güiya? Güiya ilegña: Desde qui diquique:
21"Amepatwa na mambo hayo tangu lini?" Naye akamjibu, "Tangu utoto wake.
22Ya megae na biaje nae yinite gui jalom guafe, yan y jalom janom para upinino; lao yaguin siña jao ayudajam, gaemaase nu jame.
22Na mara nyingi pepo huyo amemwangusha motoni na majini, ili amwangamize kabisa. Basi, ikiwa waweza, utuhurumie na kutusaidia!"
23Si Jesus, ilegña nu güiya: Yaguin siña jao, todo siña para y manjonggue.
23Yesu akamwambia, "Eti ikiwa waweza! Mambo yote yanawezekana kwa mtu aliye na imani."
24Enseguidas y tatan y patgon, jaagang yan y lagoña, ya elegña: Jujonggue; ayuda y taejinenggueco.
24Hapo, huyo baba akalia kwa sauti, "Naamini! Lakini imani yangu haitoshi, nisaidie!"
25Ya anae si Jesus jalie na manmalalago y linajyan taotao, jalalatde y áplacha na espiritu, ilegña: Espiritun udo yan tanga, guajo jao tumago, juyong guiya güiya, ya chamo jumajalom talo guiya güiya.
25Yesu alipouona umati wa watu unaongezeka upesi mbele yake, alimkemea yule pepo mchafu, "Pepo unayemfanya huyu mtoto kuwa bubu-kiziwi, nakuamuru, mtoke mtoto huyu wala usimwingie tena!"
26Ayo nae y espiritu umagang, ya manlalaolao güe megae, ya jumuyong; ya güiya sumaga calang matae, enaomina megae ilegñija, na esta matae.
26Hapo huyo pepo alipaaza sauti, akamwangusha huyo mtoto chini, kisha akamtoka. Mtoto alionekana kama maiti, hata wengine walisema, "Amekufa!"
27Lao si Jesus jamantiene canaeña, ya jinatsa güe; ya cajulo.
27Lakini Yesu akamshika mkono, akamwinua, naye akasimama.
28Ya anae jumalom güe gui jalom guma, y disipuluña sija mafaesen güe en secreto, ilegñija: Jafajam na ti innasiña yumute juyong?
28Yesu alipoingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza kwa faragha, "Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?"
29Ya ilegña nu sija: Este na rasan anite sija, taya siña munajanao, na y tinayuyut.
29Naye akawaambia, "Pepo wa aina hii hawezi kutoka isipokuwa kwa sala tu."
30¶ Ya manmapos güije, manmalofan inanaco Galilea; ya ti malago na guaja utiningo güe.
30Yesu na wanafunzi wake waliondoka hapo, wakaendelea na safari kupitia wilaya ya Galilaya. Yesu hakupenda watu wajue alipokuwa,
31Sa jafanagüe y disipuluña sija ya ilegña nu sija: Y Lajin taotao umaentrega gui canae taotao sija, ya umapuno; lao yaguin este matae, ucajulo talo despues di tres na jaane.
31kwa sababu alikuwa anawafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, "Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu ambao watamuua; lakini siku ya tatu baada ya kuuawa atafufuka."
32Lao sija ti jatungo este na sinangan, ya manmaañao na ujafaesen güe.
32Wanafunzi hawakufahamu jambo hilo. Wakaogopa kumwuliza.
33¶ Ya mato guiya Capernaum; ya anae mato gui guima, jafaesen sija: Jafa jamyo na manafaesen entalomiyoja gui chalan?
33Basi, walifika Kafarnaumu. Na alipokuwa nyumbani, aliwauliza, "Mlikuwa mnajadiliana nini njiani?"
34Lao sija manmamatquiquiloja; sa guine manafaesen gui chalan uno y otro, jaye guiya sija udangculo.
34Lakini wao wakanyamaza, maana njiani walikuwa wamebishana ni nani aliye mkuu kati yao.
35Ayo nae manmatachong, ya jaagang y dose ya ilegña nu sija: Y malago fuminenana, uuttimon gui tododos, yan utentagon tododos.
35Yesu akaketi chini, akawaita wale kumi na wawili, akawaambia, "Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza lazima awe wa mwisho na kuwa mtumishi wa wote."
36Ya jacone un patgon, ya japolo gui entaloñija; ya jajogüe gui canaeña, ya ilegña nu sija:
36Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kati yao, akamku mbatia, halafu akawaambia,
37Y rumesibe pot y naanjo uno ni manaegüine na famaguon, jaresibe yo, ya y rumesibe yo, ti guajo jaresibe, na y tumago yo.
37"Anayempokea mtoto kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi; na anayenipokea mimi, hanipokei mimi tu, bali anampokea yule aliyenituma."
38Si Juan, ilegña nu güiya: Maestro, inlie uno na manyute juyong anite sija pot y naanmo, ya inchema, sa ti jadadalalagjit.
38Yohane akamwambia, "Mwalimu, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako, nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
39Ya si Jesus ilegña: Chamiyo chumochoma; sa ni uno ni fumatinas milagro pot y naanjo, siña gusisija jasangan taelaye guiya guajo.
39Lakini Yesu akasema, "Msimkataze, maana hakuna mtu anayefanya muujiza kwa jina langu, na papo hapo akaweza kusema mabaya juu yangu.
40Sa ayo y ti contra jita, manjijitaja.
40Maana, asiyepingana nasi, yuko upande wetu.
41Sa jayeja y numae jamyo un copan janom, sa iyon Cristo jamyo, magajet jusangane jamyo, na sen ti ufalingo y apasña.
41Mtu yeyote atakeyewapeni kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu ninyi ni watu wake Kristo, hakika hatakosa kupata tuzo lake.
42Ya jayeja y ninaquepodong uno guine sija gui mandiquique ni jumonggue yo; mauleg para güiya, umagode gui agagaña un acho atutong, ya umayute gui jalom tase.
42"Mtu yeyote atakayemfanya mmoja wa hawa wadogo wanaoniamini atende dhambi, ingekuwa afadhali kwa mtu huyo kufungiwa shingoni mwake jiwe kubwa la kusagia na kutupwa baharini.
43Lao yaguin y canaemo ninaquepodong jao, utut; maulegña na unjalom gui linâlâ mangco, qui uguaja dos canaemo, ya unjanao para sasalaguan, y guafe ni ti siña mapuno.
43Mkono wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia kwenye uzima bila mkono mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika moto wa Jehanamu.
44(Anae y iloñija ti ufanmatae; ya y guafe taejinecog nae umapuno.)
44Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
45Ya yaguin y adengmo ninaquepodong jao, utut: maulegña na unjalom gui linâlâ cojo, qui uguaja dos adengmo ya unyenite para sasalaguan;
45Na mguu wako ukikukosesha, ukate! Afadhali kuingia katika uzima bila mguu mmoja, kuliko kuwa na miguu yote miwili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
46(Anae y iloñija ti ufanmatae, ya y guafe taejinecog nae umapuno.)
46Humo, wadudu wake hawafi na moto hauzimiki.
47Ya yaguin y atadogmo ninaquepodong jao, lagnos; maulegña na unjalom gui raenon Yuus, yan un atadogja, qui uguaja dos atadogmo ya unyenite para sasalaguan.
47Na jicho lako likikukosesha, ling'oe! Afadhali kuingia katika utawala wa Mungu ukiwa na jicho moja tu, kuliko kuwa na macho yako yote mawili na kutupwa katika moto wa Jehanamu.
48(Anae y iloñija ti ufanmatae, ya y guafe taejinecog na umapuno.)
48Humo wadudu wake hawafi, na moto hauzimiki.
49Sa todos ufanmaasne yan guafe; (ya todo y inefrese ufanmaasne yan asiga).
49"Maana kila mmoja atakolezwa kwa moto.
50Mauleg y asiga; lao yaguin y asiga malingo y maasenña, jaftaemano numamaasen? Guaja asiganmiyo guiya jamyoja; yan guaja pas gui entalomiyo.
50Chumvi ni nzuri, lakini ikipoteza ladha yake, itakolezwa na nini? Muwe na chumvi ndani yenu na kudumisha amani kati yenu."