1AYO nae jaagang y dose na disipuluña, ya janae ninasiñañija contra y manaplacha na espiritu, para ujayute juyong; yan unafanmagong todo y chetnot, yan todo y manpinite.
1Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote.
2Ya y naan y dose apostoles sija este sija: Y finenana, si Simon na mafanaan si Pedro, yan si Andres cheluña: si Santiago, lajin Sebedeo, yan si Juan cheluña;
2Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: wa kwanza ni Simoni aitwae Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;
3Si Felipe, yan si Bartolome; si Tomas, yan si Mateo y publicano; si Santiago, lajin Alfeo, yan si Lebeo, na y apiyiduña si Tadeo;
3Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;
4Si Simon Selote, yan si Judas Iscariote, ni y umintrega güe locue.
4Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
5Este y dose sija mantinago as Jesus na ufanjanao ya maninencatga ilegña: Chamiyo fanmalag y chalan y Gentiles; yan y siuda y Samaritano sija chamiyo fanjajalom:
5Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: "Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika mji wa Wasamaria.
6Lao gosmauleg para ufanmalag y malingo na quinilo gui guima Israel.
6Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.
7Anae manjanao jamyo, setmon ya alog: Y raenon langet mato jijot.
7Mnapokwenda hubirini hivi: Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8Nafanjomlo y manmalango, nafan gasgas y manategtog, nafangajulo y manmatae, nafanjanao y anite sija: pot grasia na inresibe, fanmannae pot grasia.
8Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.
9Chamiyo fannanaetnon oro ni salape ni coble gui betsanmiyo;
9Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.
10Ni tengguang para y chalan, ni dos na magago ni sapatos, ni baston; sa y fafáchocho jamerese y nengcanoña.
10Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.
11Yan todo na siuda, pat songsong na manjalom jamyo, guesaligao jaye mumerese, ya fañaga güije asta qui para infanjanao.
11"Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu yeyote aliye tayari kuwakaribisheni, na kaeni naye mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
12Yaguin manjalom jamyo gui guima, saluda.
12Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.
13Yaguin y guima jamerese, y pasmiyo usaga guiya güiya; lao yaguin ti jamerese, y pasmiyo utaloja guato guiya jamyo.
13Kama wenyeji wa nyumba hiyo wakiipokea salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawaipokei, basi amani yenu itawarudia ninyi.
14Ya jayeja y ti rumesibe jamyo, yan ti jaecungog y sinanganmiyo, fanjanao güije na guma pat suida, ya insacude contra sija todo y petbos gui adengmiyo.
14Kama mtu yeyote atakataa kuwakaribisheni au kuwasikilizeni, basi mtokapo katika nyumba hiyo au mji huo, yakung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.
15Magajet jusangane jamyo: Y mas mauleg para y tano Sodoma yan Gomora gui jaanin sentensia, qui para ayo na siuda.
15Kweli nawaambieni, Siku ya hukumu mji huo utapata adhabu kubwa kuliko ile iliyoipata miji ya Sodoma na Gomora.
16¶ Estagüe, na guajo jamyo tumago, calang quinilo gui entalo lobo sija; fanmalate calang y serpiente sija, yan y fanmanso calang y paluma sija.
16"Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa.
17Adaje jamyo nu y taotao sija; sa infaninentrega gui inetnon ofisiat, ya infanmasaolag gui sinagogañija;
17Jihadharini na watu, maana watawapeleka ninyi mahakamani na kuwapiga viboko katika masunagogi yao.
18Ya infanmacone guato gui menan magalaje yan ray pot y naanjo, para testimonio contra sija yan y Gentiles.
18Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu, mpate kutangaza Habari Njema kwao na kwa mataifa.
19Lao yaguin manmaentrega jamyo, chamiyo jumajaso jafa para insangan; so ayoja na ora infanmanae jafa para insangan.
19Basi, watakapowapeleka ninyi mahakamani, msiwe na wasiwasi mtasema nini au namna gani; wakati utakapofika, mtapewa la kusema.
20Sa ti jamyo infanguentos, lao y Espiritun y Tatanmiyo ni y cumuecuentos gui jalommiyo.
20Maana si ninyi mtakaosema, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.
21Y cheloja uinentrega y cheluña para umapuno, ya y tata y lajiña: ya y famaguon ufangajulo contra tatañija, ujanamapuno.
21"Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe, na baba atamsaliti mwanawe, nao watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
22Ya todo infanchinatlie pot y naanjo; lao y sumigue asta y uttimo, güiya ucajulo gui langet.
22Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
23Lao yaguin manmapetsigue jamyo gui un suida, fanmalag y otro: sa magajet jusangane jamyo, na ti infanmunjayan manjanao todo gui siudan Israel, asta qui mato y Lajin taotao.
23"Watu wakiwadhulumu katika mji mmoja, kimbilieni mji mwingine. Kweli nawaambieni, hamtamaliza ziara yenu katika miji yote ya Israeli kabla Mwana wa Mtu hajafika.
24Y disipulo, ti dangculoña qui y maestro, yan y tentago qui y amuña.
24"Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumishi si mkuu kuliko bwana wake.
25Bastaja y disipulo yaguin parejoja y maestruña, ya y tentago yaguin parejoja y amuña. Sa yaguin y tata gui guima mafanaan Beetsebub, cuanto mas y familiana?
25Yatosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumishi kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mkubwa wa jamaa Beelzebuli, je hawatawaita watu wengine wa jamaa hiyo majina mabaya zaidi?
26Chamiyo fanmaañao; sa taya matatampe, para ti umalie: yan manaatog para ti umatungo.
26"Basi, msiwaogope watu hao. Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, na kila kilichofichwa kitafichuliwa.
27Todo sija y jusangane jamyo gui jemjom, sanganñaejon gui manana: ya todo sija y injingog gui talanga, sanganñaejon desde y jilo guma.
27Ninalowaambieni ninyi katika giza, lisemeni katika mwanga; na jambo mlilosikia likinong'onezwa, litangazeni hadharani.
28Ya chamiyo fanmaañao ni upinino y tataotao; sa ti siña japuno y ante: lao fanmaañaoñao ni ayo y siña yumute y tataotao yan y ante guato guiya sasalaguan.
28Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu.
29Ada ti mabende dos gorrión na pájaro pot un coble? yan ni uno guiya sija upodong gui tano sin utungo si tatanmiyo.
29Shomoro wawili huuzwa kwa senti tano. Lakini hata mmoja wao haanguki chini bila kibali cha Baba yenu.
30Y gaponulonmiyo locue esta todo manmatufong.
30Lakini kwa upande wenu, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.
31Chamiyo fanmaañao; sa mas manbaliñaja jamyo qui y megae na pájaro.
31Kwa hiyo msiogope; ninyi mu wa thamani kuliko shomoro wengi.
32Jayeja y sumanganyo gui menan taotao, güajo locue jusangangüe gui menam y tatajo ni gaegue gui langet.
32"Kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
33Ya jayeja y pumuneyo gui menan taotao sija, guajo locue jupune güe gui menan y tatajo ni y gaegue gui langet.
33Lakini yeyote atakayenikana hadharani, nami nitamkana mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.
34¶ Chamiyo jumajaso na mato yo para jupolo pas gui tano: ti matoyo para jupolo pas, lao espada.
34"Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga.
35Sa mato yo para jupolo inaguaguat y laje contra y tataña, ya y jaga contra y nanaña, ya y yetna contra y suegraña.
35Maana nimekuja kuleta mafarakano kati ya mtu na baba yake, kati ya binti na mama yake, kati ya mkwe na mkwe wake.
36Ya y enemigoñija mangaegueja guiya sija.
36Na maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.
37Y gumaeya y tataña pat y nanaña mas qui guajo, ti ufanmerese nu guajo; ya y gumaeya y lajiña pat y jagaña mas qui guajo, ti ufanmerese nu guajo.
37"Ampendaye baba au mama yake kuliko anipendavyo mimi, hanistahili. Ampendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38Ya, y ti chumule y quiluusña ya udalalagyo, ti ufanmerese nu guajo.
38Mtu asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili.
39Y sumoda y linâlâña, ufinalingaeguan; ya y finalingaeguan ni y linâlâña pot y naanjo, güiya usoda.
39Anayeyashikilia maisha yake, atayapoteza; lakini anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata.
40¶ Y rumisibe jamyo, jaresibeja yo; ya y rumisibeyo, jaresibeja y tumagoyo.
40"Anayewakaribisha ninyi, ananikaribisha mimi; na anayenikaribisha mimi, anamkaribisha yule aliyenituma.
41Y rumesibe un profeta pot y naan profeta, uresibe y premion profeta; ya y rumesibe y taotao tunas pot y naan y taotao tunas, uresibe y premion y taotao tunas.
41Anayemkaribisha nabii kwa sababu ni nabii, atapokea tuzo la nabii. Anayemkaribisha mtu mwema kwa sababu ni mtu mwema, atapokea tuzo la mtu mwema.
42Ya masquesea jayeja y numae uno güine nu este sija y mandiquique, unoja bason janom ni y fresco, pot y naan y disipulo, magajet jusangane jamyo na ti ufalingo y premiuña.
42Kweli nawaambieni, yeyote atakayempa mmojawapo wa wadogo hawa kikombe cha maji baridi kwa sababu ni mfuasi wangu, hatakosa kamwe kupata tuzo lake."