Chamorro: Psalms, Gospels, Acts

Swahili: New Testament

Matthew

9

1YA jumalom gui un batco, mapos güe, ya malag y otro banda ya mato gui suidaña.
1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2Ya, estagüe, sija na manmangongone güe un malango, umaason gui cama sa paralitico; ya anae jalie si Jesus y jinenggueñija, ilegña nu y paralitico: Angoco lajijo; y isaomo unmaasie.
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
3Ya estagüe sija palo escriba na ilegñija gui sanjalomñija: Este chumatfino contra si Yuus.
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
4Ya anae jatungo si Jesus y jinasoñija, ilegña: Jafa na manmanjajaso jamyo taelaye gui corasonmiyo?
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
5Sa jafa mas guse masangan: Y isaomo unmaasie: pat masangan: Cajulo ya unfamocat?
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
6Lao para intingoja na y Lajin taotao guaja ninasiñaña, gui jilo tano, para umaasie isao; (ayo nae ilegña nu y paralitico), Cajulo, chule y camamo ya unjanao para iyajamyo.
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
7Ayo nae cajulo ya mapos para iyasija.
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
8Ya anae malie nu y linajyan taotao, ninafanmanman, ya manamalag si Yuus, sa mannae nu ayo na ninasiña gui taotao sija.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
9¶ Ya anae malofan si Jesus güije, jalie un taotao na matatachong gui bancon y tributo, na y naanña si Mateo, ya ilegña nu güiya, Dalalagyo. Ya cajulo ya dinalalag güe.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
10Ya susede anae estaba güe, matachong chumochocho gui jalom guma, estagüe, sija megae na publicano yan manisao, manmato ya mañija manmatachong gui lamasa yan si Jesus yan y disipuluña sija.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
11Ya anae malie este nu y Fariseo sija, ilegñija nu y disipuluña: Sa jafa y maestronmiyo na mañisija mañocho yan y publicano yan y manisao?
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
12Lao anae jajungog ayo, ilegña: Y manaechetnot ti janesesita medico: lao y manmalango.
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
13Janao ya inquetungo jafa este: Minaase malagojo, ya ti inefrese; sa ti mato yo para juaagang y manunas, lao y manisao para ufanmañotsot.
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
14¶ Ayo nae y disipulon Juan manmato guiya güiya ya ilegñija: Jafa jame yan y Fariseo sija na manayuyunat megae; ya y disipulumo ti manayuyunat?
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
15Ya ilegña si Jesus nu sija: Siña y mangachong y nobio, mantriste yaguin mañisijaja yan y nobio? Lao ufato y jaane, na y nobio umacone guiya sija, ya ayo nae ufanayunat.
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
16Taya ni un taotao lumimendanñaejon y nuebo na magago gui mamagagonñañajeon ni y bijo; sa ayo na lemenda usuja gui magago, ya y minatitegña sentaelaye.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
17Ni umasajguane locue y nuebo na bino gui bijo na boteyan cuero sa y boteyan cuero umafag ya umachuda y bino, ya manmalingo y boteyan cuero; lao umasajguane y nuebo na bino gui nuebo na boteyan cuero, ya uchamaog y dos.
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
18¶ Mientras jasangangane sija ni este, estagüe, un magas na mato ya inadoragüe ilegña: Y jagajo matae tiampmanja; lao nije ya maela ya unpolo y canaemo gui jiloña ya ulâlâ.
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
19Ya cajulo si Jesus ya dinalalag güe, yan y disipuluña locue.
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
20¶ Ya, estagüe, un palaoan na malango nu y minilalag y jâgâ, esta dose años, mato gui tateña ya japacha y madoblan y magaguña;
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
21Sa ilegña gui sumanjalomña: Yaguin jupachaja y magaguña, jujomlo.
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
22Lao si Jesus jabiragüe ya anae malie güe ilegña: Jagajo, angoco, y jinengguemo unninajomlo. Ya y palaoan ninajomlo desde ayo na ora.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
23Ya anae mato si Jesus gui guima ayo na magas, ya jalie y mandadandan nu y flauta yan y taotao sija manboruruca,
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
24Ylegña: Fañuja; sa y patgon palaoan ti mamatae, lao mamaego. Ya mabutleagüe.
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
25Lao y taotao sija anae mañuja, güiya mapos jalom, ya jamantiene canaeña; ya y patgon palaoan cajulo.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
26Ya malofan este na fama todo güije na tano.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
27¶ Anae mafapos si Jesus güije, madalalag güe dos taotao na bachet na umaagang ilegñija: Gaease nu jame, jago, Lajin David.
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
28Ya anae mato guato gui jalom guma, manmato guiya güiya y dos bachet, ya si Jesus ilegña nu sija: Injenggue na guajo siña jufatinas este? Ya sija ilegñija: Junggan Señot.
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
29Ayo nae japacha y atadogñija ya ilegña: Parejoja y jinengguenmiyo umafatinas.
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
30Ya y atadogñija manmababa. Ya si Jesus jagosencatga ilegña. Adaje ya chamiyo munatutungo ni uno.
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
31Lao anae manmapos sija, manafamta y famaña todo güije na tano.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
32¶ Ya anae manmapos sija; estagüe, machule guiya güiya un taotao na udo, na gaeanite.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
33Anae ninajanao y anite y udo cumuentos. Ya y linajyan taotao ninafanmanman ya ilegñija: Taya este nae malie guiya Israel.
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
34Lao y Fariseo sija ilegñija: Pot y ninasiña y prinsipen anite, janajanao y anite sija.
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
35Ya jalilicue si Jesus todo y siuda sija yan y sengsong, mamananagüe gui guima Yuusñija, ya jasesetmon y ebangelion y raeno, yan janafanmamagong todo y chetnot yan todo y pinite gui taotao sija.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
36¶ Anae jalie y linajyan taotao, ninamaase nu sija, sa manadingo ya manmachalapon calang y quinilo nu y taya pastotñija.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
37Ayo nae ilegña nu y disipuluña: Magajet na y cosecha megae: lao y manfáfachocho didide.
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
38Tayuyut y Señot y cosecha ya utago y manfáfachocho gui cosechaña.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."