1Uostalom, braćo, molimo vas i zaklinjemo u Gospodinu Isusu: primili ste od nas kako treba da živite da biste ugodili Bogu. Vi tako i živite pa sve više napredujete!
1Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
2Ta znate koje smo vam zapovijedi dali u Gospodinu Isusu.
2Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
3Doista, ovo je volja Božja: vaše posvećenje - da se uzdržavate od bludnosti,
3Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
4da svatko od vas zna svoje tijelo posjedovati u svetosti i poštovanju,
4Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
5a ne u pohotnoj strasti kao pogani koji ne poznaju Boga,
5na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
6pa time ne prikraćivati i varati svoga brata. Jer Gospodin je osvetnik za sve to, kao što vam već rekosmo i posvjedočismo.
6Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
7Bog nas, doista, nije pozvao na nečistoću, nego na svetost.
7Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
8Prema tome, tko to odbacuje, ne odbacuje čovjeka nego Boga koji svoga Duha Svetoga udahnjuje u vas.
8Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
9A o bratoljublju vam nije potrebno pisati. Ta i sami ste od Boga naučili ljubiti jedni druge,
9Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
10a to doista i činite prema svoj braći u cijeloj Makedoniji. Samo vas, braćo, potičemo da u tom još više uznapredujete
10Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
11pa da se trsite mirno živjeti, svoje činiti i raditi svojim rukama, kako smo vam zapovijedili,
11Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
12te tako časno živite prema onima vani i nikoga ne trebate.
12Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
13Nećemo da budete u neznanju, braćo, o onima koji su usnuli, da ne tugujete kao drugi koji nemaju nade.
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
14Doista, ako vjerujemo da je Isus umro i uskrsnuo, onda će Bog i one koji usnuše u Isusu, privesti zajedno s njime.
14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15Ovo vam uistinu velimo po riječi Gospodnjoj: mi živi, preostali za Dolazak Gospodnji, nećemo preteći onih koji su usnuli.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
16Jer sam će Gospodin - na zapovijed, na glas arkanđelov, na zov trublje Božje - sići s neba. I najprije će uskrsnuti mrtvi u Kristu,
16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17a zatim ćemo mi živi, preostali, zajedno s njima biti poneseni na oblacima u susret Gospodinu, u zrak. I tako ćemo uvijek biti s Gospodinom.
17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
18Tješite se dakle uzajamno ovim riječima!
18Basi, farijianeni kwa maneno haya.