1Priopćujemo vam, braćo, milost Božju koja je dana crkvama makedonskim:
1Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
2unatoč mnogim kušnjama i nevoljama izobilna njihova radost i skrajnje siromaštvo preli se u bogatstvo darežljivosti.
2Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
3Svjedočim uistinu: oni su nas dragovoljno - po svojim mogućnostima i preko mogućnosti -
3Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
4veoma usrdno molili za milost zajedništva u ovom posluživanju svetih.
4walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
5I to ne samo kako se nadasmo, nego same sebe predadoše najprvo Gospodinu, a onda nama, po volji Božjoj.
5Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
6Zato zamolismo Tita da kao što je započeo, tako i dovrši među vama i to djelo darežljivosti.
6Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
7Stoga kao što se u svemu odlikujete - u vjeri, i riječi, i spoznanju, i svakoj gorljivosti, i u ljubavi svojoj prema nama - odlikujte se i u ovoj darežljivosti.
7Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
8Ne zapovijedam, nego gorljivošću drugih prokušavam istinitost vaše ljubavi.
8Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
9Ta poznate darežljivost Gospodina našega Isusa Krista! Premda bogat, radi vas posta siromašan, da se vi njegovim siromaštvom obogatite.
9Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
10Time dajem samo savjet: to doista dolikuje vama koji već prošle godine prvi to započeste, ne samo činom nego i odlukom.
10Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
11Sada dovršite to djelo da kao što spremno odlučiste, tako prema mogućnostima i dovršite.
11Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
12Jer ima li spremnosti, mila je po onom što ima, a ne po onom čega nema.
12Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
13Ne dakako: drugima olakšica, vama oskudica, nego - jednakost!
13Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
14U sadašnjem trenutku vaš suvišak za njihovu oskudicu da jednom njihov suvišak bude za vašu oskudicu - te bude jednakost,
14Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
15kao što je pisano: Nije ništa preteklo onome koji bijaše nakupio mnogo, a niti je nedostajalo onome koji bijaše nakupio manje.
15Kama Maandiko yasemavyo: "Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa."
16A hvala Bogu koji je stavio jednaku gorljivost za vas u srce Titovo.
16Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
17On je prihvatio i molbu, ali budući da je veoma revan, otiđe k vama i dragovoljno.
17Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
18S njime pak šaljemo brata kojega s evanđelja slave sve crkve.
18Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
19Štoviše, crkve ga izabraše za našeg suputnika u ovom djelu darežljivosti kojemu služimo - na slavu samoga Gospodina i na našu želju
19Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
20kako bismo izbjegli da nas tko ne prekori zbog ovog obilja kojim raspolažemo.
20Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
21Doista, revno nastojimo oko dobra ne samo pred Gospodinom nego i pred ljudima.
21Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
22Šaljemo s njima i našega brata koji je, kako smo u mnogome često iskusili, gorljiv, a sada je još mnogo gorljiviji zbog velikoga pouzdanja u vas.
22Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
23A Tito? Moj je drug i suradnik za vas. A braća naša? Poslanici su crkava, slava Kristova.
23Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
24Pružite im dakle pred crkvama dokaz svoje ljubavi i toga da se s pravom vama ponosimo.
24Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.