1Pavao, Silvan i Timotej Crkvi Solunjana u Bogu Ocu našemu i Gospodinu Isusu Kristu.
1Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
2Milost vam i mir od Boga Oca i Gospodina Isusa Krista!
2Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3Zahvaljivati moramo Bogu uvijek za vas, braćo, kao što dolikuje jer izvanredno raste vaša vjera i množi se ljubav svakoga od vas prema drugima,
3Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
4tako da se mi sami po crkvama Božjim vama ponosimo zbog vaše postojanosti i vjere u svim progonstvima i nevoljama koje podnosite.
4Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
5One su najava pravednog Suda Božjega: da ćete se naći dostojni kraljevstva Božjega za koje i trpite.
5Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
6Jer pravo je da Bog vašim mučiteljima mukom,
6Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
7a vama, mučenima, zajedno s nama spokojem uzvrati kad se Gospodin Isus objavi s nama, zajedno s anđelima svoje moći,
7na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
8u ognju žarkome i osveti se onima koji ne poznaju Boga i ne pokoravaju se evanđelju Gospodina našega Isusa.
8na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
9Oni će biti kažnjeni vječnom propašću, daleko od lica Gospodnjega i od slave njegova veličanstva,
9Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu,
10kada - u onaj Dan - dođe da se proslavi u svojim svetima i da se prodiči u svima koji povjerovaše. Jer povjerovalo se svjedočanstvu našemu među vama.
10wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
11Zato i molimo uvijek za vas da vas Bog učini dostojnima poziva i snažno dovede do punine svako vaše nastojanje oko dobra i djelo vaše vjere
11Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
12te da se proslavi ime Gospodina našega Isusa u vama i vi u njemu - po milosti Boga našega i Gospodina Isusa Krista.
12Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.