Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

1

1Paulius, Dievo valia pašauktas Kristaus Jėzaus apaštalas, ir brolis Sostenas­
1Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2Dievo bažnyčiai Korinte, pašventintiems Kristuje Jėzuje, pašauktiesiems šventiesiems su visais, kurie šaukiasi mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus vardo kiekvienoje vietoje pas jus ir pas mus.
2tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3Malonė ir ramybė jums nuo Dievo, mūsų Tėvo, ir Viešpaties Jėzaus Kristaus!
3Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4Aš nuolat dėkoju dėl jūsų Dievui už Dievo malonę, suteiktą jums per Jėzų Kristų,
4Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5kad per Jį praturtėjote viskuo­ visokiu žodžiu ir visokiu pažinimu,­
5Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6ir Kristaus liudijimas jumyse tapo tvirtas.
6kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7Todėl jums nestinga jokios dovanos laukiant, kada apsireikš mūsų Viešpats Jėzus Kristus,
7hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8kuris ir sutvirtins jus iki galo, kad būtumėte nekalti mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus dieną.
8Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9Ištikimas yra Dievas, kuris jus pašaukė į savo Sūnaus, mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus, bendravimą.
9Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10Broliai, Viešpaties Jėzaus Kristaus vardu maldauju jus, kad visi vienaip kalbėtumėte ir nebūtų tarp jūsų susiskaldymų, bet kad būtumėte tobulai suvienyti vienos minties ir vieno sprendimo.
10Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11Mat Chlojės namiškiai pranešė man apie jus, mano broliai, kad tarp jūsų esama kivirčų.
11Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12Turiu omenyje tai, kad iš jūsų yra tokių, kurie sako: “Aš esu Pauliaus”, “aš­Apolo”, “aš­Kefo”, “o aš­Kristaus”.
12Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, "Mimi ni wa Paulo," mwingine: "Mimi ni wa Apolo," mwingine: "Mimi ni wa Kefa," na mwingine: "Mimi ni wa Kristo,".
13Argi Kristus padalytas? Argi Paulius buvo už jus nukryžiuotas? Argi vardan Pauliaus buvote pakrikštyti?
13Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14Ačiū Dievui, kad pas jus nieko daugiau nekrikštijau, išskyrus Krispą ir Gajų,
14Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15kad niekas nesakytų, jog aš krikštiju savo paties vardu.
15Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16Tiesa, pakrikštijau taip pat Stepono namus, o daugiau nežinau, ar ką pakrikštijau.
16(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17Kristus nesiuntė manęs krikštyti, bet Evangelijos skelbti,­ne žodžių išmintimi, kad Kristaus kryžius netaptų bereikšmis.
17Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18Mat žodis apie kryžių tiems, kurie žūsta, yra kvailystė, bet mums, išgelbėtiems, jis yra Dievo jėga.
18Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19Nes parašyta: “Sunaikinsiu išmintingųjų išmintį, niekais paversiu protingųjų išmanymą”.
19Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali."
20Kur išminčius? Kur Rašto žinovas? Kur šio amžiaus tyrinėtojas? Argi Dievas nepavertė šio pasaulio išminties kvailyste?
20Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
21Kadangi pasaulis išmintimi nepažino Dievo pagal Jo išmintį, tai Dievui patiko skelbimo kvailumu išgelbėti tuos, kurie tiki.
21Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22Žydai reikalauja ženklų, graikai ieško išminties,
22Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23bet mes skelbiame Kristų nukryžiuotąjį, kuris žydams yra papiktinimas, o pagonims­kvailystė.
23lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24Bet pašauktiesiems­tiek žydams, tiek graikams­skelbiame Kristų­Dievo jėgą ir Dievo išmintį.
24lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25Dievo kvailystė išmintingesnė už žmones ir Dievo silpnybė stipresnė už žmones.
25Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26Juk jūs matote savo pašaukimą, broliai,­nedaug tarp jūsų kūno atžvilgiu išmintingų, nedaug galingų, nedaug kilmingų.
26Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27Bet Dievas išsirinko, kas pasaulyje kvaila, kad sugėdintų išminčius. Dievas išsirinko, kas pasaulyje silpna, kad sugėdintų, kas galinga.
27Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28Ir kas pasaulyje žemos kilmės, kas paniekinta, kas yra niekas, Dievas išsirinko, kad niekais paverstų tai, kas laikoma kažkuo,­
28Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29kad joks kūnas nesigirtų prieš Dievą.
29Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30Jo dėka jūs esate Kristuje Jėzuje, kuris mums tapo išmintimi iš Dievo, teisumu, pašventinimu ir atpirkimu,
30Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31kad, kaip parašyta: “Kas giriasi, tesigiria Viešpačiu”.
31Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana."