1Ir aš, broliai, kai pas jus lankiausi, atėjau ne su gražbyliavimu ar išmintimi skelbti jums Dievo liudijimo.
1Ndugu, mimi nilipokuja kwenu sikuwahubiria siri ya ujumbe wa Mungu kwa ufasaha wa lugha, au kwa hekima ya binadamu.
2Nes aš nusprendžiau tarp jūsų nežinoti nieko, išskyrus Jėzų Kristų, ir Tą nukryžiuotą.
2Nilipokuwa kwenu niliamua kutojua chochote kile isipokuwa tu kumjua Yesu Kristo; naam, Kristo aliyesulubiwa.
3Aš buvau pas jus silpnas, išsigandęs ir labai drebėjau.
3Nilipokuwa kwenu nilikuwa dhaifu, natetemeka kwa hofu nyingi.
4Mano kalba ir skelbimas pasižymėjo ne įtikinančiais žmogiškos išminties žodžiais, bet Dvasios ir jėgos parodymu,
4Hotuba zangu na mahubiri yangu sikuyatoa kwa maneno ya kuvutia na ya hekima, bali kwa uthibitisho mwingi na nguvu ya Roho.
5kad ir jūsų tikėjimas remtųsi ne žmogiška išmintimi, bet Dievo jėga.
5Nilifanya hivyo kusudi imani yenu ipate kutegemea nguvu ya Mungu, na si hekima ya binadamu.
6Tiesa, tarp subrendusiųjų mes skelbiame išmintį, tačiau tai išmintis ne šio pasaulio ir ne šio pasaulio valdovų, kurie pranyks.
6Hata hivyo, sisi tunatumia lugha ya hekima kwa wale waliokomaa kiroho; lakini hekima hiyo si ya hapa duniani, wala si ya watawala wa dunia hii ambao wako katika mkumbo wa kupotea.
7Mes skelbiame paslaptingą ir paslėptą Dievo išmintį, kurią Dievas nuo amžių paskyrė mums išaukštinti,
7Hekima tunayotumia ni hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichika, ambayo Mungu aliiazimia tangu mwanzo kwa ajili ya utukufu wetu.
8kurios nepažino jokie šio pasaulio valdovai, nes, jei būtų pažinę, nebūtų šlovės Viešpaties nukryžiavę.
8Ni hekima ambayo watawala wa dunia hii hawakuielewa; maana wangalielewa, hawangalimsulubisha Bwana wa utukufu.
9Bet skelbiame, kaip parašyta: “Ko akis neregėjo, ko ausis negirdėjo, kas žmogui į širdį neatėjo, tai paruošė Dievas tiems, kurie Jį myli”.
9Lakini, ni kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mambo ambayo jicho halijapata kuyaona wala sikio kuyasikia, mambo ambayo binadamu hajapata kuyafikiria moyoni, hayo ndiyo Mungu aliyowatayarishia wale wampendao."
10Dievas mums tai apreiškė per savo Dvasią, nes Dvasia visa ištiria, net Dievo gelmes.
10Hayo ndiyo mambo Mungu aliyotufunulia kwa njia ya Roho wake. Maana Roho huchunguza kila kitu hata mambo ya ndani kabisa ya Mungu.
11Kas iš žmonių žino, kas yra žmogaus, jei ne paties žmogaus dvasia? Taip pat niekas nežino, kas yra Dievo, tik Dievo Dvasia.
11Nani awezaye kujua mambo ya ndani ya mtu isipokuwa roho yake mtu huyo? Hali kadhalika, hakuna ajuaye mambo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu.
12O mes gavome ne pasaulio dvasią, bet Dvasią iš Dievo, kad suvoktume, kas mums Dievo dovanota.
12Sasa sisi hatukuipokea roho ya ulimwengu, bali tumepokea Roho atokaye kwa Mungu ili atuwezeshe kujua yale tuliyojaliwa na Mungu.
13Apie tai ir kalbame ne žodžiais, kurių moko žmogiškoji išmintis, bet tais, kurių moko Šventoji Dvasia,dvasinius dalykus gretindami su dvasiniais.
13Basi sisi twafundisha, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya binadamu, bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua mambo ya kiroho kwa walio na huyo Roho.
14Bet sielinis žmogus nepriima to, kas yra iš Dievo Dvasios, nes jam tai kvailystė; ir negali suprasti, nes tai dvasiškai vertinama.
14Mtu wa kidunia hapokei mambo ya Roho wa Mungu. Kwake mtu huyo mambo hayo ni upumbavu mtupu; yanapita akili yake; maana yanaweza tu kutambuliwa kwa msaada wa Roho.
15O dvasinis žmogus gali spręsti apie viską, bet niekas negali spręsti apie jį.
15Lakini mtu aliye na huyo Roho anaweza kubainisha ubora wa kila kitu, naye mwenyewe hahukumiwi na mtu mwingine.
16“Kas gi suvokė Viešpaties mintį, kad galėtų Jį pamokyti?” O mes turime Kristaus protą.
16Maandiko yasema: "Nani awezaye kuifahamu akili ya Bwana? Nani awezaye kumshauri?" Lakini sisi tunayo akili ya Kristo.