Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

3

1Aš, broliai, negalėjau kalbėti jums kaip dvasiniams, bet kaip kūniškiems, kaip kūdikiams Kristuje.
1Ndugu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu mlio na huyo Roho. Nilipaswa kusema nanyi kama watu wa kidunia, kama watoto wachanga katika maisha ya Kikristo.
2Maitinau jus pienu, ne tvirtu maistu, kurio jūs negalėjote priimti. Net ir dabar negalite,
2Ilinibidi kuwalisheni kwa maziwa, na si kwa chakula kigumu, kwani hamkuwa tayari kukipokea. Hata sasa hamko tayari.
3nes tebesate kūniški. Jeigu tarp jūsų pavydas, nesantaika ir susiskaldymai,­argi nesate kūniški? Argi nesielgiate grynai žmogiškai?
3Maana bado mu watu wa kidunia. Je, si kweli kwamba bado uko wivu na magombano kati yenu? Mambo hayo yanaonyesha wazi kwamba ninyi bado ni watu wa kidunia, mnaishi mtindo wa kidunia.
4Kol vienas sako: “Aš­Pauliaus”, kitas: “Aš­Apolo”,­argi nesate kūniški?
4Mmoja wenu anaposema, "Mimi ni wa Paulo", na mwingine, "Mimi ni wa Apolo", je, hiyo haionyeshi kwamba mnaishi bado kama watu wa dunia hii tu?
5Kas yra Paulius? Kas yra Apolas? Tarnai, kurių dėka įtikėjote ir kurie tarnavo, kiek Viešpats kiekvienam skyrė.
5Apolo ni nani? na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi tu ambao tuliwaleteeni ninyi imani. Kila mmoja wetu anafanya kazi aliyopewa na Bwana.
6Aš sodinau, Apolas laistė, o Dievas augino.
6Mimi nilipanda mbegu, Apolo akamwagilia maji; lakini aliyeiotesha mbegu ni Mungu.
7Todėl nieko nereiškia nei sodintojas, nei laistytojas, bet Dievas­augintojas.
7Wa maana si yule aliyepanda mbegu, au yule aliyemwagilia maji; wa maana ni Mungu aliyeiwezesha mbegu kuota.
8Kas sodina ir kas laisto, yra viena, ir kiekvienas gaus savąjį užmokestį pagal savo triūsą.
8Yule aliyepanda na yule aliyemwagilia maji wote ni sawa, ingawa kila mmoja atapokea tuzo lake kufuatana na jitihada yake mwenyewe.
9Mes juk esame Dievo bendradarbiai, o jūs­Dievo dirva, Dievo statinys.
9Maana sisi ni ndugu, wafanyakazi pamoja na Mungu; na ninyi ni shamba lake; ninyi ni jengo lake.
10Pagal Dievo man suteiktą malonę aš, kaip išmintingas statybos vadovas, padėjau pamatą, o kitas stato ant jo. Tegul kiekvienas žiūri, kaip stato.
10Kwa msaada wa neema aliyonipa Mungu, nimefaulu, kama mwashi stadi mwenye busara, kuweka msingi ambao juu yake mtu mwingine anajenga. Basi, kila mmoja awe mwangalifu jinsi anavyojenga juu yake.
11Juk niekas negali dėti kito pamato, kaip tik tą, kuris jau padėtas, kuris yra Jėzus Kristus.
11Hakuna mtu awezaye kuweka msingi mwingine badala ya ule uliokwisha wekwa, yaani Yesu Kristo.
12Jei kas stato ant šio pamato iš aukso, sidabro, brangakmenių, medžio, šieno ar šiaudų,­
12Juu ya msingi huo mtu anaweza kujenga kwa dhahabu, fedha au mawe ya thamani; anaweza kutumia miti, majani au nyasi.
13kiekvieno darbas išaiškės. Todėl, kad diena jį atskleis, nes tai bus atskleista ugnimi ir ugnis ištirs, koks kieno darbas.
13Iwe iwavyo, ubora wa kazi ya kila mmoja utaonekana wakati Siku ile ya Kristo itakapoifichua. Maana, Siku hiyo itatokea na moto, na huo moto utaipima na kuonyesha ubora wake.
14Jei kieno statybos darbas išliks, tas gaus užmokestį.
14Ikiwa alichojenga mtu juu ya huo msingi kitaustahimili huo moto, atapokea tuzo;
15O kieno darbas sudegs, tas turės nuostolį, bet jis pats bus išgelbėtas, tačiau kaip per ugnį.
15lakini kama alichojenga kitaunguzwa, basi, atapoteza tuzo lake; lakini yeye mwenyewe ataokolewa kana kwamba ameponyoka kutoka motoni.
16Ar nežinote, kad jūs esate Dievo šventykla ir Dievo Dvasia gyvena jumyse?
16Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu, na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17Jei kas Dievo šventyklą niokoja, tą Dievas sunaikins, nes Dievo šventykla šventa, ir toji šventykla­tai jūs!
17Basi, mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu; maana hekalu la Mungu ni takatifu, na hekalu hilo ni ninyi wenyewe.
18Tegul niekas savęs neapgaudinėja. Jei kas tarp jūsų tariasi esąs išmintingas šiame pasaulyje, tepasidaro kvailas, kad būtų išmintingas.
18Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.
19Šio pasaulio išmintis Dievo akyse yra kvailystė, nes parašyta: “Jis sugauna protinguosius jų gudrybėje”.
19Maana, hekima ya kidunia ni upumbavu mbele ya Mungu. Kwani Maandiko Matakatifu yasema: "Mungu huwanasa wenye hekima katika ujanja wao."
20Ir vėl: “Viešpats žino išminčių mintis, kad jos tuščios”.
20Na tena: "Bwana ajua kwamba mawazo ya wenye hekima hayafai."
21Tad niekas tenesididžiuoja žmonėmis! Nes viskas yra jūsų:
21Basi, mtu asijivunie watu. Maana kila kitu ni chenu.
22ar Paulius, ar Apolas, ar Kefas, ar pasaulis, ar gyvenimas, ar mirtis, ar dabartis, ar ateitis,­viskas yra jūsų,
22Paulo, Apolo na Kefa, ulimwengu, maisha na kifo; mambo ya sasa na ya baadaye, yote ni yenu.
23bet jūs patys­Kristaus, o Kristus­Dievo.
23Lakini ninyi ni wa Kristo naye Kristo ni wa Mungu.