1Tegul kiekvienas laiko mus Kristaus tarnais ir Dievo paslapčių tvarkytojais.
1Mtu na atuone sisi kuwa ni watumishi wa Kristo tuliokabidhiwa siri za mungu.
2O iš tvarkytojų reikalaujama, kad būtų ištikimi.
2Kinachotakiwa kwa yeyote yule aliyekabidhiwa kazi ni kuwa mwaminifu.
3Man mažai rūpi, ką jūs ar žmonių teismas spręstų apie mane. Ir aš pats savęs neteisiu.
3Kwangu mimi si kitu nikihukumiwa na ninyi, au na mahakama ya kibinadamu; wala sijihukumu.
4Nors nematau nieko netinkamo savyje, bet tuo dar nesu išteisintas. Mano teisėjas yra Viešpats.
4Dhamiri yangu hainishtaki kwa jambo lolote, lakini hiyo haionyeshi kwamba sina lawama. Bwana ndiye anayenihukumu.
5Todėl neteiskite nieko prieš laiką, iki ateis Viešpats, kuris nušvies, kas tamsoje paslėpta, ir atskleis širdžių sumanymus. Tada kiekvienam teks pagyrimas iš Dievo.
5Basi, msihukumu kabla ya wakati wake acheni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayafichua mambo ya giza yaliyofichika, na kuonyesha wazi nia za mioyo ya watu. Ndipo kila mmoja atapata sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.
6Visa tai, broliai, jūsų labui pritaikiau sau ir Apolui, kad iš mūsų pasimokytumėte negalvoti daugiau negu parašyta ir kad nepasipūstumėte vienas prieš kitą.
6Ndugu, hayo yote niliyosema juu ya Apolo na juu yangu, ni kielelezo kwenu: kutokana na mfano wangu mimi na Apolo nataka mwelewe maana ya msemo huu: "Zingatieni yaliyoandikwa." Kati yenu pasiwe na mtu yeyote anayejivunia mtu mmoja na kumdharau mwingine.
7Kas gi tave išskiria iš kitų? Ir ką gi turi, ko nebūtum gavęs? O jei esi gavęs, tai ko didžiuojies, lyg nebūtum gavęs?
7Nani amekupendelea wewe? Una kitu gani wewe ambacho hukupewa? Na ikiwa umepewa, ya nini kujivunia kana kwamba hukukipewa?
8Jūs jau esate sotūs, jau turtingi, jau pradėjote be mūsų karaliauti! O, kad jūs iš tikrųjų karaliautumėte, kad ir mes galėtume kartu karaliauti!
8Haya, mmekwisha shiba! Mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme bila ya sisi! Naam, laiti mngekuwa kweli watawala, ili nasi pia tuweze kutawala pamoja nanyi.
9Man atrodo, kad Dievas mums, apaštalams, paskyrė paskutiniąją vietą, tarsi mirčiai pasmerktiems. Mes tapome reginys pasauliui, angelams ir žmonėms.
9Nafikiri Mungu ametufanya sisi mitume tuwe watu wa mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kuuawa, maana tumekuwa tamasha mbele ya ulimwengu wote, mbele ya malaika na watu.
10Mes kvaili dėl Kristaus, o jūs išmintingi Kristuje. Mes silpni, o jūs stiprūs; jūs gerbiami, o mes niekinami.
10Sisi ni wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye busara katika kuungana na Kristo! Sisi ni dhaifu, ninyi ni wenye nguvu. Ninyi mnaheshimika, sisi tunadharauliwa.
11Iki šios valandos alkstame ir trokštame, esame nuogi ir mušami, be pastogės
11Mpaka dakika hii, sisi tuna njaa na kiu, hatuna nguo, twapigwa makofi, hatuna malazi.
12ir vargstame, darbuodamiesi savo rankomis. Keikiamilaiminame, persekiojamikenčiame,
12Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;
13piktžodžiaujamimaloniai atsakome. Iki šiol esame laikomi pasaulio sąšlavomis, visų atmatomis.
13tukisingiziwa, tunajibu kwa adabu. Mpaka sasa tumetendewa kama uchafu wa dunia; na kwa kila mtu sisi ni takataka!
14Tai rašau, ne norėdamas jus gėdinti, bet įspėdamas kaip mylimus vaikus.
14Siandiki mambo haya kwa ajili ya kuwaaibisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwafundisheni watoto wangu wapenzi.
15Nors turėtumėte tūkstančius auklėtojų Kristuje, bet neturėsite daug tėvų, nes Evangelija aš pagimdžiau jus Kristuje Jėzuje.
15Maana hata kama mnao maelfu ya walezi katika maisha yenu ya Kikristo, baba yenu ni mmoja tu, kwani katika maisha ya Kikristo mimi ndiye niliyewazaeni kwa kuihubiri Habari Njema.
16Todėl raginu jus: būkite mano sekėjai!
16Kwa hiyo, nawasihi: fuateni mfano wangu.
17Tuo tikslu ir pasiunčiau pas jus Timotiejų, kuris yra mano mylimas sūnus ir ištikimas Viešpatyje. Jis jums primins mano kelius Kristuje, kaip aš mokau visur, kiekvienoje bažnyčioje.
17Ndiyo maana nimemtuma Timetheo kwenu. Yeye ni mtoto wangu mpenzi na mwaminifu katika Bwana. Atawakumbusheni njia ninayofuata katika kuishi maisha ya Kikristo; njia ninayofundisha kila mahali katika makanisa yote.
18Kai kurie pasipūtė, tartum neketinčiau pas jus atvykti.
18Baadhi yenu wameanza kuwa na majivuno wakidhani kwamba sitakuja tena kwenu.
19Jei Viešpats panorės, veikiai atvyksiu pas jus ir patikrinsiu ne pasipūtusių kalbas, bet jėgą.
19Lakini, Bwana akipenda, nitakuja kwenu upesi; na hapo ndipo nitakapojionea mwenyewe, sio tu kile wanachoweza kusema hao wenye majivuno, bali pia kila wanachoweza kufanya.
20Nes Dievo karalystė yra ne kalboje, bet jėgoje.
20Maana Utawala wa Mungu si shauri la maneno matupu, bali ni nguvu.
21Ko norite? Ar kad ateičiau pas jus su lazda, ar su meile ir romumo dvasia?
21Mnapendelea lipi? Nije kwenu na fimbo, ama nije na moyo wa upendo na upole?