Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

16

1Pavedu jums mūsų sesę Febę, kuri yra Kenchrėjos bažnyčios tarnautoja;
1Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2priimkite ją Viešpatyje, kaip pridera šventiesiems, ir padėkite jai, prireikus jūsų paramos, nes ir ji yra padėjusi daug kam ir man pačiam.
2Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
3Sveikinkite Priscilę ir Akvilą, mano bendradarbius Kristuje Jėzuje,
3Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
4kurie guldė galvas, gelbėdami mano gyvybę. Jiems dėkoju ne aš vienas, bet ir visos pagonių bažnyčios.
4Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
5Taip pat pasveikinkite bažnyčią, kuri yra jų namuose. Sveikinkite mano mylimąjį Epenetą­pirmąjį vaisių Kristui Azijoje.
5Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
6Sveikinkite Mariją, kuri daug darbavosi dėl mūsų.
6Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7Sveikinkite Androniką ir Juniją, mano tautiečius, kalėjusius su manimi; jie žymūs tarp apaštalų ir anksčiau už mane yra Kristuje.
7Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
8Sveikinkite mano mylimąjį Viešpatyje Ampliatą.
8Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
9Sveikinkite mūsų bendradarbį Kristuje Urboną ir mano mylimąjį Stachį.
9Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
10Sveikinkite Apelį, išbandytą Kristuje. Sveikinkite tuos, kurie iš Aristobulo namų.
10Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11Sveikinkite mano tautietį Erodioną. Sveikinkite tuos iš Narcizo šeimynos, kurie yra Viešpatyje.
11Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
12Sveikinkite Trifeną ir Trifosą, besidarbuojančias Viešpatyje. Sveikinkite mieląją Persidę, kuri daug darbavosi Viešpatyje.
12Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
13Sveikinkite išrinktąjį Viešpatyje Rufą, taip pat ir jo bei mano motiną.
13Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
14Sveikinkite Asinkritą, Flegontą, Hermį, Patrobą, Hermą ir su jais esančius brolius.
14Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15Sveikinkite Filologą ir Juliją, Nerėją ir jo seserį, Olimpą ir visus šventuosius, kurie yra su jais.
15Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
16Sveikinkite vieni kitus šventu pabučiavimu. Jus sveikina visos Kristaus bažnyčios.
16Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
17Prašau jus, broliai, įsidėmėti tuos, kurie kelia susiskaldymus bei papiktinimus, prieštaraudami mokymui, kurio jūs išmokote. Venkite jų!
17Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
18Tokie žmonės netarnauja mūsų Viešpačiui Jėzui Kristui, bet savo pilvui. Saldžiomis ir pataikūniškomis kalbomis jie apgaudinėja paprastųjų širdis.
18maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
19Jūsų klusnumas žinomas visur. Todėl džiaugiuosi jumis, ir linkiu, kad būtumėte išmintingi gėriui ir neišmanūs blogiui.
19Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
20O ramybės Dievas sutryps šėtoną po jūsų kojomis greitu laiku. Mūsų Viešpaties Jėzaus malonė tebūnie su jumis! Amen.
20Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
21Jus sveikina mano bendradarbis Timotiejus ir mano tautiečiai Liucijus, Jasonas ir Sosipatras.
21Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
22Aš, Tercijus, šio laiško surašytojas, sveikinu jus Viešpatyje.
22Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
23Jus sveikina Gajus, mano ir visos bažnyčios šeimininkas. Jus sveikina Erastas, miesto iždininkas, ir mano brolis Kvartas.
23Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
24Mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė tebūnie su jumis visais. Amen.
24Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
25Tam, kuris gali jus sustiprinti pagal mano Evangeliją ir Jėzaus Kristaus skelbimą, pagal apreiškimo paslaptį, nutylėtą nuo pasaulio pradžios,
25Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita.
26bet dabar atskleistą ir pranašų raštais amžinojo Dievo įsakymu paskelbtą visoms tautoms, kad jos paklustų tikėjimui,­
26Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii.
27vienam išmintingajam Dievui per Jėzų Kristų šlovė per amžius! Amen.
27Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina.