1Mes, stiprieji, turime pakęsti silpnųjų silpnybes ir ne sau pataikauti.
1Sisi tulio imara katika imani tunapaswa kuwasaidia wale walio dhaifu wayakabili matatizo yao. Tusijipendelee sisi wenyewe tu.
2Kiekvienas iš mūsų tebūna malonus artimui jo labui ir pažangai.
2Kila mmoja wetu anapaswa kumpendeza jirani yake kwa wema ili huyo apate kujijenga katika imani.
3Nes ir Kristus gyveno ne savo malonumui, bet, kaip parašyta: “Tave keikiančiųjų keiksmai krito ant manęs”.
3Maana Kristo hakujipendelea mwenyewe; ila alikuwa kama yasemavyo Maandiko: "Kashfa zote walizokutolea wewe zimenipata mimi."
4O visa, kas anksčiau parašyta, mums pamokyti parašyta, kad ištverme ir Raštų paguoda turėtume viltį.
4Maana yote yalioandikwa yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi ili kutokana na saburi na faraja tupewayo na Maandiko hayo Matakatifu tupate kuwa na matumaini.
5Ištvermės ir paguodos Dievas teduoda jums tarpusavyje būti vienos minties, Kristaus Jėzaus pavyzdžiu,
5Mungu aliye msingi wa saburi na faraja yote, awajalieni ninyi kuwa na msimamo mmoja kufuatana na mfano wake Kristo Yesu,
6kad sutartinai vienu balsu šlovintumėte Dievą, mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Tėvą.
6ili ninyi nyote, kwa nia moja na sauti moja, mumtukuze Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
7Todėl priimkite vienas kitą, kaip ir Kristus jus priėmė į Dievo šlovę.
7Basi, karibishaneni kwa ajili ya utukufu wa Mungu kama naye Kristo alivyowakaribisheni.
8Aš sakau: Kristus tapo apipjaustytųjų tarnas dėl Dievo tiesos, kad patvirtintų tėvams suteiktus pažadus
8Maana, nawaambieni Kristo aliwatumikia Wayahudi apate kuonyesha uaminifu wa Mungu, na zile ahadi Mungu alizowapa babu zetu zipate kutimia;
9ir kad pagonys šlovintų Dievą už Jo gailestingumą, kaip parašyta: “Todėl išpažinsiu Tave tarp pagonių, Tavo vardui giedosiu”.
9ili nao watu wa mataifa mengine wapate kumtukuza Mungu kwa sababu ya huruma yake. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa sababu hiyo, nitakusifu miongoni mwa watu wa mataifa. Nitaziimba sifa za jina lako."
10Ir vėl sakoma: “Džiaukitės, pagonys, kartu su Jo tauta”.
10Tena Maandiko yasema: "Furahini, enyi watu wa mataifa; furahini pamoja na watu wake."
11Ir dar: “Girkite Viešpatį, visi pagonys, šlovinkite Jį visos tautos”.
11Na tena: "Enyi mataifa yote, msifuni Bwana; enyi watu wote, msifuni."
12Ir Izaijas vėl sako: “Bus Jesės šaknis, Tas, kuris pakils valdyti pagonių, ir Juo vilsis pagonys”.
12Tena Isaya asema: "Atatokea mtu katika ukoo wa Yese, naye atawatawala watu wa mataifa; nao watamtumainia."
13Tegul vilties Dievas pripildo jus dideliu džiaugsmu ir tikėjimo ramybe, kad Šventosios Dvasios jėga būtumėte pertekę vilties.
13Basi, Mungu aliye msingi wa matumaini, awajazeni furaha yote na amani kutokana na imani yenu; tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
14Aš, mano broliai, esu įsitikinęs, kad jūs esate kupini gerumo, pilni visokio pažinimo ir galite vieni kitus perspėti.
14Ndugu zangu, mimi binafsi nina hakika kwamba ninyi pia mmejaa wema, elimu yote, na mnaweza kushauriana ninyi kwa ninyi.
15Parašiau jums, broliai, kai kur kiek per drąsiai, norėdamas jums priminti, kad dėl Dievo man suteiktos malonės
15Lakini nimewaandikia hapa na pale katika barua hii bila woga, nipate kuwakumbusheni juu ya mambo fulani. Nimefanya hivyo kwa sababu ya neema aliyonijalia Mungu
16turiu būti pagonims Jėzaus Kristaus tarnas ir skelbti Dievo Evangeliją, kad pagonių auka taptų priimtina, Šventosios Dvasios pašventinta.
16ya kuwa mtumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa. Ni jukumu langu la kikuhani kuihubiri Habari Njema ya Mungu ili watu wa mataifa mengine wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, dhabihu iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.
17Taigi Kristuje Jėzuje aš galiu pasigirti Dievo darbais.
17Kwa hiyo, nikiwa nimeungana na Kristo Yesu, naweza kujivunia huduma yangu kwa ajili ya Mungu.
18Juk nedrįsčiau ko nors pasakoti, ko Kristus nebūtų per mane nuveikęs, kad pagonys paklustų žodžiu ir darbu;
18Sithubutu kusema kitu kingine chochote isipokuwa tu kile ambacho Kristo Yesu amekifanya kwa kunitumia mimi ili watu wa mataifa wapate kutii. Amefanya hivyo kwa maneno na vitendo,
19galingais ženklais ir stebuklais, Dievo Dvasios jėga nuo Jeruzalės ir aplinkui, iki Ilyrijos, aš iki galo paskelbiau Kristaus Evangeliją.
19kwa nguvu ya miujiza na maajabu, na kwa nguvu ya Roho wa Mungu. Basi, kwa kusafiri kila mahali, tangu kule Yerusalemu mpaka Iluriko, nimeihubiri kikamilifu Habari Njema ya Kristo.
20Be to, kad nestatyčiau ant svetimų pamatų, aš stengiausi skelbti Evangeliją ne ten, kur Kristaus vardas jau pagarsintas,
20Nia yangu imekuwa daima kuihubiri Habari Njema popote pale ambapo jina la Kristo halijapata kusikika, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine.
21bet, kaip parašyta: “Pamatys tie, kuriems nebuvo apie Jį skelbta, ir supras tie, kurie nebuvo girdėję”.
21Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Watu wote ambao hawakuambiwa habari zote wataona; nao wale ambao hawajapata kusikia, wataelewa."
22Todėl aš ir buvau daug kartų sutrukdytas pas jus atvykti.
22Kwa sababu hiyo nilizuiwa mara nyingi kuja kwenu.
23Bet dabar, neturėdamas vietos šiuose kraštuose ir daugel metų trokšdamas atvykti pas jus,
23Lakini maadam sasa nimemaliza kazi yangu pande hizi, na kwa kuwa kwa miaka mingi nimekuwa na nia kubwa ya kuja kwenu,
24aš apsilankysiu, kai keliausiu į Ispaniją. Turiu vilties, keliaudamas pro šalį, išvysti jus ir tikiuosi, kad jūs palydėsite mane, prieš tai nors kiek pasimėgavusį bendravimu su jumis.
24natumaini kufanya hivyo sasa. Ningependa kuwaoneni nikiwa safarini kwenda Spania na kupata msaada wenu kwa safari hiyo baada ya kufurahia kuwa kwa muda pamoja nanyi.
25Bet dabar vykstu į Jeruzalę šventiesiems patarnauti.
25Lakini, kwa sasa nakwenda kuwahudumia watu wa Mungu kule Yerusalem.
26Mat Makedonijai ir Achajai buvo malonu padaryti rinkliavą Jeruzalės šventųjų beturčiams.
26Maana makanisa ya Makedonia na Akaya yemeamua kutoka mchango wao kuwasaidia watu wa Mungu walio maskini huko Yerusalem.
27Joms tai labai patiko, ir iš tikro jos yra jų skolininkės. Jeigu pagonys tapo jų dvasinių gėrybių dalininkais, tai jų pareigapatarnauti medžiaginėmis gėrybėmis.
27Wao wenyewe wameamua kufanya hivyo; lakini, kwa kweli, hilo ni jukumu lao kwa hao. Maana, ikiwa watu wa mataifa mengine wameshiriki baraka za kiroho za Wayahudi, wanapaswa nao pia kuwahudumia Wayahudi katika mahitaji yao ya kidunia.
28Taigi, baigęs šį reikalą ir jiems saugiai atidavęs, kas surinkta, keliausiu pro jus į Ispaniją.
28Nitakapokwisha tekeleza kazi hiyo na kuwakabidhi mchango huo uliokusanywa kwa ajili yao, nitawatembeleeni ninyi nikiwa safarini kwenda Spania.
29Ir aš esu tikras, kad atvyksiu pas jus Kristaus Evangelijos palaiminimo pilnatvėje.
29Najua ya kuwa nikija kwenu nitawaletea wingi wa baraka za Kristo.
30Todėl maldauju jus, broliai, dėl Viešpaties Jėzaus Kristaus ir Dvasios meilės, kad jūs kartu su manimi kovotumėte už mane maldose Dievui,
30Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa ajili ya upendo uletwao na Roho, mniunge mkono kwa kuniombea kwa Mungu.
31kad būčiau išgelbėtas nuo netikinčiųjų Judėjoje, kad mano paslauga Jeruzalei būtų priimtina šventiesiems,
31Ombeni nipate kutoka salama miongoni mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, nayo huduma yangu huko Yerusalem ipate kukubaliwa na watu wa Mungu walioko huko.
32ir kad pagal Dievo valią atvykčiau pas jus su džiaugsmu ir atsigaivinčiau drauge su jumis.
32Hivyo, Mungu akipenda, nitaweza kuja kwenu na moyo wa furaha, nikapumzike pamoja nanyi.
33Ramybės Dievas tebūnie su jumis visais! Amen.
33Mungu aliye chanzo cha amani na awe nanyi nyote! Amina!