Lithuanian

Swahili: New Testament

Romans

14

1Silpno tikėjimo žmogų priimkite, bet venkite ginčų dėl skirtingų nuomonių.
1Mkaribisheni kwenu mtu aliye dhaifu, lakini msibishane naye juu ya mawazo yake binafsi.
2Vienas įsitikinęs, kad galima viską valgyti, o silpnas valgo tik daržoves.
2Watu huhitilafiana: mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu; lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula tu mboga za majani.
3Kuris valgo, teneniekina nevalgančio, o kuris nevalgo, teneteisia valgančio, nes Dievas jį priėmė.
3Mtu ambaye hula kila kitu asimdharau yule ambaye hawezi kula kila kitu; naye ambaye hula tu mboga za majani asimhukumu anayekula kila kitu, maana Mungu amemkubali.
4Kas tu toks, kad drįsti teisti kito tarną?! Ar jis stovi, ar krenta­tai savajam Viešpačiui. Bet jis stovės, nes Dievas turi galią jį išlaikyti.
4Wewe ni nani hata uthubutu kumhukumu mtumishi wa mwingine? Akisimama au akianguka ni shauri la Bwana wake; naam, atasimama imara, maana Bwana anaweza kumsimamisha.
5Vienas išskiria vieną dieną iš kitų dienų, o kitam jos visos vienodos. Kiekvienas tebūna įsitikinęs pagal savo išmanymą.
5Mtu anaweza kufikiria siku fulani kuwa ya maana zaidi kuliko nyingine; mtu mwingine aweza kuzifikiria siku zote kuwa sawa. Kila mmoja na afuate msimamo wa akili yake.
6Tas, kuris išskiria dieną, daro tai Viešpačiui, ir tas, kuris neišskiria dienos, nesilaiko jos Viešpačiui. Tas, kuris valgo­valgo Viešpačiui, nes jis dėkoja Dievui, o tas, kuris nevalgo­nevalgo Viešpačiui ir dėkoja Dievui.
6Anayeadhimisha siku fulani anaadhimisha siku hiyo kwa ajili ya kumtukuza Mungu; naye anayekula chakula fulani anafanya hivyo kwa kumtukuza Bwana maana anamshukuru Mungu. Kadhalika naye anayeacha kula chakula fulani anafanya hivyo kwa ajili ya kumtukuza Bwana, naye pia anamshukuru Mungu.
7Nė vienas iš mūsų negyvena sau ir nė vienas sau nemiršta.
7Maana hakuna mtu yeyote miongoni mwetu aishiye kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna anayekufa kwa ajili yake mwenyewe
8Jei mes gyvename, gyvename Viešpačiui, ir jeigu mirštame, Viešpačiui mirštame. Todėl, ar mes gyvename, ar mirštame,­ esame Viešpaties.
8maana tukiishi twaishi kwa ajili ya Bwana; tukifa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi, kama tukiishi au tukifa, sisi ni mali yake Bwana.
9Nes dėl to Kristus ir mirė, ir prisikėlė, ir atgijo, kad būtų ir mirusiųjų, ir gyvųjų Viešpats.
9Maana Kristo alikufa, akafufuka ili wapate kuwa Bwana wa wazima na wafu.
10Tai kodėl gi tu teisi savo brolį? Arba kodėl niekini savo brolį? Juk mes visi stosime prieš Kristaus teismo krasę.
10Kwa nini, basi wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
11Parašyta: “Kaip Aš gyvas,­sako Viešpats,­prieš mane suklups kiekvienas kelis, ir kiekvienos lūpos išpažins Dievą”.
11Maana Maandiko yanasema: "Kama niishivyo, asema Bwana kila mtu atanipigia magoti, na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu."
12Taigi kiekvienas iš mūsų duos Dievui apyskaitą už save.
12Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja yake mbele ya Mungu.
13Tad liaukimės teisti vieni kitus. Verčiau nuspręskime neduoti broliui akstino nupulti ar pasipiktinti.
13Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu yetu au kumsababisha aanguke katika dhambi.
14Žinau ir esu įsitikinęs Viešpatyje Jėzuje, kad nieko nėra savaime netyro. Bet tam, kas mano esant netyrų dalykų, tam jie netyri.
14Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.
15Jei tavo brolis įsižeidžia dėl maisto, tu jau nebesielgi iš meilės. Savo maistu nežlugdyk to, už kurį mirė Kristus!
15Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na mapendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!
16Jūsų gėris tegul nebūna akstinas piktžodžiauti.
16Basi, msikubalie kitu mnachokiona kuwa kwenu ni kitu chema kidharauliwe.
17Dievo karalystė nėra valgymas ir gėrimas, bet teisumas, ramybė ir džiaugsmas Šventojoje Dvasioje.
17Maana Utawala wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.
18Kas taip Kristui tarnauja, tas priimtinas Dievui ir vertas žmonių pritarimo.
18Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.
19Tad siekime to, kas atneša ramybę ir pasitarnauja tarpusavio ugdymui.
19Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.
20Negriauk Dievo darbo dėl maisto! Nors viskas tyra, bet yra bloga žmogui, kuris valgo kitų papiktinimui.
20Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.
21Gera yra nevalgyti mėsos, negerti vyno ir vengti visko, kas tavo brolį piktina, žeidžia ar silpnina.
21Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.
22Turi tikėjimą? Turėk jį sau, prieš Dievą. Laimingas tas, kuris nesmerkia savęs už tai, ką pasirenka.
22Basi, shikilia unachoamini kati yako na Mungu wako. Heri mtu yule ambaye, katika kujiamulia la kufanya, haipingi dhamiri yake.
23O kas valgo abejodamas, tas smerktinas, nes valgo ne iš įsitikinimo. Visa, kas daroma ne iš įsitikinimo, yra nuodėmė.
23Lakini mtu anayeona shaka juu ya chakula anachokula, anahukumiwa kama akila, kwa sababu msimamo wa kitendo chake haumo katika imani. Na, chochote kisicho na msingi wake katika imani ni dhambi.