Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

14

1Siekite meilės ir trokškite dvasinių dovanų, ypač, kad pranašautumėte.
1Jitahidini kuwa na upendo. Vilevile fanyeni bidii ya kupata vipaji vingine vya kiroho, hasa kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu.
2Kas kalba kalbomis, ne žmonėms kalba, bet Dievui; niekas jo nesupranta, nes jis dvasioje kalba paslaptis.
2Mwenye kunena lugha ngeni hasemi na watu bali anasema na Mungu. Yeye hunena kwa nguvu ya Roho mambo yaliyofichika.
3Bet kas pranašauja, tas kalba žmonių ugdymui, paraginimui ir paguodai.
3Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, husema na watu kwa ajili ya kuwajenga, kuwafariji na kuwatia moyo.
4Kas kalba kalbomis, pats save ugdo, o kas pranašauja­ugdo bažnyčią.
4Mwenye kunena lugha ngeni anajijenga mwenyewe. Lakini mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, analijenga kanisa.
5Aš norėčiau, kad jūs visi kalbėtumėte kalbomis, bet būtų geriau, jei pranašautumėte, nes kas pranašauja, yra didesnis už tą, kuris kalba kalbomis, nebent pastarasis ir aiškintų, kad būtų ugdoma bažnyčia.
5Basi, ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha ngeni lakini ningependelea hasa muwe na kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, maana mtu mwenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, ni wa maana zaidi kuliko yule mwenye kusema lugha ngeni, isipokuwa tu kama yupo hapo mtu awezaye kuyafafanua hayo mambo asemayo, ili kanisa lipate kujengwa.
6Bet dabar, broliai, jei ateičiau pas jus, kalbėdamas kalbomis, kokia jums būtų nauda, jeigu neskelbčiau jums apreiškimo, pažinimo, pranašystės ar mokymo?
6Hivyo, ndugu zangu, kama nikija kwenu na kusema nanyi kwa lugha ngeni itawafaa nini? Haitawafaa chochote, isipokuwa tu kama nitawaelezeni ufunuo wa Mungu au ujuzi fulani au ujumbe wa Mungu au mafundisho fulani.
7Taip pat ir negyvi daiktai, skleidžiantys garsus, ar tai būtų fleita, ar kanklės, jei neduotų skirtingų garsų, iš ko pažintume, kas grojama ar skambinama?
7Ndivyo ilivyo kwa vyombo visivyo na uhai vyenye kutoa sauti kama vile filimbi au kinanda. Je, mtu anawezaje kuutambua wimbo unaochezwa kama vyombo hivyo havitoi sauti waziwazi vinapopigwa?
8Ir jeigu trimitas duotų neaiškų garsą, kas ruoštųsi į mūšį?
8La mgambo likilia bila kufuata taratibu zake, nani atajiweka tayari kwa vita?
9Tas pat ir su jumis. Jei kalbėsite nesuprantamus žodžius, kaip bus galima suprasti, ką sakote? Jūs kalbėsite vėjams!
9Hali kadhalika na ninyi, kama ulimi wenu hausemi kitu chenye kueleweka, nani ataweza kufahamu mnayosema? Maneno yenu yatapotea hewani.
10Kas žino, kiek daug yra įvairių kalbų pasaulyje, bet nė viena iš jų nėra bereikšmė.
10Zipo lugha mbalimbali ulimwenguni, na hakuna hata mojawapo isiyo na maana.
11Todėl jei nesuprantu kalbos prasmės, būsiu kalbėtojui svetimšalis, ir kalbėtojas bus man svetimšalis.
11Lakini ikiwa mimi sifahamu maana ya lugha asemayo mtu fulani, mimi ni mgeni kwake mtu huyo naye pia ni mgeni kwangu.
12Taigi ir jūs, karštai trokštantys dvasinių dovanų, siekite jų bažnyčios ugdymui, kad gausiai jų turėtumėte.
12Hali kadhalika na ninyi, maadam mna hamu ya kupata vipaji vya Roho, jitahidini hasa kujipatia vile vinavyosaidia kulijenga kanisa.
13Todėl, kas kalba kalbomis, tesimeldžia, kad galėtų aiškinti.
13Kwa hiyo, mwenye kunena lugha ngeni na aombe apate uwezo wa kuzifafanua.
14Nes jei meldžiuosi kalbomis, meldžiasi mano dvasia, bet protas lieka bevaisis.
14Maana, nikisali kwa lugha ngeni roho yangu ndiyo inayosali, lakini akili yangu hubaki bure.
15Ką gi tada daryti? Melsiuosi dvasia ir melsiuosi protu; giedosiu dvasia ir giedosiu protu.
15Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.
16Be to, jei tu laimini dvasia, kaip neišmanantis pasakys tavo padėkai “amen”, nesuprasdamas, ką tu kalbi?
16Ukimsifu Mungu kwa roho yako tu, atawezaje mtu wa kawaida aliye katika mkutano kuitikia sala yako ya shukrani kwa kusema: "Amina," kama haelewi unachosema?
17Juk tu gražiai dėkoji, tačiau kitas nėra ugdomas.
17Sala yako ya shukrani yaweza kweli kuwa bora, lakini huyo mwingine haitamfaidia.
18Dėkui mano Dievui, aš kalbu kalbomis daugiau už jus visus,
18Namshukuru Mungu kwamba mimi nasema kwa lugha ngeni zaidi kuliko ninyi nyote.
19vis dėlto bažnyčioje geriau pasakysiu penkis žodžius savo protu, kad pamokyčiau ir kitus, negu tūkstančius žodžių kalbomis.
19Lakini katika mikutano ya waumini napendelea zaidi kusema maneno matano yenye kueleweka ili niwafundishe wengine, kuliko kusema maneno elfu ya lugha ngeni.
20Broliai! Nebūkite vaikai išmanymu. Verčiau blogybe būkite kūdikiai, bet išmanymu­subrendę.
20Ndugu, msiwe kama watoto katika fikira zenu. Kuhusu uovu muwe kama watoto wachanga lakini katika kufikiri ni lazima muwe kama watu waliokomaa.
21Įstatyme parašyta: “Svetimomis kalbomis ir svetimųjų lūpomis Aš kalbėsiu šiai tautai, bet ir tada jie nepaklausys manęs”,­sako Viešpats.
21Imeandikwa katika Sheria: "Bwana asema hivi: Kwa njia ya wenye kunena lugha ngeni, na kwa midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, hata hivyo, hawatanisikiliza."
22Todėl kalbos yra ženklas ne tikintiems, bet netikintiems. O pranašavimas­ne netikintiems, bet tikintiems.
22Hivyo basi, kipaji cha kusema lugha ngeni ni ishara, si kwa ajili ya watu wenye imani, bali kwa ajili ya wale wasioamini; lakini kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni kwa ajili ya wale wanaoamini na si kwa ajili ya wasioamini.
23Juk jei susirinktų visa bažnyčia ir visi imtų kalbėti kalbomis, ir įeitų neišmanantys ar netikintys,­argi jie nesakytų, kad jūs išėję iš proto?
23Basi, kanisa lote linapokutana pamoja, na wote wakaanza kusema kwa lugha ngeni, kama wakija watu wa kawaida au wasioamini, je, hawatasema kwamba ninyi mna wazimu?
24Bet jeigu visi pranašautų ir įeitų netikintis ar neišmanantis, jis būtų visų apkaltintas ir visų atpažintas.
24Lakini, wote wakiwa wanautangaza ujumbe wa Mungu, akija mtu wa kawaida au asiyeamini, yote atakayosikia yatamhakikishia ubaya wake mwenyewe; yote atakayosikia yatamhukumu.
25Jo širdies paslaptys būtų atskleistos, ir jis, puolęs veidu žemėn, pagarbintų Dievą ir išpažintų: “Dievas iš tiesų yra tarp jūsų!”
25Siri za moyo wake zitafichuliwa, naye atapiga magoti na kumwabudu Mungu akisema: "Kweli Mungu yupo pamoja nanyi."
26Tad kaip bus, broliai? Kai susirenkate, kiekvienas turi giesmę ar pamokymą, ar kalbą, ar apreiškimą, ar aiškinimą. Tegul viskas tarnauja ugdymui.
26Ndugu, tuseme nini, basi? Mnapokutana pamoja, mmoja aimbe wimbo, mwingine atoe mafundisho, mwingine awe na ufunuo kutoka kwa Mungu, mwingine atumie kipaji cha kusema kwa lugha ngeni na mwingine afafanue yanayosemwa. Yote yawe kwa ajili ya kulijenga kanisa.
27Jei kalba kas kalbomis, tekalba du, daugiausia trys, paeiliui, o vienas tegul aiškina.
27Wakiwepo watu wenye vipaji vya kusema kwa lugha ngeni, waseme wawili au watatu, si zaidi, tena mmojammoja; na aweko mtu wa kufafanua yanayosemwa.
28Bet jeigu nėra aiškintojo, tegul tas bažnyčioje tyli ir tekalba tik sau ir Dievui.
28Lakini kama hakuna awezaye kufafanua, basi, mwenye kusema lugha ngeni anyamaze mkutanoni, aseme na nafsi yake mwenyewe na Mungu.
29Ir pranašai tekalba du ar trys, o kiti teapsvarsto.
29Kuhusu wale wenye kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu, waseme wawili au watatu, na wengine wayapime maneno yao.
30Bet jei kitam šalia sėdinčiam kas nors apreiškiama, pirmasis tenutyla.
30Ikiwa mmoja anaposema mwingine wa wasikilizaji amepata ufunuo kutoka kwa Mungu, basi, yule anayesema anyamaze.
31Nes jūs visi galite vienas po kito pranašauti, kad visi pasimokytų ir visi būtų paguosti.
31Maana nyote mwaweza kutangaza ujumbe wa Mungu, mmoja baada ya mwingine, ili nyote mpate kujifunza na kutiwa moyo.
32Pranašų dvasios yra paklusnios pranašams,
32Kipaji cha kutangaza ujumbe wa Mungu ni lazima kitawaliwe na huyo mwenye hicho kipaji.
33nes Dievas nėra sumaišties, bet ramybės Dievas,­kaip ir visose šventųjų bažnyčiose.
33Maana Mungu si Mungu wa fujo, ila wa amani.
34Jūsų moterys bažnyčiose tetyli, nes joms neleidžiama kalbėti, jos turi būti klusnios, kaip sako ir įstatymas.
34Kama ilivyo desturi katika makanisa yote ya watu wa Mungu, wanawake wakae kimya katika mikutano ya waumini. Hawana ruhusa kusema; ila wawe watii kama isemavyo Sheria.
35Ir jeigu jos nori ko nors išmokti, tepasiklausia namie savo vyro, nes moterims gėdinga bažnyčioje kalbėti.
35Ikiwa wanayo maswali ya kuuliza, wawaulize waume zao nyumbani, maana ni aibu kwa mwanamke kusema katika mikutano ya waumini.
36Argi iš jūsų išėjo Dievo žodis? Ar tik jus vienus pasiekė?
36Je, mnadhani neno la Mungu limetoka kwenu ninyi au kwamba limewajieni ninyi peke yenu?
37Jei kas mano esąs pranašas ar dvasinis žmogus, tegu pripažįsta, kad tai, ką jums rašau, yra Viešpaties įsakymai.
37Kama mtu yeyote anadhani kwamba yeye ni mjumbe wa Mungu au kwamba anacho kipaji cha Roho, na ajue kwamba haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.
38Bet jei kas neišmano, tegul neišmano.
38Lakini mtu asiyetambua hayo, basi, mtu asimjali mtu huyo.
39Todėl, broliai, karštai trokškite pranašauti ir nedrauskite kalbėti kalbomis.
39Hivyo basi, ndugu zangu, mnapaswa kuwa na hamu ya kutangaza ujumbe wa Mungu; lakini msimkataze mtu kusema kwa lugha ngeni.
40Tebūnie viskas daroma padoriai ir tvarkingai.
40Lakini yote yafanyike kwa heshima na kwa utaratibu.