1Broliai, aiškinu jums Evangeliją, kurią jums paskelbiau, kurią jūs ir priėmėte ir kurioje stovite,
1Sasa ndugu, napenda kuwakumbusha ile Habari Njema niliyowahubirieni nanyi mkaipokea na kusimama imara ndani yake.
2ir kuria esate išgelbėti,jeigu jūs laikotės to žodžio, kurį jums paskelbiau; kitaip jūs įtikėjote veltui.
2Kwa njia yake mnaokolewa, ikiwa mnayazingatia maneno niliyowahubirieni, na kama kuamini kwenu hakukuwa bure.
3Pirmiausia jums perdaviau tai, ką pats gavau: kad Kristus numirė už mūsų nuodėmes pagal Raštus;
3Mimi niliwakabidhi ninyi mambo muhimu sana ambayo mimi niliyapokea: kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kufuatana na Maandiko Matakatifu;
4ir kad Jis buvo palaidotas, ir kad prisikėlė trečią dieną pagal Raštus;
4kwamba alizikwa, akafufuka siku ya tatu kama ilivyoandikwa;
5ir kad Jis pasirodė Kefui, po to dvylikai.
5kwamba alimtokea Kefa, na baadaye aliwatokea wale kumi na wawili.
6Po to Jis pasirodė iš karto daugiau nei penkiems šimtams brolių, kurių daugumas tebegyvena iki šiol, o kai kurie yra užmigę.
6Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
7Po to Jis pasirodė Jokūbui, paskui visiems apaštalams.
7Baadaye alimtokea Yakobo kisha akawatokea mitume wote.
8O visų paskiausiai, lyg ne laiku gimusiam, Jis pasirodė ir man.
8Baada ya wote, akanitokea hata mimi, mimi niliyekuwa kama mtu aliyezaliwa kabla ya wakati.
9Juk aš esu mažiausias iš apaštalų, nevertas vadintis apaštalu, nes persekiojau Dievo bažnyčią.
9Maana mimi ni mdogo kabisa miongoni mwa mitume na wala sistahili kuitwa mtume, kwa sababu nililidhulumu kanisa la Mungu.
10Bet Dievo malone esu, kas esu, ir Jo malonė man neliko bergždžia, bet aš darbavausi daug daugiau už juos visus, nors ne aš, bet Dievo malonė, esanti su manimi.
10Lakini, kwa neema yake Mungu, nimekuwa kama nilivyo. Na neema yake kwangu haikuwa bure. Mimi nimefanya kazi kuliko wote; si mimi hasa, ila ni neema ya Mungu ifanyayo kazi pamoja nami.
11Taigi ar aš, ar jie,taip mes skelbiame, ir taip jūs įtikėjote.
11Lakini hata hivyo, iwe wao ndio wahubirio au mimi nihubiriye, haidhuru, hiki ndicho tunachuhubiri, na hiki ndicho mnachoamini.
12Jeigu apie Kristų skelbiama, kad Jis buvo prikeltas iš numirusių, tad kaip kai kurie iš jūsų sako, kad nėra mirusiųjų prisikėlimo?!
12Sasa, maadam inahubiriwa kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, baadhi yenu wanawezaje kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu?
13Jeigu nėra mirusiųjų prisikėlimo, tai Kristus nebuvo prikeltas.
13Kama hakuna ufufuo wa wafu, basi, Kristo naye hakufufuka;
14O jei Kristus nebuvo prikeltas, tai tuščias mūsų skelbimas ir tuščias jūsų tikėjimas.
14na kama Kristo hakufufuka, basi mahubiri yetu hayana maana na imani yenu haina maana.
15Ir mes tada liekame melagingi Dievo liudytojai, nes liudijome apie Dievą, kad Jis prikėlė Kristų, kurio Jis nėra prikėlęs, jeigu mirusieji neprisikelia.
15Zaidi ya hayo sisi tungekuwa mashahidi wa uongo mbele ya Mungu, maana tulisema kwamba Mungu alimfufua Kristo kutoka wafu na kumbe yeye hakumfufua--kama ni kweli kwamba wafu hawafufuliwi.
16Nes jei mirusieji neprisikelia, tada ir Kristus nebuvo prikeltas.
16Maana, ikiwa ni kweli kwamba wafu hawafufuki, basi naye Kristo hakufufuka.
17O jei Kristus nebuvo prikeltas, tai jūsų tikėjimas tuščias; jūs dar tebesate savo nuodėmėse.
17Na kama Kristo hakufufuliwa, basi, imani yenu ni ya bure; mngali bado katika dhambi zenu.
18Tuomet ir užmigusieji Kristuje yra žuvę.
18Zaidi ya hayo, wale wote waliokufa wakiwa wameungana na Kristo wamepotea kabisa.
19Ir jei vien tik šiame gyvenime mes viliamės Kristumi, tai mes esame labiausiai apgailėtini iš visų žmonių.
19Kama matumaini yetu katika Kristo yanahusu tu maisha haya ya sasa, basi, sisi ni watu wa kusikitikiwa zaidi kuliko wengine wote duniani.
20Bet dabar Kristus yra prikeltas iš numirusiųpirmasis iš užmigusiųjų.
20Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka wafu, limbuko lao wale waliolala katika kifo.
21Kaip per žmogųmirtis, taip per žmogų ir mirusiųjų prisikėlimas.
21Maana kama vile kifo kilivyoletwa duniani na mtu mmoja, vivyo hivyo nako kufufuka kutoka wafu kumesababishwa na mtu mmoja.
22Kaip Adome visi miršta, taip Kristuje visi bus atgaivinti,
22Kama vile watu wote wanavyokufa kwa kujiunga na Adamu, vivyo hivyo wote watafufuliwa kwa kuungana na Kristo.
23tačiau kiekvienas pagal savo eilę: Kristuspirmasis, vėliaupriklausantys Kristui Jo atėjimo metu.
23Lakini kila mmoja kwa mpango wake: Kristo kwanza, halafu wale walio wake Kristo wakati Kristo atakapokuja.
24Po to bus galas, kai Jis perduos karalystę Dievui Tėvui, sunaikinęs visas kunigaikštystes, visas valdžias ir jėgas.
24Baada ya hayo, mwisho utafika wakati ambapo Kristo atamkabidhi Mungu Baba Utawala, baada ya kufutilia mbali kila tawala na mamlaka na nguvu.
25Nes Jis turi valdyti, kol paguldys visus priešus po savo kojomis.
25Maana Kristo sharti atawale mpaka Mungu atakapowashinda adui zake na kuwaweka chini ya miguu yake.
26Kaip paskutinis priešas bus sunaikinta mirtis.
26Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni kifo.
27Nes “Jis visa paklojo Jam po kojų”. Bet kai Jis sako, kad visa paklota, tai savaime suprantama, kad išskyrus Tą, kuris Jam visa paklojo.
27Maana, Maandiko yasema: "Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake." Lakini, Maandiko yanaposema: "Vitu vyote vimewekwa chini ya miguu yake avitawale" ni dhahiri kwamba Mungu haingii katika kundi hilo la vitu, maana yeye ndiye anayeviweka vitu hivyo chini ya Kristo.
28Kai Jam bus visa pajungta, tada ir pats Sūnus nusilenks Tam, kuris viską Jam pajungė, kad Dievas būtų viskas visame kame.
28Lakini vitu vyote vitakapowekwa chini ya Utawala wa Kristo, ndipo naye Mwana atakapojiweka chini ya Mungu, aliyeweka vyote chini ya Utawala wake; ili Mungu atawale juu ya vyote.
29Kita vertus, ką darys tie, kuriuos krikštija už mirusiuosius? Jei iš viso mirusieji neprisikels, tai kam gi jie krikštijami už mirusiuosius?
29Kama hakuna ufufuo, je watu wale wanaobatizwa kwa ajili ya wafu wanatumainia kupata nini? Kama wafu hawafufuliwi, ya nini kubatizwa kwa ajili yao?
30Ir kodėl ir mes kas valandą esame pavojuje?
30Na sisi, ya nini kujitia hatarini kila saa?
31Prisiekiu savo pasididžiavimu jumis, broliai, mūsų Viešpatyje Jėzuje Kristuje, jog aš kasdien mirštu!
31Ndugu, mimi nakikabili kifo kila siku! Fahari niliyo nayo juu yenu katika kuungana na Kristo Yesu Bwana wetu inanifanya nitangaze jambo hili.
32Jei grynai kaip žmogus kovojau Efeze su laukiniais žvėrimis, tai kokia man iš to nauda? Jeigu mirusieji neprisikels, tai “valgykime ir gerkime, nes rytoj mirsime”.
32Kama kusudi langu lingalikuwa la kibinadamu tu, kule kupigana kwangu na wanyama wakali hapa Efeso kungalinifaa kitu gani? Kama wafu hawafufuki, basi, "Tule na tunywe, maana kesho tutakufa."
33Neapsirikite: “Blogos draugijos gadina gerus papročius!”
33Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
34Pabuskite teisumui ir nenuodėmiaukite, nes kai kurie iš jūsų nepažįsta Dievo. Tai sakau jūsų gėdai.
34Amkeni! Anzeni kuishi vema, na acheni kutenda dhambi. Baadhi yenu hawamjui Mungu kabisa. Hii nawaambieni, ni aibu kubwa kwenu!
35Bet gal kas paklaus: “Kaip bus prikelti mirusieji? Su kokiu kūnu jie pasirodys?”
35Lakini mtu anaweza kuuliza: "Wafu watafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani wakati watakapokuja tena?"
36Kvaily! Ką tu pasėji, neatgyja, jei prieš tai nenumiršta.
36Hayo ni maswali ya kijinga! Ukipanda mbegu, isipokufa kwanza haitaota.
37Ir ką besėtum, tu sėji ne būsimąjį kūną, bet pliką grūdą, sakysime, kviečių ar kitokių javų.
37Unachopanda ni mbegu tu, labda ya ngano au nafaka nyingine, na si mmea mzima ambao hutokea baadaye.
38Tuo tarpu Dievas duoda jam kūną tokį, koks Jam patinka, ir kiekvienai sėklai jos kūną.
38Mungu huipa hiyo mbegu mwili anaoutaka mwenyewe; kila mbegu hupata mwili wake wa pekee.
39Ne visi kūnai yra vienodi. Vienoks žmonių kūnas, kitoks gyvulių, kitoks žuvų ir kitoks paukščių.
39Miili ya viumbe vyote si sawa. Miili ya binadamu ni ya namna moja, ya wanyama ni ya namna nyingine, ya ndege ni ya namna nyingine na miili ya samaki pia ni ya namna nyingine.
40Taip pat yra dangaus kūnai ir žemės kūnai, bet vienokia dangaus kūnų šlovė ir kitokia žemės kūnų.
40Iko miili ya mbinguni na miili ya duniani; uzuri wa miili ya mbinguni ni mwingine, na na uzuri wa miili ya duniani ni mwingine.
41Vienokia yra saulės šlovė, kitokia šlovė mėnulio ir dar kitokia šlovė žvaigždžių. Ir žvaigždė nuo žvaigždės skiriasi šlove.
41Uko uzuri wa jua, wa mwezi na wa nyota; hata nyota nazo huhitilafiana kwa uzuri.
42Taip ir su mirusiųjų prisikėlimu. Sėjamas gendantis kūnas, prikeliamas negendantis.
42Ndivyo ilivyo kuhusu ufufuo wa wafu. Kama vile mbegu, mwili huzikwa ardhini ukiwa katika hali ya kuharibika, lakini hufufuliwa katika hali ya kutoharibika.
43Sėjamas negarbingas, prikeliamas šlovingas. Sėjamas silpnas, prikeliamas galingas.
43Huzikwa katika hali duni, hufufuliwa katika hali tukufu; huzikwa katika hali dhaifu, hufufuliwa ukiwa wenye nguvu.
44Sėjamas sielinis kūnas, prikeliamas dvasinis kūnas. Yra sielinis kūnas ir yra dvasinis kūnas.
44Unapozikwa ni mwili wa kawaida, unapofufuliwa ni mwili wa kiroho. Kuna mwili wa kawaida na kutakuwa na mwili wa kiroho.
45Taip ir parašyta: “Pirmasis žmogus Adomas tapo gyva siela”; paskutinysis Adomasgyvybę teikiančia dvasia.
45Maana Maandiko yasema: "Mtu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe mwenye uhai;" lakini adamu wa mwisho ni Roho awapaye watu uzima.
46Bet ne dvasinis pirmiau, o sielinis, ir tik po to dvasinis.
46Lakini unaotangulia kuwako si ule mwili wa kiroho, ila ule mwili wa kawaida kisha ule mwili wa kiroho.
47Pirmasis žmogusiš žemės, žemiškas; antrasis žmogusViešpats iš dangaus.
47Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, alitoka ardhini; mtu wa pili alitoka mbinguni.
48Koks buvo žemiškasis, tokie yra ir žemiškieji, o koks yra dangiškasis, tokie yra ir dangiškieji.
48Wote walio wa dunia wako kama huyo mtu aliyeumbwa kwa udongo; wale walio wa mbinguni wako kama yule aliyetoka mbinguni.
49Ir kaip nešiojame žemiškojo atvaizdą, taip nešiosime ir dangiškojo atvaizdą.
49Kama vile tulivyofanana na yule aliyeumbwa kwa udongo, vivyo hivyo tutafanana na huyohuyo aliyetoka mbinguni.
50Bet aš jums, broliai, sakau, kad kūnas ir kraujas nepaveldės Dievo karalystės, ir kas genda, nepaveldės to, kas negenda.
50Basi, ndugu, nasema hivi: kile kilichofanywa kwa mwili na damu hakiwezi kuushiriki Ufalme wa Mungu; na chenye kuharibika hakiwezi kuwa na hali ya kutoharibika.
51Aš jums atskleidžiu paslaptį: ne visi užmigsime, bet visi būsime pakeisti,
51Sikilizeni, nawaambieni siri: sisi hatutakufa sote, ila sote tutageuzwa
52staiga, viena akimirka, skambant paskutiniam trimitui. Trimitas nuskambės, ir mirusieji bus prikelti negendantys, o mes būsime pakeisti.
52wakati wa mbiu ya mwisho, kwa nukta moja, kufumba na kufumbua. Maana mbiu itakapolia, wafu watafufuliwa katika hali ya kutoweza kufa tena, na sisi tutageuzwa.
53Nes šis gendantis turi apsivilkti negendamybe, ir šis marus apsivilkti nemarybe.
53Maana ni lazima kila kiharibikacho kijivalie hali ya kutoharibika, mwili uwezao kufa ujivalie hali ya kutokufa.
54Kada šis gendantis apsivilks negendamybe ir šis marusis apsivilks nemarybe, tada išsipildys užrašytas žodis: “Pergalė prarijo mirtį!
54Basi, mwili huu wenye kuharibika utakapojivalia hali ya kutoharibika, na kile chenye kufa kitakapojivalia hali ya kutokufa, hapo ndipo litakapotimia lile neno lililoandikwa: "Kifo kimeangamizwa ushindi umekamilika!"
55Kurgi, mirtie, tavo geluonis? Kurgi, mirtie, tavo pergalė?”
55"Kifo, ushindi wako uko wapi? Uwezo wako wa kuumiza uko wapi?"
56Mirties geluonis yra nuodėmė, o nuodėmės jėgaįstatymas.
56Ukali wa kifo hutokana na dhambi, nayo dhambi hupata nguvu yake katika Sheria.
57Bet dėkui Dievui, kuris duoda mums pergalę per mūsų Viešpatį Jėzų Kristų!
57Lakini tumshukuru Mungu anayetupatia ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58Todėl, mano mylimieji broliai, būkite tvirti, nepajudinami, visada gausūs Viešpaties darbais, žinodami, kad jūsų triūsas ne veltui Viešpatyje.
58Basi, ndugu zangu wapenzi, simameni imara na thabiti. Endeleeni daima kuwa na bidii katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi mnayofanya katika utumishi wa Bwana haitapotea bure.