Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Corinthians

16

1Su rinkliava šventiesiems darykite taip, kaip nurodžiau Galatijos bažnyčioms.
1Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2Pirmąją savaitės dieną kiekvienas iš jūsų teatideda pagal tai, kiek turi, kad rinkliavos neprasidėtų man atvykus.
2Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3Atvykęs pasiųsiu į Jeruzalę žmones, kuriuos jūs nutarsite esant tinkamus, kad jie su palydimaisiais laiškais nugabentų jūsų dovaną.
3Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
4Jei pasirodytų tinkama ir man keliauti, tai jie vyks kartu su manimi.
4Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5Atvyksiu pas jus, perėjęs Makedoniją. Mat per Makedoniją eisiu,
5Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia--maana nataraji kupitia Makedonia.
6o pas jus, galimas daiktas, pabūsiu arba ir peržiemosiu, kad jūs mane palydėtumėte, kai vyksiu toliau.
6Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7Nenoriu dabar su jumis susitikti prabėgomis. Tikiuosi, jei Viešpats leis, kurį laiką pasilikti pas jus.
7Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
8Bet Efeze išbūsiu iki Sekminių.
8Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9Mat man yra atvertos plačios durys našiam darbui, ir priešininkų daug.
9Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10Ir jeigu atvyks Timotiejus, žiūrėkite, kad jis gyventų pas jus be baimės, nes jis dirba Viešpaties darbą kaip ir aš.
10Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11Taigi tegul niekas jo neniekina. Išlydėkite jį su ramybe, kad atvyktų pas mane, nes laukiu jo su broliais.
11Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12O dėl brolio Apolo, tai aš didžiai troškau, kad jis su broliais keliautų pas jus, bet jis niekaip nenori šiuo metu. Bet atvyks, radęs tinkamą laiką.
12Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13Budėkite, tvirtai stovėkite tikėjime, elkitės vyriškai, būkite stiprūs!
13Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
14Viską, ką darote, darykite su meile.
14Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15Prašau jūsų, broliai (jūs pažįstate Stepono namus: jie yra Achajos pirmatikiai ir atsidavę tarnauti šventiesiems),
15Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16kad jūs taip pat paklustumėt tokiems žmonėms ir visiems, kurie mums padeda ir su mumis dirba.
16muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17Aš džiaugiuosi Stepono, Fortunato ir Achaiko apsilankymu. Jie man atstojo jus,
17Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18atgaivino mano ir jūsų dvasią. Todėl pripažinkite tokius žmones!
18Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19Jus sveikina Azijos bažnyčios. Karštai sveikina Viešpatyje Akvilas ir Priscilė kartu su bažnyčia, kuri jų namuose.
19Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20Jus sveikina visi broliai. Pasveikinkite vienas kitą šventu pabučiavimu.
20Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21Sveikinu jus savo, Pauliaus, ranka.
21Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22Jei kas nemyli Viešpaties Jėzaus Kristaus, tebūna prakeiktas! Mūsų Viešpatie, ateik!
22Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA--BWANA, njoo!
23Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė tebūna su jumis.
23Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24Mano meilė jums visiems Kristuje Jėzuje. Amen.
24Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.