Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Peter

2

1Taigi, atmetę visokį blogį, visokią klastą ir veidmainystes, pavyduliavimus ir visokias apkalbas,
1Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena.
2lyg naujagimiai trokškite tyro žodžio pieno, kad nuo jo augtumėte išgelbėjimui,
2Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
3jeigu tikrai paragavote, koks Viešpats yra maloningas.
3Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mmegundua kwamba Bwana ni mwema."
4Ženkite prie Jo, gyvojo akmens, tiesa, žmonių atmesto, bet Dievo išrinkto, brangaus,
4Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule, na la thamani kubwa.
5ir patys, kaip gyvieji akmenys, statydinkitės į dvasinius namus, kad būtumėte šventa kunigystė ir atnašautumėte dvasines aukas, priimtinas Dievui per Jėzų Kristų.
5Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho, ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea dhabihu za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
6Todėl Rašte pasakyta: “Štai dedu Sione kertinį akmenį, rinktinį, brangų; ir kas tiki Jį, nebus sugėdintas”.
6Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Tazama! Naweka huko sioni jiwe kuu la msingi, jiwe la thamani kubwa nililoliteua. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa."
7Tad jums, kurie tikite, Jis yra brangus, o nepaklūstantiems “tas statytojų atmestas akmuo tapo kertiniu akmeniu,
7Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, "Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi."
8suklupimo akmeniu ir papiktinimo uola”. Jie suklumpa, neklausydami žodžio; tam jie ir skirti.
8Tena Maandiko yasema: "Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu." Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.
9O jūs esate “išrinktoji giminė, karališkoji kunigystė, šventoji tauta, ypatingi žmonės, kad skelbtumėte dorybes” To, kuris pašaukė jus iš tamsybių į savo nuostabią šviesą.
9Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.
10Seniau ne tauta, dabar Dievo tauta, seniau neradę gailestingumo, dabar jį suradę.
10Wakati mmoja ninyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa ninyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmeipokea.
11Mylimieji, maldauju jus kaip svečius ir ateivius: susilaikykite nuo kūno geidulių, kurie kovoja prieš sielą.
11Wapenzi wangu, nawasihi ninyi kama wageni na wakimbizi hapa duniani! Achaneni na tamaa za mwili ambazo hupingana na roho.
12Jūsų elgesys tarp pagonių tebūna kilnus, kad jie už tai, už ką šmeižia jus kaip piktadarius, pamatę jūsų gerus darbus, imtų šlovinti Dievą aplankymo dieną.
12Mwenendo wenu kati ya watu wasiomjua Mungu unapaswa kuwa mwema kabisa, ili hata watakapowasingizieni kwamba mnatenda mabaya, waweze kutambua matendo yenu mema na hivyo wamtukuze Mungu Siku ya kuja kwake.
13Būkite klusnūs kiekvienai žmonių valdžiai dėl Viešpaties: tiek karaliui, kaip vyriausiajam,
13Basi, jiwekeni chini ya mamlaka yote ya kibinadamu, kwa ajili ya Bwana: utii kwa mfalme aliye mtawala mkuu,
14tiek valdytojams, kaip jo pasiųstiems bausti piktadarių ir pagirti geradarių.
14utii kwa wakuu wa mikoa ambao wameteuliwa naye kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema.
15Mat tokia Dievo valia, kad, darydami gera, nutildytumėte neprotingų žmonių neišmanymą.
15Maana Mungu anataka mweze kuyakomesha maneno ya kijinga ya watu wasio na akili kwa matendo mema mnayofanya.
16Elkitės kaip laisvi; ne kaip tie, kurie laisve pridengia blogį, bet kaip Dievo tarnai.
16Ishini kama watu huru; lakini msiutumie uhuru wenu kuuficha ubaya, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
17Gerbkite visus, mylėkite broliją, bijokite Dievo, gerbkite karalių.
17Waheshimuni watu wote, wapendeni ndugu zenu waumini, mcheni Mungu, mheshimuni mfalme.
18Tarnai, su visa baime būkite klusnūs šeimininkams, ne tik geriems ir švelniems, bet ir rūstiems.
18Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza.
19Girtina, jeigu kas dėl Dievo pažinimo pakelia skausmus, nekaltai kentėdamas.
19Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili.
20Menka garbė, jei jūs kantrūs, kai esate plakami už nusikaltimus. Bet kai esate kantrūs, darydami gera ir kentėdami, Dievo akyse tai verta pagyrimo.
20Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
21Juk jūs tam pašaukti; ir Kristus kentėjo už mus, palikdamas mums pavyzdį, kad eitumėte Jo pėdomis.
21Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili muufuate mwenendo wake.
22Jis “nepadarė nuodėmės, ir Jo lūpose nerasta klastos”.
22Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake.
23Šmeižiamas neatsakė tuo pačiu, kentėdamas negrasino, bet pavedė save Tam, kuris teisia teisingai.
23Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
24Jis pats savo kūne užnešė mūsų nuodėmes ant medžio, kad mirę nuodėmėms, gyventume teisumui. “Jo žaizdomis jūs buvote išgydyti”.
24Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.
25Jūs buvote tarsi klaidžiojančios avys, o dabar sugrįžote pas savo sielų Ganytoją ir Sargą.
25Ninyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.