1Jūs, žmonos, būkite klusnios savo vyrams, kad tie, kurie neklauso žodžio, ir be žodžio būtų laimėti savo žmonų elgesiu,
1Nanyi wake, jiwekeni chini ya mamlaka ya waume zenu, ili kama wako waume wowote wasioamini neno la Mungu, wapate kuamini kwa kuuona mwenendo wenu. Haitakuwa lazima kwenu kusema neno,
2matydami jūsų gyvenimo skaistumą ir dievobaimingumą.
2kwani wataona jinsi mwenendo wenu ulivyo safi na wa kumcha Mungu.
3Tegu puošia jus ne išorėsupinti plaukai, aukso papuošalai ar ištaigingi drabužiai,
3Katika kujipamba kwenu msitegemee mambo ya njenje, kama vile mitindo ya kusuka nywele, kujivalia vitu vya dhahabu na nguo maridadi.
4bet paslėptas širdies žmogus: nenykstančia, romia ir taikinga dvasia, kuri labai brangi Dievo akyse.
4Bali, uzuri wenu unapaswa kutokana na hali ya ndani ya utu wa kweli, uzuri usioharibika wa wema na utulivu wa roho, ambao ni wa thamani kubwa mbele ya Mungu.
5Juk kadaise taip ir puošdavosi šventos moterys, kurios turėjo viltį Dieve, būdamos klusnios savo vyrams.
5Ndivyo walivyojipamba hapo kale wanawake waadilifu waliomtumainia Mungu; walijiweka chini ya mamlaka ya waume zao.
6Taip Sara klausė Abraomo ir vadino jį viešpačiu. Jūs tapote jos dukterimis, darydamos gera ir nebijodamos jokių bauginimų.
6Sara kwa mfano alimtii Abrahamu na kumwita yeye bwana. Ninyi mmekuwa sasa binti zake kama mkitenda mema bila kuogopa tisho lolote.
7Ir jūs, vyrai, gyvenkite su žmonomis supratingai, kaip su silpnesniu indu, gerbdami jas kaip gyvenimo malonės bendrapaveldėtojas, kad jūsų maldos nebūtų trukdomos.
7Kadhalika nanyi waume, katika kuishi na wake zenu mnapaswa kutambua kwamba wao ni dhaifu na hivyo muwatendee kwa heshima; maana nao pia watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima anayowapeni Mungu. Hapo ndipo sala zenu hazitakataliwa.
8Galiausiai visi būkite vienminčiai, užjaučiantys kitus, mylintys brolius, gailestingi, draugiški.
8Mwisho nasema hivi: mnapaswa kuwa na moyo mmoja, na fikira moja; mnapaswa kupendana kidugu, kuwa wapole na wanyenyekevu ninyi kwa ninyi.
9Neatsilyginkite piktu už pikta ar keiksmu už keiksmą, bet, priešingai, laiminkite, žinodami, kad ir patys esate pašaukti paveldėti palaiminimo.
9Msiwalipe watu ovu kwa ovu, au tusi kwa tusi; bali watakieni baraka, maana ninyi mliitwa na Mungu mpate kupokea baraka.
10“Kas trokšta mylėti gyvenimą ir matyti gerų dienų, tepažaboja liežuvį nuo pikto ir lūpas nuo klastingų kalbų.
10Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Anayetaka kufurahia maisha, na kuona siku za fanaka, anapaswa kuacha kusema mabaya na kuacha kusema uongo.
11Tegu jis nusigręžia nuo pikto ir daro gera, teieško ramybės ir tesiveja ją.
11Na ajiepushe na uovu, atende mema, atafute amani na kuizingatia.
12Viešpaties žvilgsnis lydi teisiuosius, ir Jo ausys girdi jų maldas, bet Viešpaties veidasprieš darančius pikta”.
12Maana Bwana huwatazama kwa wema waadilifu na kuzisikiliza sala zao. Lakini huwapa kisogo watu watendao maovu."
13Kas gi jums pakenks, jei darysite gera?
13Ni nani atakayeweza kuwadhuru ninyi kama mkizingatia kutenda mema?
14Bet jei jums ir tektų kentėti už teisumą,jūs palaiminti! “Jų gąsdinimo neišsigąskite ir nesutrikite”.
14Lakini, hata kama itawapasa kuteseka kwa sababu ya kutenda mema, basi, mna heri. Msimwogope mtu yeyote, wala msikubali kutiwa katika wasiwasi.
15Šventu laikykite Viešpatį Dievą savo širdyse, visada pasiruošę atsakyti kiekvienam klausiančiam apie jumyse esančią viltį romiai ir pagarbiai,
15Lakini mtukuzeni Kristo kama Bwana mioyoni mwenu. Muwe tayari kumjibu yeyote atakayewaulizeni juu ya matumaini yaliyo ndani yenu,
16turėdami tyrą sąžinę, kad šmeižiantys jūsų gerą elgesį Kristuje liktų sugėdinti.
16lakini fanyeni hivyo kwa upole na heshima. Muwe na dhamiri njema, kusudi mnapotukanwa, wale wanaosema ubaya juu ya mwenendo wenu mwema kama Wakristo, waone aibu.
17Geriau, jei tokia būtų Dievo valia, kentėti už gerus darbus negu už piktus.
17Maana ni afadhali kuteseka kwa sababu ya kutenda mema, kama Mungu akipenda, kuliko kuteseka kwa sababu ya kutenda uovu.
18Ir Kristus vieną kartą kentėjo už nuodėmes, teisusis už neteisiuosius, kad mus nuvestų pas Dievą, beje, kūnu numarintas, bet atgaivintas Dvasia.
18Kwa maana Kristo mwenyewe alikufa kwa ajili ya dhambi zenu; alikufa mara moja tu na ikatosha, mtu mwema kwa ajili ya waovu, ili awapeleke ninyi kwa Mungu. Aliuawa kimwili lakini akafanywa hai kiroho;
19Ja Jis nužengė žemyn ir skelbė kalėjime esančioms dvasioms,
19na kwa maisha yake ya kiroho alikwenda kuwahubiria wale roho waliokuwa kifungoni.
20kurios kadaise buvo neklusnios, kai Nojaus dienomis Dievo kantrybė laukė, bestatant arką, kuria nedaugelis, tai yra aštuonios sielos, buvo išgelbėtos vandeniu.
20Hao ndio wale waliokataa kumtii Mungu alipowangoja kwa saburi wakati Noa alipokuwa anatayarisha ile safina. Ndani ya chombo hicho ni watu wachache tu, yaani watu wanane, waliookolewa majini,
21Ir mus dabar gelbsti tų įvykių vaizdinyskrikštas. Jis nėra kūno nešvaros nuplovimas, bet grynos sąžinės atsakas Dievui per prisikėlimą Jėzaus Kristaus,
21ambayo yalikuwa mfano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo si shauri la kuondoa uchafu mwilini, bali ni ahadi kwa Mungu inayofanyika katika dhamiri njema. Huwaokoeni kwa njia ya ufufuo wa Yesu Kristo,
22kuris, įžengęs į dangų, yra Dievo dešinėje; Jam yra pavaldūs angelai, valdžios ir jėgos.
22ambaye alikwenda mbinguni na sasa amekaa upande wa kulia wa Mungu, anatawala juu ya malaika, wakuu na wenye enzi.