1Pagaliau, broliai, prašome ir raginame jus Viešpatyje Jėzuje: jeigu išmokote iš mūsų, kaip privalote elgtis ir patikti Dievuitaip ir elkitės, darydami vis daugiau pažangos!
1Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
2Jūs juk žinote, kokių nurodymų jums davėme Viešpaties Jėzaus vardu.
2Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
3Nes tokia Dievo valiajūsų šventėjimas; kad susilaikytumėte nuo ištvirkavimo
3Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
4ir kiekvienas iš jūsų mokėtų saugoti savąjį indą šventume ir pagarboje,
4Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
5o ne aistringame geiduly, kaip pagonys, kurie nepažįsta Dievo;
5na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
6kad nė vienas neperžengtų ribų ir šituo dalyku neapgaudinėtų savo brolio, nes Dievas už visa tai keršija, kaip jau esame įspėję ir patvirtinę.
6Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
7Dievas nepašaukė mūsų nedorybei, bet šventumui.
7Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
8Todėl, kas tai atmeta, ne žmogų atmeta, bet Dievą, kuris ir davė mums savo Šventąją Dvasią.
8Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
9Apie brolišką meilę nebereikia jums rašyti, nes jūs patys esate Dievo išmokyti mylėti vienas kitą,
9Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
10ir jūs taip darote visiems broliams visoje Makedonijoje. Mes tik raginame jus, broliai, daryti vis daugiau pažangos,
10Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
11stengtis gyventi ramiai, atsidėti saviesiems reikalams ir dirbti savo rankomis, kaip jums įsakėme.
11Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
12Taip jūs deramai elgsitės pašalinių akyse ir jums nieko netrūks.
12Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
13Aš nenoriu, kad jūs, broliai, liktumėte nežinioje dėl užmigusiųjų ir nusimintumėte kaip kiti, kurie neturi vilties.
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
14Jeigu tikime, kad Jėzus mirė ir prisikėlė, tai Dievas ir tuos, kurie užmigo su Jėzumi, atves kartu su Juo.
14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15Ir tai jums sakome Viešpaties žodžiu, jog mes, gyvieji, išlikusieji iki Viešpaties atėjimo, nepralenksime užmigusiųjų.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
16Nes pats Viešpats nužengs iš dangaus, nuskambėjus paliepimui, arkangelo balsui ir Dievo trimitui, ir mirusieji Kristuje prisikels pirmiausia,
16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
17paskui mes, gyvieji, išlikusieji, kartu su jais būsime pagauti į debesis susitikti su Viešpačiu ore ir taip visuomet pasiliksime su Viešpačiu.
17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
18Todėl guoskite vieni kitus šiais žodžiais.
18Basi, farijianeni kwa maneno haya.