1Dėl valandos ir laiko, broliai, nėra reikalo jums rašyti.
1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2Jūs patys gerai žinote, kad Viešpaties diena užklups lyg vagis naktį.
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3Kai žmonės kalbės: “Ramybė ir saugumas”, tada juos ir ištiks netikėtas žlugimas, tarytum gimdymo skausmai nėščią moterį, ir jie niekur nepaspruks.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4Bet jūs, broliai, nesate tamsoje, kad toji diena jus užkluptų lyg vagis.
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5Juk jūs visi esate šviesos ir dienos vaikai. Mes nepriklausome nei nakčiai, nei tamsai.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6Todėl nemiegokime kaip kiti, bet budėkime ir būkime blaivūs!
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7Mat kas miega, miega naktį, ir kas pasigeria, pasigeria naktį.
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8O mes, priklausydami dienai, būkime blaivūs ir apsirengę tikėjimo bei meilės šarvus ir užsidėję išgelbėjimo vilties šalmą.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9Juk Dievas mus paskyrė ne rūstybei, bet kad įgytume išgelbėjimą per mūsų Viešpatį Jėzų Kristų,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10kuris mirė už mus, kad mes ar budėdami, ar miegodami gyventume kartu su Juo.
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11Todėl guoskite ir statydinkite vieni kitus, ką jūs ir darote.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12Prašome jus, broliai, gerbti tuos, kurie darbuojasi tarp jūsų, vadovauja jums Viešpatyje ir teikia jums pamokymų.
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13Be galo branginkite juos, mylėdami dėl jų darbo! Taikiai sugyvenkite tarpusavyje!
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14Raginame jus, broliai: įspėkite nedrausminguosius, padrąsinkite liūdinčiuosius, palaikykite silpnuosius, būkite kantrūs su visais!
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15Žiūrėkite, kad kas neatsimokėtų kam nors blogu už bloga, bet visada siekite daryti gera vieni kitiems ir visiems.
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16Visada džiaukitės,
16Furahini daima,
17be paliovos melskitės!
17salini kila wakati
18Už viską dėkokite, nes tokia Dievo valia jums Kristuje Jėzuje.
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19Negesinkite Dvasios!
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
20Neniekinkite pranašavimų!
20msidharau unabii.
21Visa ištirkite ir to, kas gera, laikykitės!
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22Susilaikykite nuo visokio blogio!
22na epukeni kila aina ya uovu.
23Pats ramybės Dievas iki galo jus tepašventina ir teišlaiko jūsų dvasią, sielą ir kūną nepeiktiną mūsų Viešpaties Jėzaus atėjimui.
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24Ištikimas yra Tas, kuris jus šaukia, Jis ir įvykdys!
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25Broliai, melskitės už mus!
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26Sveikinkite visus brolius šventu pabučiavimu.
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27Saikdinu jus Viešpačiu, kad šis laiškas būtų perskaitytas visiems šventiesiems broliams.
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28Mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė tebūna su jumis! Amen.
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.