1Paulius, Silvanas ir Timotiejus tesalonikiečių bažnyčiai Dieve, mūsų Tėve, ir Viešpatyje Jėzuje Kristuje.
1Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
2Malonė jums ir ramybė nuo Dievo, mūsų Tėvo, ir Viešpaties Jėzaus Kristaus!
2Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3Mes jaučiame pareigą visada dėkoti, broliai, už jus Dievui, ir tai teisinga, nes jūsų tikėjimas smarkiai auga ir jūsų visų meilė vienas kitam vis didėja.
3Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
4Todėl mes ir giriamės jumis Dievo bažnyčiosejūsų kantrybe bei tikėjimu visuose jūsų persekiojimuose ir sunkumuose, kuriuos jums tenka pakelti.
4Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
5O tai ir yra teisingo Dievo teismo požymis: jūs turite tapti verti Dievo karalystės, dėl kurios ir kenčiate.
5Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
6Teisinga iš Dievo pusės atmokėti jūsų prispaudėjams priespauda,
6Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
7o jums, prispaustiesiems,poilsiu drauge su mumis, kai iš dangaus apsireikš Viešpats Jėzus su savo galingais angelais.
7na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
8Liepsnojančioje ugnyje Jis atkeršys tiems, kurie nepažįsta Dievo ir nepaklūsta mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Evangelijai.
8na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
9Jie bus nubausti amžina pražūtimi ir atskirti nuo Viešpaties veido ir nuo Jo galybės šlovės
9Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu,
10tą dieną, kada Jis ateis, kad būtų pašlovintas savo šventuosiuose ir keliantis susižavėjimą visuose, kurie įtikėjo. Jūs irgi patikėjote mūsų liudijimu.
10wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
11Todėl mes nuolat meldžiamės už jus, kad mūsų Dievas padarytų jus vertus šio pašaukimo ir parodytų visą savo gerumą ir palankumą bei galingus tikėjimo darbus,
11Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
12kad mūsų Viešpaties Jėzaus vardas būtų pašlovintas jumyse, o jūs Jame, pagal mūsų Dievo ir Viešpaties Jėzaus Kristaus malonę.
12Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.