1Mes prašome jus, broliai, dėl mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus atėjimo ir dėl mūsų surinkimo pas Jį:
1Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
2nesiduokite taip greitai nukreipiami nuo sveiko proto ir įbauginami ar dvasia, ar žodžiu, ar neva mūsų parašytu laišku, esą Kristaus diena jau atėjo.
2msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
3Tegul niekas jūsų neapgauna kuriuo nors būdu! Pirmiau turi ateiti atkritimas ir būti apreikštas nuodėmės žmogus, pražūties sūnus,
3Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
4prieštarautojas, kuris išaukština save prieš visa, kas vadinama Dievu ar garbinama, ir pats sėdasi kaip Dievas Dievo šventykloje, rodydamas save esant Dievu.
4Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
5Ar neprisimenate, jog aš tai sakiau jums, tebebūdamas tarp jūsų?
5Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
6Jūs gi žinote, kas dabar jį sulaiko, kad jis būtų apreikštas savo metu.
6Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
7Nedorybės paslaptis jau veikia, kol bus patrauktas tas, kas jį sulaiko.
7Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
8Tada pasirodys nedorėlis, kurį Viešpats sunaikins savo burnos kvėpimu ir sutriuškins savo atėjimo spindesiu.
8Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
9Ano nedorėlio atėjimą, šėtonui veikiant, lydės visokios jėgos, ženklai ir netikri stebuklai
9Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
10ir visokia neteisumo apgaulė žūstantiems už tai, kad atsisakė mylėti tiesą savo išgelbėjimui.
10na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
11Todėl Dievas jiems pasiųs stiprų paklydimą, kad jie tikėtų melu
11Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
12ir būtų nuteisti visi, kurie netikėjo tiesa, bet pamėgo neteisumą.
12Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
13Mes jaučiame pareigą visada dėkoti Dievui už jus, Viešpaties numylėti broliai, kad Dievas jus nuo pradžios išsirinko išgelbėjimui per Dvasios pašventinimą ir tiesos tikėjimą,
13Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
14kuriam Jis pašaukė jus per mūsų Evangeliją, kad įgytumėte mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus šlovę.
14Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
15Todėl, broliai, tvirtai stovėkite ir laikykitės nurodymų, kurių išmokote iš mūsų žodžių ar laiško.
15Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
16O pats mūsų Viešpats Jėzus Kristus ir Dievas, mūsų Tėvas, kuris pamilo mus ir iš malonės suteikė mums amžiną paguodą ir gerą viltį,
16Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema,
17tepaguodžia jūsų širdis ir tesustiprina kiekviename gerame žodyje ir darbe.
17aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.