1Pagaliau, broliai, melskitės už mus, kad Viešpaties žodis skintųsi kelią ir būtų pašlovintas, kaip ir pas jus,
1Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu.
2ir kad mes būtume išgelbėti nuo netikusių ir nedorų žmonių, nes ne visi turi tikėjimą.
2Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanaoamini ujumbe huu.
3O Viešpats ištikimas; Jis sustiprins jus ir apsaugos nuo pikto.
3Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu.
4Mes pasitikime jumis Viešpatyje, kad vykdote ir vykdysite, ką jums įsakome.
4Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni.
5Viešpats telenkia jūsų širdis į Dievo meilę ir Kristaus kantrybę.
5Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.
6Viešpaties Jėzaus Kristaus vardu įsakome jums, broliai, šalintis kiekvieno brolio, kuris tinginiauja ir nesilaiko tradicijos, gautos iš mūsų.
6Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa.
7Jūs patys žinote, kaip reikia sekti mumis. Mes gi pas jus netinginiavome
7Ninyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu;
8ir nevalgėme kieno nors duonos dykai, bet, sunkiai triūsdami, darbavomės dieną ir naktį, kad tik neapsunkintume nė vieno iš jūsų;
8hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu.
9ir ne todėl, kad neturime teisės, bet norime būti jums pavyzdžiu, kad sektumėte mumis.
9Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano.
10Dar būdami pas jus, mes įsakėme: “Kas nenori dirbtitenevalgo!”
10Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, "Mtu asiyefanya kazi, asile."
11Nes mes girdime, kad kai kurie pas jus tinginiauja, nieko nedirba, tik kišasi į svetimus reikalus.
11Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
12Tokiems įsakome ir juos raginame per mūsų Viešpatį Jėzų Kristų ramiai dirbti ir valgyti pačių pelnytą duoną.
12Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe.
13O jūs, broliai, nepailskite darę gera!
13Lakini ninyi ndugu, msichoke kutenda mema.
14O kas nepaklustų mūsų laiško žodžiams, tokį įsidėmėkite ir nebendraukite su juo, kad susigėstų.
14Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye kusudi aone aibu.
15Nelaikykite jo priešu, bet įspėkite kaip brolį.
15Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16Patsai ramybės Viešpats tegul teikia jums ramybę visada ir visais būdais. Viešpats su jumis visais!
16Bwana mwenyewe ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote.
17Šis sveikinimas prirašytas mano, Pauliaus, ranka. Tai ženklas kiekviename laiške: taip aš rašau.
17Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika.
18Mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė tebūna su jumis visais! Amen.
18Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.