1Paulius, Jėzaus Kristaus apaštalas, Dievo, mūsų Gelbėtojo, ir Viešpaties Jėzaus Kristaus, mūsų vilties, paliepimu,
1Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
2Timotiejui, tikram sūnui tikėjime: malonė, gailestingumas ir ramybė nuo Dievo, mūsų Tėvo, ir Jėzaus Kristaus, mūsų Viešpaties!
2nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
3Dar keliaudamas į Makedoniją, aš prašiau tave pasilikti Efeze, kad įsakytum kai kuriems, jog jie nemokytų kitaip,
3Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
4nekreiptų dėmesio į pasakas ir į begalines giminystės eiles, kurios veikiau sukelia ginčus negu dievišką ugdymą, esantį tikėjime.
4Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
5Įsakymo tikslas yra meilė iš tyros širdies, geros sąžinės ir nuoširdaus tikėjimo.
5Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
6Kai kurie, nuklydę nuo šių dalykų, paskendo tuščiuose plepaluose.
6Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
7Jie norėtų būti įstatymo mokytojais, bet nesupranta nei ką kalba, nei ką tvirtina.
7Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
8O mes žinome, jog įstatymas geras, jeigu kas teisingai juo naudojasi,
8Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
9suprasdamas, kad įstatymas nėra skirtas teisiajam, bet nusikaltėliams ir neklusniems, bedieviams ir nusidėjėliams, nešventiems ir šventvagiškiems, tėvažudžiams ir motinžudžiams, žmogžudžiams,
9Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
10paleistuviams, homoseksualistams, vergų pirkliams, melagiams, priesaikos laužytojams ir viskam, kas priešinga sveikam mokymui
10sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
11pagal palaimintojo Dievo šlovingąją Evangeliją, kuri man yra patikėta.
11Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
12Aš dėkoju mūsų Viešpačiui Kristui Jėzui, kuris įgalino mane, nes palaikė mane ištikimu, paskirdamas tarnavimui,
12Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
13nors anksčiau buvau piktžodžiautojas, persekiotojas ir akiplėša. Manęs buvo pasigailėta, nes taip elgiausi dėl neišmanymo ir netikėjimo.
13ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
14Bet mūsų Viešpaties malonė išsiliejo be saiko su tikėjimu ir meile Kristuje Jėzuje.
14Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
15Tikras žodis ir vertas visiško pritarimo, kad Kristus Jėzus atėjo į pasaulį išgelbėti nusidėjėlių, kurių pirmasis esu aš.
15Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
16Todėl ir buvo manęs pasigailėta, kad manyje pirmame Jėzus Kristus parodytų visą savo kantrybę, duodamas pavyzdį tiems, kurie Jį įtikės amžinajam gyvenimui.
16lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele.
17Amžių Karaliui, nemirtingajam, neregimajam, vieninteliam išmintingajam Dievui tebūna garbė ir šlovė per amžių amžius! Amen.
17Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee--kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.
18Šį įsakymą perduodu tau, sūnau Timotiejau, pagal ankstesnes pranašystes apie tave, kad, jomis remdamasis, kovotum gerą kovą,
18Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
19turėdamas tikėjimą ir gerą sąžinę. Jos atsižadėjus, kai kurių tikėjimo laivas sudužo.
19na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
20Iš jų yra Himenėjas ir Aleksandras, kuriuos atidaviau šėtonui, kad jie pasimokytų nebepiktžodžiauti.
20Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.