Lithuanian

Swahili: New Testament

1 Timothy

3

1Štai tikras žodis: jei kas siekia vyskupauti, trokšta gero darbo.
1Msemo huu ni wa kweli: mtu akitaka kuwa kiongozi katika kanisa, huyo anatamani kazi nzuri.
2O vyskupas privalo būti nepeiktinas, vienos žmonos vyras, santūrus, protingas, padorus, svetingas, sugebantis mokyti;
2Basi, kiongozi wa kanisa anapaswa awe mtu asiye na lawama; anapaswa awe na mke mmoja tu, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha;
3ne girtuoklis, ne kivirčius, ne geidžiantis nešvaraus pelno, bet švelnus, nemėgstantis vaidytis, negodus pinigų,
3asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha;
4geras savo namų šeimininkas, turintis klusnius ir tikrai dorus vaikus.
4anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote.
5Jei kas nesugeba šeimininkauti savo namuose, kaipgi jis rūpinsis Dievo bažnyčia?
5Maana kama mtu hawezi kuongoza vema nyumba yake, atawezaje kulitunza kanisa la Mungu?
6Vyskupas neturi būti naujatikis, kad nepasididžiuotų ir nepakliūtų į pasmerkimą kaip velnias.
6Mtu ambaye hajakomaa bado katika imani asifanywe kuwa kiongozi katika kanisa, asije akajaa majivuno na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alivyohukumiwa.
7Be to, jam privalu turėti gerą liudijimą tarp pašalinių, kad nebūtų jam priekaištaujama ir neįkliūtų į velnio pinkles.
7Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi.
8Taip pat ir diakonai privalo būti garbingi, ne dviliežuviai, ne besaikiai vyno gėrėjai, ne geidžiantys nešvaraus pelno,
8Wasaidizi katika kanisa wanapaswa pia kuwa watu wenye tabia njema na wanyofu; wasiwe wanywaji mno wa divai au wenye tamaa ya fedha;
9saugantys tikėjimo paslaptį tyroje sąžinėje.
9wanapaswa kuzingatia kwa dhamiri njema ukweli wa ndani wa imani.
10Ir pirmiausia jie turi būti išbandyti, o paskui, jei pasirodys esą be kaltės, tegul diakonauja.
10Ni lazima kwanza wathibitishwe, na wakionekana kuwa wanafaa, basi, watoe huduma yao.
11Jų žmonos taip pat privalo būti garbingos, ne šmeižikės, santūrios ir ištikimos visame kame.
11Wake zao wanapaswa pia kuwa na tabia njema, wasiowasengenya watu, wenye kiasi na waaminifu katika mambo yote.
12Diakonai tebūna vienos žmonos vyrai, gerai prižiūrintys vaikus ir savo pačių namus.
12Msaidizi katika kanisa lazima awe na mke moja tu, na awezaye kuongoza vema watoto wake na nyumba yake.
13Gerai diakonaujantys įgyja garbingą laipsnį ir didelę tikėjimo drąsą Kristuje Jėzuje.
13Maana wasaidizi wanaofanya kazi yao vizuri hujipatia msimamo mzuri, na wanaweza kusema bila hofu juu ya imani yao katika Kristo Yesu.
14Aš tau rašau apie šiuos dalykus, nors tikiuosi greit atvykti pas tave.
14Ninakuandikia barua hii nikiwa na matumaini ya kuja kwako hivi karibuni.
15Bet jeigu užtrukčiau, noriu, kad žinotum, kaip reikia elgtis Dievo namuose, kurie yra gyvojo Dievo bažnyčia, tiesos ramstis ir pamatas.
15Lakini kama nikicheleweshwa, basi, barua hii itakufahamisha mwenendo tunaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, ambayo ni kanisa la Mungu aliye hai, na ambalo ni nguzo na msingi wa ukweli.
16Ir neginčijamai yra didelė dievotumo paslaptis: Dievas buvo apreikštas kūne, išteisintas Dvasioje, matomas angelų, paskelbtas pagonims, įtikėtas pasaulyje ir paimtas į šlovę.
16Hakuna mashaka yoyote juu ya ukuu wa siri ya dini yetu: Alionekana katika umbo la kibinadamu alithibitishwa na Roho kuwa ni mwadilifu, akaonekana na malaika. Alihubiriwa kati ya mataifa, aliaminiwa popote ulimwenguni, akachukuliwa juu mbinguni katika utukufu.