1Dvasia aiškiai sako, kad paskutiniais laikais kai kurie atsitrauks nuo tikėjimo, pasidavę klaidinančioms dvasioms ir demonų mokymams,
1Roho asema waziwazi kwamba siku za baadaye watu wengine wataitupilia mbali imani; watazitii roho danganyifu na kufuata mafundisho ya pepo.
2veidmainingiems melo skelbėjams, turintiems sudegintą sąžinę,
2Mafundisho ya namna hiyo yanaenezwa na watu waongo wadanganyifu, ambao dhamiri zao ziko kama zimechomwa kwa chuma cha moto.
3draudžiantiems tuoktis, liepiantiems susilaikyti nuo maisto, kurį sukūrė Dievas, kad jį su padėka priimtų tikintieji ir pažinusieji tiesą.
3Watu hao hufundisha kwamba ni makosa kuona na pia kula vyakula fulani. Lakini Mungu aliviumba vyakula hivyo, ili wale walio waumini na ambao wanapata kuujua ukweli, wavitumie kwa shukrani.
4Kiekvienas gi Dievo kūrinys yra geras, ir niekas neatmestina, jei priimama su padėka,
4Kila kitu alichoumba Mungu ni chema, wala hakuna kinachohitaji kukataliwa, bali vyote vipokelewe kwa sala ya shukrani,
5nes tai pašventinama Dievo žodžiu ir malda.
5kwa sababu neno la Mungu na sala hukifanya kitu hicho kikubalike kwa Mungu.
6Jeigu šitaip aiškinsi broliams, būsi geras Jėzaus Kristaus tarnas, besimaitinantis tikėjimo žodžiais ir geru mokymu, kuriuo tu rūpestingai pasekei.
6Kama ukiwapa ndugu wote maagizo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, ukijiendeleza kiroho kwa maneno ya imani na mafundisho ya kweli, ambayo wewe umeyafuata.
7Bedieviškų ir bobiškų pasakų venk, o ugdykis dievotumą.
7Lakini achana na hadithi zile zisizo za kidini na ambazo hazina maana. Jizoeshe kuishi maisha ya uchaji wa Mungu.
8Kūno lavinimas nedaug naudos duoda, o dievotumas viskam naudingas; jis turi esamojo ir būsimojo gyvenimo pažadą.
8Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
9Šis žodis yra tikras, vertas visiško pritarimo.
9Usemi huo ni wa kusadikika kabisa na unastahili kukubaliwa.
10Mes todėl ir triūsiame bei kenčiame panieką, nes pasitikime gyvuoju Dievu, kuris yra visų žmonių, o ypač tikinčiųjų, Gelbėtojas.
10Sisi tunajitahidi na kufanya kazi kwa bidii kwani tumemwekea tumaini letu Mungu aliye hai ambaye ni Mwokozi wa watu wote, na hasa wale wanaoamini.
11Taip įsakinėk ir mokyk!
11Wape maagizo hayo na mafundisho hayo.
12Niekas tegul neniekina tavo jaunystės. Tiktai pats būk tikintiesiems pavyzdys žodžiu, elgesiu, meile, dvasia, tikėjimu, skaistumu.
12Usikubali mtu yeyote akudharau kwa sababu wewe ni kijana, lakini jitahidi uwe mfano kwa wanaoamini: katika usemi wako, mwenendo wako, upendo, imani na maisha safi.
13Kol atvyksiu, užsiiminėk skaitymu, raginimu, mokymu.
13Tumia wakati wako na juhudi yako katika kusoma hadharani Maandiko Matakatifu, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
14Neapleisk tavyje esančios dovanos, kuri tau buvo suteikta per pranašystę su vyresniųjų rankų uždėjimu.
14Usiache kukitumia kile kipaji cha Kristo ndani yako ulichopewa kwa maneno ya manabii na kwa kuwekewa mikono na wazee.
15Mąstyk apie šituos dalykus, atsidėk jiems visiškai, kad tavo pažanga būtų visiems akivaizdi.
15Fikiri kwa makini juu ya hayo yote na kuyatekeleza kusudi maendeleo yako yaonekane na wote.
16Žiūrėk savęs ir mokymo, būk pastovus tame. Taip išgelbėsi save ir savo klausytojus.
16Angalia sana mambo yako mwenyewe, na mafundisho yako. Endelea kufanya hayo maana ukifanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.