1O, kad jūs pakęstumėte truputėlį mano kvailumo! Betgi jūs ir pakenčiate.
1Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
2Aš pavyduliauju dėl jūsų Dievo pavydu, nes sužiedavau jus su vienu vyru, kad nuvesčiau jus Kristui kaip skaisčią mergelę.
2Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3Bet bijau, kad kaip gyvatė savo gudrumu suvedžiojo Ievą, taip ir jūsų mintys nesugestų be paprastumo Kristuje.
3Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4Mat jei kas užklydęs ima skelbti kitą Jėzų, kurio mes neskelbėme, arba jei jūs priimate kitą dvasią, kurios nebuvote priėmę, ar kitą evangeliją, kurios nebuvote gavę, jūs ramiausiai tai pakenčiate.
4Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5Bet aš manau nesąs prastesnis už pačius didžiausius apaštalus.
5Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao "mitume wakuu."
6Ir jei man trūksta iškalbingumo, tai anaiptol ne pažinimo. Ir tai jums esame aiškiai įrodę visais atžvilgiais.
6Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
7Nejaugi nusidėjau, kad pažeminau save ir išaukštinau jus, paskelbdamas jums Dievo Evangeliją už dyką?
7Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8Apiplėšiau kitas bažnyčias, imdamas iš jų atlyginimą, kad galėčiau tarnauti jums.
8Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9O būdamas pas jus ir stokodamas, nė vieno neapsunkinau, nes ko man trūko, parūpino iš Makedonijos atvykę broliai. Aš saugojausi ir ateityje saugosiuos tapti jums našta bet kuria prasme.
9Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10Sakau jums vardan Kristaus tiesos, esančios manyje, kad šio pasididžiavimo Achajos srityse niekas iš manęs neatims.
10Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11Kodėl? Ar todėl, kad jūsų nemyliu? Dievas žino!
11Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
12Ką darau, darysiu ir toliau, kad negalėtų pasiteisinti norintys pasiteisinti, kad tuo, kuo giriasi, jie pasirodytų esą tokie kaip ir mes.
12Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13Juk tokie yra netikri apaštalai, apgaulingi darbininkai, besidedantys Kristaus apaštalais.
13Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
14Ir nenuostabu. Juk pats šėtonas apsimeta šviesos angelu.
14Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15Tad nieko ypatingo, jei jo tarnai apsimeta teisumo tarnais. Bet jų galas bus pagal jų darbus.
15Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
16Kartoju: tegu nei vienas nelaiko manęs kvailiu! O jeigu jau laikote, tai pasiklausykite manęs kaip kvailo, kad irgi galėčiau truputį pasigirti.
16Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17Ką pasakysiu, pasakysiu ne pagal Viešpatį, bet tarytum kvailiodamas ir manydamas galįs pasigirti.
17Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
18Matydamas, kad daug kas giriasi pagal kūną, tai pasigirsiu ir aš.
18Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19Juk, būdami protingi, mokate mielai pakęsti kvailius.
19Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20Nes jūs pakenčiate, kai jus pavergia, kai apryja, kai atima, kai didžiuojasi, kai smogia per veidą.
20Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21Mūsų gėdai pasakysiu, kad buvome tam per silpni. Bet jei kas kuo nors drąsus,tai sakau iš kvailumo, aš drąsus taip pat.
21Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu--nasema kama mtu mpumbavu--mimi nathubutu pia.
22Jie žydai? Ir aš. Jie izraelitai? Ir aš. Jie Abraomo palikuonys? Ir aš.
22Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
23Jie Kristaus tarnai? Kalbu kaip kvailys: aš juo labiau! Aš daug daugiau darbavausi, gavau rykščių be saiko, daugiau kalėjau ir daugel kartų buvau mirties pavojuje.
23Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi--nanena hayo kiwazimu--ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24Nuo žydų gavau penkis kartus po keturiasdešimt be vieno kirčio.
24Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25Tris kartus buvau muštas lazdomis, vienąkart buvau užmėtytas akmenimis. Tris kartus pergyvenau laivo sudužimą, ištisą parą plūduriavau jūroje.
25Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26Dažnai buvau kelionėse, upių pavojuose, pavojuose nuo plėšikų, pavojuose nuo tautiečių, pavojuose nuo pagonių, pavojuose mieste, dykumos pavojuose, pavojuose jūroje, pavojuose nuo netikrų brolių.
26Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
27Kenčiau nuovargį ir skausmą, dažnai budėjau naktimis, alkau ir troškau, dažnai pasninkavau, kenčiau šaltį ir nuogumą.
27Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28Neminint viso kito, kas atsitinka kasdien, rūpinuosi visomis bažnyčiomis.
28Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29Jei kas silpsta, ar aš nesilpstu? Jei kas piktinasi, ar aš nedegu apmaudu?
29Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
30Jei reikia girtis, girsiuosi savo silpnumu.
30Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31Dievas, mūsų Viešpaties Jėzaus Kristaus Tėvas, kuris palaimintas per amžius, žino, kad nemeluoju.
31Mungu na Baba wa Bwana Yesu--jina lake litukuzwe milele--yeye anajua kwamba sisemi uongo.
32Damaske karaliaus Areto valdytojas saugojo damaskiečių miestą, norėdamas mane suimti,
32Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33bet buvau pro langą nuleistas pintinėje per sieną ir taip ištrūkau iš jo rankų.
33Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.