Lithuanian

Swahili: New Testament

2 Corinthians

12

1Jei reikia girtis (nors iš to jokios naudos), eisiu prie Viešpaties regėjimų ir apreiškimų.
1Nitajivuna basi, ingawa haifai! Lakini sasa nitasema juu ya maono na ufunuo alivyonijalia Bwana.
2Pažįstu žmogų Kristuje, kuris prieš keturiolika metų,­ar kūne, ar be kūno­nežinau, Dievas žino,­buvo paimtas iki trečiojo dangaus.
2Namjua mtu mmoja Mkristo, ambaye miaka kumi na minne iliyopita alinyakuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
3Ir žinau, kad šitas žmogus,­ar kūne, ar be kūno­nežinau, Dievas žino,­
3Narudia: najua kwamba mtu huyo alinyakuliwa mpaka peponi. (Lakini sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
4buvo paimtas į rojų ir girdėjo neišreiškiamus žodžius, kurių nevalia žmogui ištarti.
4Huko akasikia mambo ya siri ambayo binadamu hastahili kuyatamka.
5Tokiu pasigirsiu, o ne savimi, nebent savo negaliomis.
5Basi, nitajivunia juu ya mtu wa namna hiyo, na si juu yangu mimi binafsi, isipokuwa tu juu ya udhaifu wangu.
6Jei norėčiau girtis, nebūčiau kvailys, nes kalbėčiau tiesą. Bet susilaikau, kad kas nors apie mane nepagalvotų daugiau negu tai, ką manyje mato ar iš manęs girdi.
6Kama ningetaka kujivuna singekuwa mpumbavu hata kidogo, maana ningekuwa nasema ukweli mtupu. Lakini sitajivuna; sipendi mtu anifikirie zaidi ya vile anavyoona na kusikia kutoka kwangu.
7Ir kad perdėm neišpuikčiau dėl gausybės apreiškimų, man duotas dyglys kūne, šėtono pasiuntinys, kad mane smūgiuotų ir aš neišpuikčiau.
7Lakini, kusudi mambo haya makuu niliyofunuliwa yasinifanye nilewe majivuno, nilipewa maumivu mwilini kama mwiba, mjumbe wa Shetani mwenye kunipiga nisijivune kupita kiasi.
8Dėl to tris kartus meldžiau Viešpatį, kad tai nuo manęs atitrauktų.
8Nilimsihi Bwana mara tatu kuhusu jambo hili ili linitoke.
9Bet Viešpats man pasakė: “Pakanka tau mano malonės, nes mano stiprybė tampa tobula silpnume”. Todėl mieliausiai girsiuosi savo silpnumais, kad Kristaus jėga ilsėtųsi ant manęs.
9Lakini akaniambia: "Neema yangu inatosha kwa ajili yako; maana uwezo wangu hukamilishwa zaidi katika udhaifu." Basi, ni radhi kabisa kujivunia udhaifu wangu ili uwezo wake Kristo ukae juu yangu.
10Patenkintas tad silpnumu, paniekinimais, sunkumais, persekiojimais ir priespauda dėl Kristaus, nes, būdamas silpnas, esu galingas.
10Kwa hiyo nakubali kwa radhi udhaifu, madharau, taabu, udhalimu na mateso, kwa ajili ya Kristo; maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.
11Jūsų verčiamas, tapau kvailiu besigirdamas. Iš tikro tai jūs turėtumėte mane girti, nes aš ne prastesnis už pačius didžiausius apaštalus, nors esu niekas.
11Nimekuwa kama mpumbavu, lakini, ninyi mmenilazimisha kuwa hivyo. Ninyi ndio mngalipaswa kunisifu. Maana, ingawa mimi si kitu, kwa vyovyote, mimi si mdogo zaidi kuliko hao "mitume wakuu."
12Iš tiesų jūsų akyse pasitvirtino apaštalo ženklai: visokeriopa kantrybė, ženklai, stebuklai ir galingi darbai.
12Miujiza na maajabu yaonyeshayo wazi kwamba mimi ni mtume yalifanyika miongoni mwenu kwa uvumilivu wote.
13Tad ko jums trūksta palyginti su kitomis bažnyčiomis? Vien to, kad nebuvau jums našta. Atleiskite man šitą nusikaltimą!
13Je, mlipungukiwa nini zaidi kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi kwa upande wangu sikuwasumbueni kupata msaada wenu? Samahani kwa kuwakoseeni haki hiyo!
14Esu pasiruošęs trečią kartą atvykti pas jus, tačiau neapsunkinsiu jūsų. Ieškau ne to, kas jūsų, bet jūsų pačių. Juk ne vaikai privalo krauti turtą tėvams, bet tėvai vaikams.
14Sasa niko tayari kabisa kuja kwenu mara ya tatu, na sitawasumbua. Maana ninachotafuta si mali zenu, bali ni ninyi wenyewe. Ni kawaida ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba, na si watoto kuwawekea wazazi wao.
15Todėl mielai išleisiu tai, kas mano, ir dar save pridėsiu jūsų sielų labui; nors, kuo daugiau jus myliu, tuo mažiau esu mylimas.
15Mimi ni radhi kabisa kutumia nilicho nacho, na hata kujitolea mimi mwenyewe kabisa, kwa faida ya roho zenu. Je, mtanipenda kidogo ati kwa kuwa mimi nawapenda ninyi mno?
16Tebūnie ir taip,­sakysite,­aš jūsų neapsunkinau, bet, būdamas gudrus, klasta jus pagavau.
16Basi, mtakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu. Lakini labda mtu mwingine atasema: "Kwa vile Paulo ni mwerevu, amewafanyieni ulaghai."
17Bet ar kaip nors išnaudojau jus per kurį savo pasiuntinį?
17Je, mimi niliwanyonyeni kwa njia ya mjumbe yeyote niliyemtuma kwenu?
18Paprašiau Titą keliauti ir pasiunčiau su juo vieną brolį. Ar Titas jus išnaudojo? Ar mes veikėme ne ta pačia dvasia? Ar nevaikščiojome tomis pačiomis pėdomis?
18Mimi nilimwita Tito, nikamtuma kwenu na ndugu yetu mwingine. Je, Tito aliwanyonyeni? Je, hamjui kwamba sisi tumekuwa tukiongozwa na roho yuleyule, na mwenendo wetu ni mmoja?
19Vėl jūs manote, kad prieš jus teisinamės. Mes kalbame prieš Dievą Kristuje: viską darome, mylimieji, jūsų ugdymui.
19Labda mnafikiri kwamba mpaka sasa tumekuwa tukijitetea wenyewe mbele yenu! Lakini, tunasema mambo haya mbele ya Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo. Mambo hayo, yote, wapenzi wangu, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
20Mat bijau, kad atvykęs nerasčiau jūsų tokių, kokių nenoriu, ir kad pats nebūčiau toks, kokio jūs nenorite; kad nebūtų nesantaikos, pavydo, piktumo, barnių, šmeižtų, apkalbų, pasididžiavimo, netvarkos,
20Naogopa, huenda nitakapokuja kwenu nitawakuta katika hali nisiyopenda, nami itanilazimu kuwa katika hali msiyoipenda. Naogopa huenda kukawa na ugomvi, wivu, uhasama, ubishi, masengenyano, kunong'ona, majivuno na fujo kati yenu.
21kad, kai vėl atvyksiu, Dievas nepažemintų manęs prieš jus ir man netektų liūdėti dėl daugelio, kurie pirmiau buvo nusidėję ir dar neatgailavo dėl padarytų netyrumo, ištvirkavimo ir gašlumo darbų.
21Naogopa huenda hapo nitakapokuja safari ijayo Mungu wangu atanifanya niaibike mbele yenu, nami nitaomboleza kwa ajili ya wengi wa wale waliotenda dhambi lakini hawakujutia huo uchafu, tamaa zao mbaya na uzinzi waliokuwa wamefanya.