1Jau trečią kartą keliauju pas jus. “Dviejų ar trijų liudytojų lūpomis bus patvirtintas kiekvienas žodis”.
1Hii ni mara yangu ya tatu kuja kwenu. "Kila tatizo litatatuliwa kwa ushahidi wa watu wawili au watatu," yasema Maandiko.
2Jau sakiau anksčiau ir sakau, kaip ir antrąkart lankydamasis pas jus, ir, būdamas atstu, dabar rašau tiems, kurie anksčiau nusidėjo, ir visiems kitiems,jeigu atvyksiu vėl, būsiu negailestingas.
2Nilikwisha sema, na kama ilivyokuwa safari ya pili, sasa nasema tena nikiwa mbali: wale wote waliotenda uovu bila kutubu, na pia wale wengine, nitakapokuja, watakiona cha mtema kuni.
3Jūs reikalaujate įrodymo, kad manyje kalba Kristus, o Jis nėra silpnas prieš jus, bet galingas jumyse.
3Mtajionea wenyewe kwamba Kristo anasema ndani yangu. Kwenu Kristo si dhaifu; bali nguvu yake yafanya kazi miongoni mwenu.
4Nors Jis buvo nukryžiuotas dėl silpnumo, bet dabar gyvas Dievo jėga. Nors mes irgi silpni Jame, bet jums gyvensime su Juo Dievo galybe.
4Maana hata kama alisulubiwa kwa sababu ya udhaifu, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Sisi pia tu dhaifu kwa kuungana naye lakini tutaishi naye kwa uwezo wa Mungu kwa ajili yenu.
5Patikrinkite patys save, ar esate tikėjime. Ištirkite save! Ar nepažįstate savęs ir nežinote, kad jumyse yra Jėzus Kristus, jeigu tik nesate atmestini?
5Jichunguzeni ninyi wenyewe mpate kujua kama kweli mnayo imani. Jichunguzeni ninyi wenyewe. Je, hamjui kwamba Kristo Yesu yumo ndani yenu? Kama sivyo, basi ninyi mmeshindwa.
6Bet turiu vilties, kad jūs suprasite, jog mes nesame atmestini.
6Lakini natumaini kwamba ninyi mnajua kuwa sisi hatukushindwa.
7Aš meldžiu Dievą, kad jūs nedarytumėte nieko blogo,ne tam, kad pasirodytume tinkami, bet kad jūs darytumėte gera, o mes būtume tartum atmestini.
7Tunamwomba Mungu msifanye uovu wowote, lakini si kusudi tuonekane kama watu waliokwisha faulu, bali mpate kutenda mema, hata kama sisi tunaonekana kuwa tumeshindwa.
8Juk nieko negalime daryti prieš tiesą, bet tik už tiesą.
8Maana hatuwezi kuupinga ukweli; uwezo tulio nao ni wa kuuendeleza ukweli.
9Mes džiaugiamės, kai esame silpni, o jūs stiprūs. Ir taip pat norime jūsų tobulumo.
9Tunafurahi kwamba sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; kwa hiyo tunaomba mpate kuwa wakamilifu.
10Todėl, būdamas toli, tai rašau, kad atvykęs neturėčiau griežtai elgtis, naudodamas valdžią, kurią man Viešpats suteikė tam, kad ugdyčiau, o ne kad griaučiau.
10Basi, ninaandika barua hii nikiwa mbali, ili nitakapofika kwenu nisilazimike kuwa mkali kwenu kwa kutumia ule uwezo alionipa Bwana; naam, uwezo wa kujenga na si wa kubomoa.
11Galiausiai, broliai, likite sveiki. Būkite tobuli, džiaukitės paguoda, būkite vienos minties, gyvenkite taikiai, ir meilės bei ramybės Dievas bus su jumis.
11Kwa sasa, ndugu, kwaherini! Muwe na ukamilifu, shikeni mashauri yangu, muwe na nia moja; kaeni kwa amani. Naye Mungu wa mapendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
12Pasveikinkite vieni kitus šventu pabučiavimu.
12Salimianeni kwa ishara ya upendo.
13Jus sveikina visi šventieji. Viešpaties Jėzaus Kristaus malonė, Dievo meilė ir Šventosios Dvasios bendravimas tebūna su jumis visais! Amen.
13(G13-12) Watu wote wa Mungu huku wanawasalimuni.
14(G13-13) Neema ya Bwana Yesu Kristo na upendo wa Mungu na umoja wa Roho Mtakatifu, viwe nanyi nyote.