Lithuanian

Swahili: New Testament

3 John

1

1Vyresnysis mylimajam Gajui, kurį myliu tiesoje.
1Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2Mylimasis, aš meldžiu, kad tau visame kame gerai sektųsi, kad būtum sveikas,­taip, kaip gerai sekasi tavo sielai.
2Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3Aš labai apsidžiaugiau, kai atvykę broliai paliudijo apie tavo tiesą, kaip tu vaikščioji tiesoje.
3Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4Neturiu didesnio džiaugsmo, kaip girdėti, jog mano vaikai gyvena tiesoje.
4Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5Mielasis, tu ištikimai elgiesi, pagelbėdamas broliams ir atvykstantiems iš kitur.
5Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6Jie paliudijo bažnyčiai apie tavo meilę. Tu puikiai padarysi, išruošdamas juos į kelionę taip, kaip Dievui patinka,
6Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7nes jie išvyko Jo vardo labui, nieko neimdami iš pagonių.
7Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8Mes turime tokius priimti, kad taptume tiesos bendradarbiais.
8Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9Aš parašiau bažnyčiai, bet mėgstantis jiems vadovauti Diotrefas nepriima mūsų.
9Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10Todėl, jei atvyksiu, priminsiu jo darbus, kuriuos jis daro, skleisdamas apie mus piktas kalbas; maža to, nei pats nepriima brolių, nei kitiems, kurie norėtų priimti, neleidžia ir išmeta juos iš bažnyčios.
10Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11Mielasis, nesek tuo, kas pikta, bet tuo, kas gera. Kuris daro gera, yra iš Dievo, o kuris pikta, nėra matęs Dievo.
11Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12Apie Demetriją gerai liudija visi ir pati tiesa. Ir mes liudijame, o tu žinai, kad mūsų liudijimas tikras.
12Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13Dar daug ką turėčiau tau parašyti, bet nenoriu rašyti rašalu ir plunksna.
13Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14Tikiuosi greitai pamatyti tave ir pasikalbėti iš lūpų į lūpas. Ramybė tau! Sveikina tave bičiuliai. Sveikink draugus pavardžiui!
14Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. (G1-15) Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.