1O jūs, šeimininkai, duokite vergams, kas teisinga ir kas dera, atsimindami, kad ir jūs turite Šeimininką danguje.
1Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2Nuolat melskitės, budėdami ir dėkodami;
2Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3melskitės taip pat ir už mus, kad Dievas mums atvertų žodžio duris skelbti Kristaus paslaptį, dėl kurios aš surakintas,
3Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4kad sugebėčiau ją atskleisti taip, kaip privalau ją skelbti.
4Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5Elkitės protingai su pašaliniais, išnaudodami laiką.
5Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6Jūsų kalba visuomet tebūna maloni ir druska pasūdyta, kad sugebėtumėte kiekvienam atsakyti.
6Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7Apie mano reikalus jums viską praneš Tichikas, mylimas brolis, ištikimas tarnas ir bendradarbis Viešpatyje.
7Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8Aš tam jį ir siunčiu, kad sužinotų, kaip jums sekasi, ir paguostų jūsų širdis.
8Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9Jis su Onesimu, ištikimu ir mylimu broliu, kuris yra iš jūsų, papasakos jums visa, kas čia dedasi.
9Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10Jus sveikina mano kalėjimo draugas Aristarchas ir Barnabo pusbrolis Morkusdėl jo jau gavote nurodymų; jei jis atvyks pas jus, priimkite jį.
10Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11Dar jus sveikina Jėzus, vadinamas Justu. Iš apipjaustytųjų jie yra vieninteliai mano bendradarbiai dėl Dievo karalystės, tapę mano paguoda.
11Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12Jus sveikina jūsiškis Epafras, Kristaus tarnas, kuris visada grumiasi už jus maldose, kad jūs būtumėt tobuli ir visiškai įsitikinę, kas yra Dievo valia.
12Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13Aš galiu paliudyti, kad jis labai uolus dėl jūsų, laodikiečių ir hierapoliečių.
13Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14Sveikina jus mylimasis gydytojas Lukas ir Demas.
14Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15Pasveikinkite brolius Laodikėjoje ir Nimfą bei bažnyčią, kuri jo namuose.
15Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16Kai šitas laiškas bus perskaitytas pas jus, pasirūpinkite, kad jis būtų perskaitytas ir laodikiečių bažnyčioje, o jūs perskaitykite laišką, kuris ateis iš Laodikėjos.
16Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17Taip pat pasakykite Archipui: “Žiūrėk, kad vykdytum tarnavimą, kurį gavai Viešpatyje!”
17Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18Sveikinimas, parašytas mano, Pauliaus, ranka. Prisiminkite mano pančius. Malonė su jumis! Amen.
18Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.