1Kadangi Įstatymas turi tiktai būsimųjų gėrybių šešėlį, o ne patį dalykų vaizdą, jis niekada negali tomis pačiomis aukomis, kurios kasmet vis aukojamos ir aukojamos, padaryti tobulus tuos, kurie artinasi.
1Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2Argi tos aukos nesiliautų, jeigu aukotojai, vienąkart apvalyti, daugiau nebejaustų sąžinėje nuodėmių?
2Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3Priešingai: jos metai iš metų vis primena nuodėmes.
3Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4Juk neįmanoma, kad jaučių ir ožių kraujas panaikintų nuodėmes.
4Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5Todėl, ateidamas į pasaulį, Jis sako: “Aukų ir atnašų Tu nenorėjai, bet paruošei man kūną.
5Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: "Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6Tau nepatiko deginamosios atnašos ir aukos už nuodėmes.
6Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7Tuomet tariau: ‘Štai ateinu, kaip knygos rietime apie mane parašyta, vykdyti Tavo, o Dieve, valios!’ ”
7Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria."
8Anksčiau pasakęs: “Aukų ir atnašų, deginamųjų atnašų ir atnašų už nuodėmes Tu nenorėjai ir nemėgai”,jos aukojamos pagal Įstatymą,
8Kwanza alisema: "Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi." Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9paskui paskelbė: “Štai ateinu vykdyti Tavo, o Dieve, valios”. Jis panaikina viena, kad įtvirtintų kita.
9Kisha akasema: "Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako." Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10Tos valios dėka esame Jėzaus Kristaus kūno auka vieną kartą pašventinti visiems laikams.
10Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11Kiekvienas kunigas diena iš dienos tarnauja ir daug kartų aukoja tas pačias aukas, kurios niekada negali panaikinti nuodėmių.
11Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12O šis, paaukojęs vienintelę auką už nuodėmes, amžiams atsisėdo Dievo dešinėje,
12Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13nuo tol laukdamas, kol Jo priešai bus patiesti tarsi pakojis po Jo kojų.
13Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14Vienintele atnaša Jis amžiams padarė tobulus šventinamuosius.
14Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15Tai mums liudija ir Šventoji Dvasia. Ji yra pasakiusi:
15Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16“Štai Sandora, kurią su jais sudarysiu, praslinkus anoms dienoms,sako Viešpats:Aš įdėsiu savo įstatymus į jų širdis ir juos įrašysiu jų mintyse,
16"Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao."
17ir jų nuodėmių bei jų nedorybių daugiau nebeprisiminsiu”.
17Kisha akaongeza kusema: "Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu."
18O kur jos atleistos, ten nebereikia atnašos už nuodėmę.
18Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19Taigi, broliai, galėdami drąsiai įeiti į Švenčiausiąją dėl Jėzaus kraujo
19Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20nauju ir gyvu keliu, kurį Jis atvėrė mums per uždangą, tai yra savąjį kūną,
20Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21ir turėdami didį Kunigą Dievo namams,
21Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22artinkimės su tyra širdimi ir giliu, užtikrintu tikėjimu, apšlakstymu apvalę širdis nuo nešvarios sąžinės ir nuplovę kūną švariu vandeniu!
22Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23Išlaikykime nepajudinamą vilties išpažinimą, nes ištikimas Tas, kuris pažadėjo.
23Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24Žiūrėkime vieni kitų, skatindami mylėti ir daryti gerus darbus.
24Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25Neapleiskime savųjų susirinkimo, kaip kai kurie yra pratę, bet raginkime vieni kitus juo labiau, juo aiškiau regime besiartinančią dieną.
25Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26Jeigu, pasiekę tiesos pažinimą, sąmoningai nusidedame, tada nebelieka aukos už nuodėmes,
26Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27bet kažkoks baisus laukimas teismo ir liepsnojančio pykčio, kuris praris priešininkus.
27Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28Jei kas atstumia Mozės Įstatymą, tas be jokio pasigailėjimo turi mirti, dviem ar trims liudytojams paliudijus.
28Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29Tik pagalvokite: kaip dar sunkesnės bausmės nusipelnys tas, kuris sutrypė kojomis Dievo Sūnų, nešventu palaikė Sandoros kraują, kuriuo buvo pašventintas, ir įžeidė malonės Dvasią!
29Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30Juk pažįstame Tą, kuris pasakė: “Mano kerštas, Aš atsilyginsiu, sako Viešpats”. Ir vėl: “Viešpats teis savo tautą”.
30Maana tunamfahamu yule aliyesema, "Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza," na ambaye alisema pia, "Bwana atawahukumu watu wake."
31Baisu pakliūti į gyvojo Dievo rankas!
31Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32Prisiminkite ankstesnes dienas, kada jūs apšviesti ištvėrėte didelę kentėjimų kovą,
32Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33tiek patys išstatyti viešam reginiui su paniekinimais ir smurtu, tiek būdami dalininkai tų, su kuriais buvo taip elgiamasi.
33Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34Jūs užjautėte mane, kalinį, ir linksmai sutikote savo turto išplėšimą, žinodami, jog turite danguje geresnį ir išliekantį turtą.
34Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35Tad nepameskite savo pasitikėjimo, už kurį skirtas didelis atlygis!
35Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36Taip, reikia jums ištvermės, kad, įvykdę Dievo valią, gautumėte, kas pažadėta.
36Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37Nes “dar trumpa, trumpa valandėlė, ir ateis Tas, kuris turi ateiti, ir neužtruks.
37Maana kama yasemavyo Maandiko: "Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38Bet teisusis gyvens tikėjimu, ir, jeigu jis atsitrauktų, mano siela juo nebesigėrės”.
38Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye."
39Tačiau mes nesame tie, kurie atsitraukia savo pražūčiai, bet tie, kurie tiki, kad išgelbėtume sielą.
39Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.