1Tiesa, ir pirmoji Sandora turėjo tarnavimo Dievui potvarkius ir žemišką šventyklą.
1Agano la kwanza lilikuwa na taratibu zake za ibada na pia mahali patakatifu pa ibada palipojengwa na watu.
2Buvo įrengta palapinė: priešakinė dalis, kur buvo žvakidė, stalas ir padėtinės duonos kepalai, vadinosi Šventoji.
2Palitengenezwa hema ambayo sehemu yake ya nje iliitwa Mahali Patakatifu. Humo mlikuwa na kinara cha taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.
3Už antrosios uždangos buvo palapinės dalis, vadinama Šventų švenčiausioji.
3Nyuma ya pazia la pili, kulikuwa na hema iliyoitwa Mahali Patakatifu Kupita Pote.
4Ten stovėjo auksinis smilkytuvas ir iš visų šonų auksu apmušta Sandoros skrynia, kurioje buvo auksinis ąsotis su mana, išsprogusi Aarono lazda ir Sandoros plokštės.
4Humo mlikuwa na madhabahu ya dhahabu kwa ajili ya kufukizia ubani, na Sanduku la Agano, ambalo lilikuwa limepakwa dhahabu pande zote, na ndani yake mlikuwa na chungu cha dhahabu kilichokuwa na mana; fimbo ya Aroni iliyokuwa imechanua majani, na vile vibao viwili vilivyoandikwa agano.
5Viršum jos buvo šlovės cherubai, kurie gaubė sutaikinimo dangtį. Apie tai dabar nėra reikalo smulkiau kalbėti.
5Juu ya hilo Sanduku kulikuwa na viumbe vilivyodhihirisha kuweko kwa Mungu, na mabawa yao yalitanda juu ya mahali ambapo dhambi huondolewa. Lakini sasa, hatuwezi kusema kinaganaga juu ya mambo hayo.
6Esant tokiai sąrangai, į priekinę palapinės dalį visada eina kunigai atlikti apeigų,
6Mipango hiyo ilitekelezwa kisha ikawa desturi kwa makuhani kuingia kila siku katika hema ya nje kutoa huduma zao.
7o į antrąjąkartą per metus vienas tik vyriausiasis kunigas, ir tai ne be kraujo, kurį aukoja už save ir už tautos nuodėmes, padarytas dėl nežinojimo.
7Lakini kuhani Mkuu peke yake ndiye anayeingia katika lile hema la pili; naye hufanya hivyo mara moja tu kwa mwaka. Anapoingia ndani huwa amechukua damu ambayo anamtolea Mungu kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya dhambi ambazo watu wamezitenda bila wao wenyewe kujua.
8Šitaip Šventoji Dvasia nurodo, kad kelias į Šventų švenčiausiąją dar nėra atviras, kol tebestovi pirmoji palapinė,
8Kutokana na taratibu hizo Roho Mtakatifu anafundisha wazi kwamba wakati ile hema ya nje ingali ipo imesimama, njia ya kuingia Mahali Patakatifu haijafunguliwa.
9kuri yra dabartinio laikotarpio atvaizdas. Joje aukojamos dovanos ir aukos, kurios negali padaryti aukotojo sąžinėje tobulo,
9Jambo hili ni mfano wa nyakati za sasa. Linaonyesha kwamba zawadi na dhabihu zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kuifanya mioyo ya wale wanaoabudu kuwa mikamilifu,
10bet apima tik valgius, gėrimus, įvairius apiplovimus ir kūniškus potvarkius, galiojančius iki atnaujinimo.
10kwani haya yote yanahusika na vyakula, vinywaji na taratibu mbalimbali za kutawadha. Yote hayo ni maagizo ya njenje tu; na nguvu yake hukoma wakati Mungu atakaporekebisha vitu vyote.
11Bet Kristus, atėjęs kaip būsimųjų gėrybių vyriausiasis Kunigas, pro aukštesnę ir tobulesnę palapinę, ne rankų darbo, tai yra ne šitos kūrinijos,
11Lakini Kristo amekwisha fika, akiwa Kuhani Mkuu wa mambo yaliyo mema, ambayo sasa yamekwisha fika. Yeye anatoa huduma zake katika hema iliyo bora na kamilifu zaidi, isiyofanywa kwa mikono ya watu, yaani isiyo ya ulimwengu huu ulioumbwa.
12taip pat ne ožių ar veršių krauju, o savuoju krauju vieną kartą visiems laikams įžengė į Švenčiausiąją ir įvykdė amžinąjį atpirkimą.
12Yeye aliingia Mahali Patakatifu mara moja tu, tena hakuwa amechukua damu ya mbuzi wala ng'ombe, bali aliingia kwa damu yake yeye mwenyewe, akatupatia ukombozi wa milele.
13Jeigu jaučių bei ožių kraujas ir telyčios pelenai per apšlakstymą pašventina susitepusius, kad kūnas būtų švarus,
13Watu waliokuwa najisi kidini waliweza kutakasika na kuwa safi waliponyunyiziwa damu ya mbuzi na ya ng'ombe pamoja na majivu ya ndama.
14tai nepalyginti labiau kraujas Kristaus, kuris per amžinąją Dvasią paaukojo save kaip auką be dėmės Dievui, nuvalys jūsų sąžinę nuo mirties darbų, kad tarnautumėte gyvajam Dievui.
14Lakini, kwa damu ya Kristo, mambo makuu zaidi hufanyika! Kwa nguvu za Roho wa milele, Kristo alijitolea mwenyewe dhabihu kamilifu kwa Mungu. Damu yake itatutakasa dhamiri zetu kutokana na matendo yaletayo kifo, ili tupate kumtumikia Mungu aliye hai.
15Ir todėl Jis yra naujosios Sandoros tarpininkas, kad, įvykus mirčiai pirmojoje Sandoroje padarytiems nusikaltimams atpirkti, pašauktieji gautų amžinojo palikimo pažadą.
15Kwa hiyo, Kristo ndiye aliyeratibisha agano jipya ili wale walioitwa na Mungu wazipokee baraka za milele walizoahidiwa. Watazipata, kwani kifo kimetokea ambacho huwakomboa watu kutoka yale makosa waliyofanya wakati wa lile agano la kale.
16Kur tik yra testamentas, ten būtina įrodyti testatoriaus mirtį.
16Kwa kawaida wosia hutambuliwa tu kama kifo cha yule aliyeufanya huo wosia kimethibitishwa.
17Testamentas įgyja galią, mirus jo sudarytojui, o jam tebesant gyvam, testamentas negalioja.
17Wosia hauwezi kutekelezwa mpaka kumetokea kifo, kwani wosia hauna maana ikiwa mwenye kuufanya bado anaishi.
18Štai kodėl ir pirmoji Sandora nebuvo patvirtinta be kraujo.
18Ndiyo maana hata lile agano la kwanza halikuwekwa bila damu kumwagwa.
19Paskelbęs visai tautai visus įstatymo nuostatus, Mozė, paėmęs veršių bei ožių kraujo su vandeniu ir purpurinės vilnos su yzopu, apšlakstė pačią knygą ir visą tautą,
19Kwanza Mose aliwatangazia watu wote amri zote kama ilivyokuwa katika Sheria; kisha akachukua damu ya ndama pamoja na maji, na kwa kutumia majani ya mti uitwao husopo na pamba nyekundu, akakinyunyizia kile kitabu cha Sheria na hao watu wote.
20sakydamas: “Tai yra kraujas Sandoros, kurią įsakė jums Dievas!”
20Mose alisema: "Hii ni damu inayothibitisha agano mliloamriwa na Mungu mlitii."
21Jis taip pat apšlakstė krauju palapinę ir visus tarnavimo indus.
21Vilevile Mose aliinyunyizia damu ile hema na vyombo vya ibada.
22Taip pat beveik viskas pagal įstatymą apvaloma krauju, ir be kraujo praliejimo nėra atleidimo.
22Naam, kadiri ya Sheria karibu kila kitu chaweza kutakaswa kwa damu, na dhambi nazo zaondolewa tu ikiwa damu imemwagwa.
23Todėl dangiškųjų dalykų atvaizdai turėjo būti šitaip apvalomi, o patys dangaus dalykaigeresnėmis aukomis negu šitos.
23Vitu hivi ambavyo ni mfano tu wa mambo halisi ya mbinguni, vililazimika kutakaswa kwa namna hiyo. Lakini vitu vya mbinguni huhitaji dhabihu iliyo bora zaidi.
24Mat Kristus įžengė ne į rankų darbo šventyklątikrosios atvaizdą, bet į patį dangų, kad dabar pasirodytų už mus Dievo akivaizdoje.
24Maana Kristo hakuingia Mahali Patakatifu palipojengwa kwa mikono ya watu, ambapo ni mfano tu wa kile kilicho halisi. yeye aliingia mbinguni kwenyewe ambako sasa anasimama mbele ya Mungu kwa ajili yetu.
25Ir ne tam, kad pakartotinai aukotų save, kaip daro vyriausiasis kunigas, kuris kasmet įeina į Švenčiausiąją su svetimu krauju,
25Kuhani Mkuu wa Wayahudi huingia Mahali Patakatifu kila mwaka akiwa amechukua damu ya mnyama; lakini Kristo hakuingia humo ili ajitoe mwenyewe mara nyingi,
26tuomet Kristui būtų reikėję daugelį kartų kentėti nuo pasaulio sutvėrimo. Bet dabar Jis vieną kartą pasirodė amžių pabaigoje, kad savo auka sunaikintų nuodėmę.
26maana ingalikuwa hivyo, Kristo angalipaswa kuteswa mara nyingi tangu kuumbwa ulimwengu. Lakini sasa nyakati hizi zinapokaribia mwisho wake, yeye ametokea mara moja tu, kuondoa dhambi kwa kujitoa yeye mwenyewe dhabihu.
27Ir kaip žmonėms skirta vieną kartą mirti, o po toteismas,
27Basi, kama vile kila mtu hufa mara moja tu, kisha husimama mbele ya hukumu ya Mungu,
28taip ir Kristus, vieną kartą paaukotas, kad pasiimtų daugelio nuodėmes, antrą kartą pasirodys be nuodėmės Jo laukiančiųjų išgelbėjimui.
28vivyo hivyo Kristo naye alijitoa dhabihu mara moja tu kwa ajili ya kuziondoa dhambi za wengi. Atakapotokea mara ya pili si kwa ajili ya kupambana na dhambi, bali ni kwa ajili ya kuwaokoa wale wanaomngojea.