Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

8

1Bet iš to, ką sakome, svarbiausia yra štai kas: mes turime tokį vyriausiąjį Kunigą, kuris danguje atsisėdo Didybės sosto dešinėje
1Basi, jambo muhimu katika hayo tunayosema ni hili: sisi tunaye Kuhani Mkuu wa namna hiyo, ambaye anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu mbinguni.
2ir tarnauja šventykloje bei tikroje palapinėje, kurią pastatė ne žmogus, o Viešpats.
2Yeye hutoa huduma ya Kuhani Mkuu katika Mahali Patakatifu sana, yaani ndani ya ile hema ya kweli iliyojengwa na Bwana, siyo na binadamu.
3Kiekvienas vyriausiasis kunigas skiriamas aukoti dovanas ir aukas, tad ir šis privalo turėti, ką aukoti.
3Kila Kuhani Mkuu ameteuliwa kumtolea Mungu vipawa na dhabihu, na hivyo Kuhani Mkuu wetu lazima pia awe na kitu cha kutolea.
4Jeigu Jis būtų žemėje, Jis nebūtų kunigas, nes čia yra kunigai, kurie pagal įstatymą aukoja dovanas.
4Kama yeye angekuwa wa hapa duninani, asingekuwa kamwe kuhani, kwani wako makuhani wengine wanaotoa sadaka kufuatana na Sheria.
5Jie tarnauja dangiškųjų dalykų paveikslui ir šešėliui, panašiai kaip buvo pamokytas Mozė, kai rengėsi statyti palapinę: “Žiūrėk,­sako Jis,­kad visa padarytum pagal tą pavyzdį, kuris tau buvo parodytas ant kalno”.
5Huduma zao za kikuhani ni mfano tu na kivuli cha yale yaliyoko mbinguni. Ndivyo pia ilivyokuwa kwa Mose. Wakati alipokuwa karibu kuitengeneza ile hema, Mungu alimwambia: "Tengeneza kila kitu kufuatana na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani."
6Bet dabar Jis gavo juo prakilnesnį tarnavimą, juo tobulesnės, geresniais pažadais besiremiančios Sandoros tarpininkas yra.
6Lakini sasa Yesu amepewa huduma ya kikuhani iliyo bora zaidi kuliko yao, kama vile agano alilothibitisha kati ya watu na Mungu ni bora zaidi, kwani lina msingi wake katika ahadi za mambo yaliyo bora zaidi.
7Jeigu ta pirmoji Sandora būtų buvusi be trūkumų, nebūtų reikėję ieškoti vietos antrajai.
7Maana kama lile agano la kwanza halingalikuwa na dosari, hakungalikuwa na haja ya agano la pili.
8Jis sakė, peikdamas juos: “Štai ateina dienos,­sako Viešpats,­ kai Aš su Izraelio namais ir Judo namais sudarysiu naują Sandorą.
8Lakini Mungu aliwalaumu watu wake aliposema: "Siku zinakuja, asema Bwana, ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na kabila la Yuda.
9Ne tokią Sandorą, kokią buvau sudaręs su jų tėvais tą dieną, kai paėmiau juos už rankos, norėdamas išvesti iš Egipto žemės. Jie neišsaugojo mano Sandoros, ir Aš juos apleidau,­sako Viešpats.­
9Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao siku ile nilipowaongoza kwa mkono kutoka nchi ya Misri. Hawakuwa waaminifu kwa agano langu; na hivyo mimi sikuwajali, asema Bwana.
10Štai kokia bus Sandora, kurią sudarysiu su Izraelio namais, praslinkus anoms dienoms,­sako Viešpats:­Aš duosiu savo įstatymus jų protams ir juos įrašysiu jų širdyse, ir būsiu jų Dievas, ir jie bus mano tauta.
10Na hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu akilini mwao, na kuziandika mioyoni mwao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
11Ir nė vienas nebemokys savo artimo nei savo brolio, sakydamas: ‘Pažink Viešpatį!’, nes visi mane pažins nuo mažiausio iki didžiausio.
11Hakuna mtu atakayemfundisha mwananchi mwenzake, wala atakayemwambia ndugu yake: Mjue Bwana. Maana watu wote, wadogo na wakubwa, watanijua mimi.
12Aš būsiu gailestingas dėl jų neteisumo ir jų nuodėmių bei nedorybių daugiau nebeprisiminsiu”.
12Nitawasamehe makosa yao, wala sitakumbuka tena dhambi zao."
13Sakydamas “naują Sandorą”, Jis nurodė, kad pirmoji yra pasenusi. O kas pasensta ir nukaršta, to greit nebeliks.
13Kwa kusema juu ya agano jipya, Mungu alilichakaza lile la kwanza; na chochote kinachochakaa na kuwa kikuukuu kitatoweka karibuni.