Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

7

1Tasai Melchizedekas, Salemo karalius, aukščiausiojo Dievo kunigas, sutiko Abraomą, kai jis grįžo, sumušęs karalius, ir palaimino jį.
1Melkisedeki alikuwa mfalme wa Salemu, na kuhani wa Mungu Mkuu. Abrahamu alipokuwa anarudi kutoka vitani ambako aliwaua wafalme, Melkisedeki alikutana naye akambariki,
2Abraomas atidavė jam nuo visko dešimtinę. Išvertus jo vardą, jis pirmiausia teisumo karalius, paskui Salemo, arba ramybės, karalius,­
2naye Abrahamu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo. (Maana ya kwanza ya jina hili Melkisedeki ni "Mfalme wa Uadilifu"; na, kwa vile yeye alikuwa mfalme wa Salemu, jina lake pia lina maana ya "Mfalme wa Amani.")
3be tėvo, be motinos, be kilmės sąrašo, neturintis nei dienų pradžios, nei gyvenimo pabaigos, panašus į Dievo Sūnų. Jis lieka kunigas visam laikui.
3Baba yake na mama yake hawatajwi, wala ukoo wake hautajwi; haisemwi alizaliwa lini au alikufa lini. Anafanana na Mwana wa Mungu, na anaendelea kuwa kuhani daima.
4Pažvelkite, koks didis tas, kuriam ir patriarchas Abraomas davė dešimtinę nuo karo grobio!
4Basi, mwaona jinsi mtu huyu alivyokuwa maarufu. Baba Abrahamu alimpa sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyoteka vitani.
5Beje, ir Levio sūnūs, kurie gauna kunigystę, pagal įstatymą turi įsakymą imti dešimtines iš žmonių, tai yra imti iš savo brolių, nors ir jie kilę iš Abraomo strėnų.
5Tunajua vilevile kwamba kufuatana na Sheria, wana wa Lawi ambao ni makuhani, wanayo haki ya kuchukua sehemu ya kumi kutoka kwa watu, yaani ndugu zao, ingawaje nao ni watoto wa Abrahamu.
6O tas, kuris nėra kilęs iš jų, ėmė dešimtinę iš Abraomo ir palaimino tą, kuris turėjo pažadus.
6Lakini huyo Melkisedeki hakuwa wa ukoo wa Lawi, hata hivyo alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu; tena akambariki yeye ambaye alikuwa amepewa ahadi ya Mungu.
7Be jokių abejonių, visada žemesnį laimina aukštesnis.
7Hakuna mashaka hata kidogo kwamba anayebariki ni mkuu zaidi kuliko yule anayebarikiwa.
8Čia dešimtines ima mirtingi žmonės, o tenai­tas, apie kurį paliudyta, jog jis gyvena.
8Tena, hao makuhani wanaopokea sehemu ya kumi, ni watu ambao hufa; lakini hapa anayepokea sehemu ya kumi, yaani Melkisedeki, anasemekana kwamba hafi.
9Ir, taip sakant, per Abraomą ir Levis mokėjo dešimtines, pats būdamas dešimtinių ėmėjas.
9Twaweza, basi, kusema kwamba Abrahamu alipotoa sehemu moja ya kumi, Lawi (ambaye watoto wake hupokea sehemu moja ya kumi) alitoa sehemu moja ya kumi pia.
10Žinoma, jis dar tebebuvo strėnose tėvo, kai šį pasitiko Melchizedekas.
10Maana Lawi hakuwa amezaliwa bado, bali ni kama alikuwa katika mwili wa baba yake, Abrahamu, wakati Melkisedeki alipokutana naye.
11Jeigu tobulumas būtų buvęs pasiekiamas levitų kunigystės dėka,­o tauta jos pagrindu buvo gavusi įstatymą,­tai kam dar būtų reikėję iškilti kitam kunigui Melchizedeko būdu ir nesivadinti kunigu Aarono būdu?
11Kutokana na ukuhani wa Walawi, watu wa Israeli walipewa Sheria. Sasa, kama huduma ya Walawi ingalikuwa kamilifu hapangekuwa tena na haja ya kutokea ukuhani mwingine tofauti, ukuhani ambao umefuata utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki, na si ule wa Aroni.
12Juk, besikeičiant kunigystei, keičiasi ir įstatymas.
12Maana ukuhani ukibadilika ni lazima Sheria nayo ibadilike.
13O tas, apie kurį tai sakoma, priklausė kitai giminei, iš kurios niekas netarnavo aukurui.
13Naye Bwana wetu ambaye mambo hayo yote yanasemwa juu yake, alikuwa wa kabila lingine, na wala hakuna hata mmoja wa kabila lake aliyepata kutumikia madhabahuni akiwa kuhani.
14Juk aišku, kad mūsų Viešpats kilo iš Judo giminės, apie kurią Mozė nieko nėra kalbėjęs dėl kunigystės.
14Inafahamika wazi kwamba yeye alizaliwa katika kabila la Yuda ambalo Mose hakulitaja alipokuwa anasema juu ya makuhani.
15Tai dar labiau paaiškėja, kai iškyla kitas kunigas, panašus į Melchizedeką,
15Tena jambo hili ni dhahiri zaidi: kuhani mwingine anayefanana na Melkisedeki amekwisha tokea.
16tapęs kunigu ne kūniško įstatymo įsakymu, bet nesibaigiančio gyvenimo jėga.
16Yeye hakufanywa kuwa kuhani kwa sheria na maagizo ya kibinadamu, bali kwa nguvu ya uhai ambao hauna mwisho.
17Juk Jis liudija: “Tu esi kunigas per amžius Melchizedeko būdu”.
17Maana Maandiko yasema: "Wewe ni kuhani milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki."
18Šitaip atšaukiamas ankstyvesnis įsakymas dėl savo silpnumo ir bergždumo,­
18Basi, ile amri ya zamani ilifutwa kwa sababu ilikuwa hafifu na isiyofaa kitu.
19įstatymas juk nieko nepadarė tobulo,­ir įvedama tvirtesnė viltis, kuria priartėjame prie Dievo.
19Maana Sheria ya Mose haikuweza kukamilisha jambo lolote. Lakini sasa, mahali pake pamewekwa tumaini lililo bora zaidi ambalo kwalo tunaweza kumkaribia Mungu.
20Juo labiau, kad tai neįvyko be priesaikos,
20Zaidi ya hayo hapa pana kiapo cha Mungu. Wakati wale wengine walipofanywa makuhani hapakuwako kiapo.
21mat anie tapdavo kunigais be priesaikos, o šis su priesaika To, kuris Jam pasakė: “Viešpats prisiekė, ir Jis nesigailės: ‘Tu esi kunigas per amžius Melchizedeko būdu’ ”.
21Lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alipomwambia: "Bwana ameapa, wala hataigeuza nia yake: Wewe ni kuhani milele."
22Taigi Jėzus yra tapęs geresnės Sandoros garantu.
22Basi, kutokana na tofauti hii, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
23Anų kunigų buvo daug, nes mirtis jiems sukliudydavo ilgiau pasilikti.
23Kuna tofauti nyingine pia: hao makuhani wengine walikuwa wengi kwa sababu walikufa na hawakuweza kuendelea na kazi yao.
24O kadangi šis išlieka per amžius, Jis turi neatšaukiamą kunigystę.
24Lakini Yesu si kama wao, yeye anaishi milele; ukuhani wake hauondoki kwake.
25Todėl Jis ir gali visada išgelbėti tuos, kurie per Jį eina prie Dievo, nes Jis amžinai gyvas, kad juos užtartų.
25Hivyo, yeye anaweza daima kuwaokoa kabisa wote wanaomwendea Mungu kwa njia yake, maana yeye anaishi milele kuwaombea kwa Mungu.
26Mums ir priderėjo turėti tokį vyriausiąjį Kunigą: šventą, nekaltą, tyrą, atskirtą nuo nusidėjėlių ir išaukštintą virš dangų.
26Basi, Yesu ndiye Kuhani Mkuu ambaye anatufaa sana katika mahitaji yetu. Yeye ni mtakatifu, hana hatia wala dhambi ndani yake; hayumo katika kundi la wenye dhambi na ameinuliwa mpaka juu mbinguni.
27Jam nereikia, kaip tiems vyriausiesiems kunigams, kasdien atnašauti aukas pirma už savo nuodėmes, paskui už tautos, nes Jis tai atliko vieną kartą visiems laikams, paaukodamas pats save.
27Yeye si kama wale makuhani wakuu wengine; hana haja ya kutoa dhabihu kila siku, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu. Yeye alifanya hivyo mara moja tu wakati alipojitoa yeye mwenyewe, na hiyo yatosha kwa nyakati zote.
28Įstatymas skiria vyriausiaisiais kunigais žmones su silpnybėmis, o priesaikos žodis, duotas po įstatymo, paskyrė amžiams ištobulintą Sūnų.
28Sheria ya Mose huwateua watu waliokuwa dhaifu kuwa makuhani wakuu; lakini ahadi ya Mungu aliyoifanya kwa kiapo na ambayo imefika baada ya sheria imemteua Mwana ambaye amefanywa mkamilifu milele.