Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

6

1Todėl, palikę pradinį Kristaus mokymą, veržkimės prie tobulumo, užuot vėl dėję pamatus iš atsivertimo nuo negyvų darbų, iš tikėjimo Dievu,
1Basi, tusonge mbele kwa yale yaliyokomaa na kuyaacha nyuma yale mafundisho ya mwanzo ya Kikristo. Hatuhitaji kuweka msingi tena kwa kurudia yale mafundisho ya mwanzo kama vile kuachana na matendo ya kifo, kumwamini Mungu;
2iš mokymo apie krikštus, rankų uždėjimo, mirusiųjų prikėlimo ir amžinybės teismo.
2mafundisho juu ya ubatizo na kuwekewa mikono; ufufuo wa wafu na hukumu ya milele.
3Jei Dievas leis, ir tai padarysime.
3tusonge mbele! Hayo tutayafanya, Mungu akitujalia.
4Kurie kartą jau buvo apšviesti, paragavo dangiškos dovanos, tapo Šventosios Dvasios dalininkais,
4Maana watu wanaoiasi imani yao inawezekanaje kuwarudisha watubu tena? Watu hao walikwisha kuwa katika mwanga wa Mungu, walikwisha onja zawadi ya mbinguni na kushirikishwa Roho Mtakatifu;
5paragavo gerojo Dievo žodžio bei ateinančio amžiaus jėgų
5walikwisha onja wema wa neno la Mungu na nguvu za ulimwengu ujao,
6ir atpuolė, tų nebeįmanoma vėl grąžinti naujai atgailai, nes jie kryžiuoja sau Dievo Sūnų ir išstato Jį viešai paniekai.
6kisha wakaiasi imani yao! Haiwezekani kuwarudisha watubu tena, kwa sababu wanamsulubisha tena Mwana wa Mungu na kumwaibisha hadharani.
7Jeigu žemė sugeria dažną lietų ir iš jos želia želmenys, naudingi tiems, kurie ją dirba, tai ji susilaukia Dievo palaiminimo,
7Mungu huibariki ardhi ambayo huipokea mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuotesha mimea ya faida kwa mkulima.
8bet jeigu ji teželdo erškėčius bei usnis, tai ji niekam tikusi, greitai bus prakeikta ir galiausiai sudeginta.
8Lakini kama ardhi hiyo ikiota miti ya miiba na magugu, haina faida; karibu italaaniwa na Mungu na mwisho wake ni kuchomwa moto.
9Nors taip kalbame, bet jums, mylimieji, tikimės geresnių, vedančių į išgelbėjimą dalykų.
9Lakini, ingawa twasema namna hii, wapenzi wetu, tunalo tumaini kubwa juu ya hali yenu. Tunajua kwamba mmepokea baraka zile bora za wokovu wenu.
10Dievas nėra neteisingas, kad pamirštų jūsų darbą ir meilės triūsą, kurį parodėte Jo vardui, kai tarnavote ir tebetarnaujate šventiesiems.
10Mungu hakosi haki; yeye hataisahau kazi mliyoifanya au upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake katika huduma mliyowapa na mnayowapa sasa watu wake.
11Todėl trokštame, kad kiekvienas iš jūsų rodytų ankstesnį uolumą iki galo, kol pasieks visišką vilties užtikrintumą,­
11Hamu yetu ni kwamba kila mmoja wenu aonyeshe bidii hiyohiyo mpaka mwisho, ili yale mnayotumainia yapate kutimia.
12kad neaptingtumėte, bet būtumėte sekėjai tų, kurie tikėjimu ir kantrybe paveldi pažadus.
12Msiwe wavivu, bali muwe kama wale wanaoamini na wenye uvumilivu na hivyo wanapokea yake aliyoahidi Mungu.
13Kai Dievas davė Abraomui pažadą, neturėdamas kuo aukštesniu prisiekti, prisiekė savimi,
13Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa.
14sakydamas: “Iš tiesų, Aš laiminte palaiminsiu tave, dauginte padauginsiu tave”.
14Mungu alisema: "Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi."
15Ir Abraomas, kantriai laukdamas, gavo, kas buvo pažadėta.
15Abrahamu alisubiri kwa uvumilivu na hivyo alipokea kile alichoahidiwa na Mungu.
16Žmonės prisiekia aukštesniais dalykais ir kiekvieno ginčo pabaigoje patvirtinimui imasi priesaikos.
16Watu wanapoapa, huapa kwa mmoja aliye mkuu zaidi kuliko wao, na kiapo hicho husuluhisha ubishi wote.
17Todėl Dievas, norėdamas stipriau pabrėžti pažado paveldėtojams savo valios nekintamumą, pridėjo priesaiką.
17Naye Mungu aliimarisha ahadi yake kwa kiapo; na kwa namna hiyo akawaonyesha wazi wale aliowaahidia kwamba hatabadili nia yake.
18Tad du nekintami dalykai, kuriuose neįmanoma, kad Dievas meluotų, tvirtai guodžia mus, atradusius prieglobstį mums skirtoje viltyje.
18Basi, kuna vitu hivi viwili: ahadi na kiapo, ambavyo haviwezi kubadilika na wala juu ya hivyo Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hiyo sisi tuliokimbilia usalama kwake, tunapewa moyo wa kushikilia imara tumaini lililowekwa mbele yetu.
19Ji mums yra tarsi saugus ir tvirtas sielos inkaras, prasiskverbiantis pro uždangą vidun,
19Tunalo tumaini hilo kama nanga ya maisha yetu. Tumaini hilo ni imara na thabiti, nalo lapenya lile pazia la hekalu la mbinguni mpaka patakatifu ndani.
20kur už mus kaip pirmtakas įžengė Jėzus, tapęs amžiams vyriausiuoju Kunigu Melchizedeko būdu.
20Yesu ametangulia kuingia humo kwa niaba yetu, na amekuwa kuhani mkuu milele, kufuatana na utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.