1Tikėjimas užtikrina tai, ko viliamės, ir parodo tai, ko nematome.
1Kuwa na imani ni kuwa na hakika ya mambo tunayotumainia; kusadiki kabisa mambo tusiyoyaona.
2Per jį protėviai gavo gerą liudijimą.
2Maana wazee wa kale walipata kibali cha Mungu kwa sababu ya imani yao.
3Tikėjimu suvokiame, kad pasauliai buvo sutverti Dievo žodžiu, būtent iš neregimybės atsirado regima.
3Kwa imani sisi tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu; vitu vinavyoonekana kutoka vitu visivyoonekana.
4Tikėjimu Abelis aukojo geresnę auką negu Kainas ir dėl tikėjimo gavo liudijimą, kad yra teisus, Dievui paliudijus apie jo dovanas. Dėl tikėjimo jis ir miręs tebekalba.
4Kwa imani Abeli alimtolea Mungu dhabihu iliyokuwa bora zaidi kuliko ile ya Kaini. Kwa imani yake alikubaliwa na Mungu kuwa mwadilifu; Mungu mwenyewe alizikubali sadaka zake. Kwa imani yake ingawa amekufa, bado ananena.
5Tikėjimu Henochas buvo perkeltas, kad nematytų mirties, ir “jo neberado, nes Dievas jį perkėlė”. Mat prieš perkeliamas, jis gavo liudijimą, kad patikęs Dievui.
5Kwa imani Henoki alichukuliwa na Mungu, asipate kufa. Hakuonekana tena kwa sababu Mungu alikuwa amemchukua. Maandiko yasema kwamba kabla ya kuchukuliwa kwake, yeye alikuwa amempendeza Mungu.
6O be tikėjimo neįmanoma patikti Dievui. Kas artinasi prie Dievo, tam būtina tikėti, kad Jis yra ir kad uoliai Jo ieškantiems atsilygina.
6Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Kwa maana kila mtu anayemwendea Mungu ni lazima aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba huwatuza wale wanaomtafuta.
7Tikėjimu Nojus, Dievo perspėtas apie tuo metu dar nematomus dalykus, būdamas dievobaimingas, pastatė arką savo šeimai išgelbėti; tikėjimu jis pasmerkė pasaulį ir paveldėjo tikėjimo teisumą.
7Kwa imani Noa alionywa na Mungu juu ya mambo ya baadaye ambayo hakuweza kuyaona bado. Alimtii Mungu, akajenga ile safina ambamo aliokolewa yeye pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo ulimwengu ulihukumiwa, naye Noa akapokea uadilifu unaotokana na imani.
8Tikėjimu Abraomas pakluso, kai buvo pašauktas keliauti į šalį, kurią turėjo paveldėti, ir išvyko, nežinodamas kur einąs.
8Kwa imani Abrahamu alimtii Mungu alipoitwa aende katika nchi ambayo Mungu angempa iwe yake. Ingawa hakujua alikokuwa anakwenda, Abrahamu alihama.
9Tikėjimu jis apsigyveno pažado žemėje, tarytum svetimoje, gyvendamas palapinėse su Izaoku ir Jokūbu, to paties pažado bendrapaveldėtojais.
9Kwa imani aliishi kama mgeni katika nchi aliyoahidiwa na Mungu. Aliishi huko katika hema kama walivyoishi Isaka na Yakobo, ambao pia walishiriki ahadi ileile.
10Mat jis laukė miesto su pamatais, kurio statytojas ir kūrėjas yra Dievas.
10Maana Abrahamu alikuwa akingojea mji wenye misingi imara, mji ambao Mungu mwenyewe ndiye fundi aliyeubuni na kuujenga.
11Tikėjimu ir pati Saranevaisinga ir nebe to amžiausgavo galios pastoti ir pagimdė vaiką, nes ji laikė ištikimu Tą, kuris pažadėjo.
11Kwa imani hata Sara aliamini kwamba Mungu hutimiza ahadi zake, kwa hiyo akajaliwa kuchukua mimba ingawaje alikuwa amepita umri.
12Todėl iš vieno vyro, ir dar apmirusio, gimė palikuonys, gausūs tartum dangaus žvaigždės ir nesuskaitomi kaip jūros pakrantės smiltys.
12Kwa hiyo, kutoka katika mtu huyo mmoja, Abrahamu, ambaye alikuwa kama amekufa, walitokea watu wengi wasiohesabika kama vile nyota za mbinguni na mchanga wa pwani.
13Jie visi mirė tikėdami, dar negavę pažadėtųjų dalykų, bet iš tolo juos regėdami, buvo įsitikinę jais ir priėmė juos, išpažindami, jog jie žemėje svečiai ir keleiviai.
13Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.
14Kurie taip kalba, parodo, kad ieško tėvynės.
14Watu wanaosema mambo kama hayo, huonyesha wazi kwamba wanaitafuta nchi yao wenyewe.
15Jeigu jie būtų minėję aną, iš kurios iškeliavo, jie būtų turėję laiko sugrįžti atgal.
15Kama wangalikuwa wanaifikiria nchi walikotoka zamani, wangalipata nafasi ya kurudi huko.
16Bet dabar jie siekė geresnės tėvynės, tai yra dangiškosios. Todėl Dievas nesigėdija vadintis jų Dievu: juk Jis paruošė jiems Miestą!
16Lakini sasa wanataka nchi iliyo bora zaidi, yaani nchi ya mbinguni. Ndiyo maana Mungu haoni haya wakimwita yeye Mungu wao, kwa sababu yeye mwenyewe amekwisha watayarishia mji.
17Tikėjimu Abraomas aukojo Izaoką, kai buvo mėginamas. Jis, kuris buvo gavęs pažadą, aukojo savo viengimį sūnų,
17Kwa imani, Abrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
18apie kurį buvo pasakyta: “Iš Izaoko bus pašaukti tavo palikuonys”.
18ingawa Mungu alikuwa amemwambia: "Wazawa wako watatokana na Isaka."
19Jis suprato, kad Dievas gali prikelti net iš mirties, ir atgavo sūnų tarytum iš numirusių.
19Abrahamu aliamini kwamba Mungu anaweza kuwafufua wafu: na kwa namna fulani kweli Abrahamu alimpata tena mwanae kutoka wafu.
20Tikėjimu Izaokas palaimino ateičiai Jokūbą ir Ezavą.
20Kwa imani Isaka aliwabariki Yakobo na Esau, wapate baraka zitakazokuja baadaye.
21Tikėjimu Jokūbas mirties valandą palaimino kiekvieną Juozapo sūnų ir pagarbino, atsirėmęs į savo lazdos drūtgalį.
21Kwa imani Yakobo alipokuwa karibu kufa, aliwabariki kila mmoja wa wana wa Yosefu, akamwabudu Mungu akiegemea ile fimbo yake.
22Tikėjimu merdintis Juozapas priminė apie Izraelio vaikų iškeliavimą ir davė nurodymų dėl savo palaikų.
22Kwa imani Yosefu alipokuwa karibu kufa, alinena juu ya kutoka kwa Waisraeli katika nchi ya Misri, na pia akawaachia maagizo kuhusu mifupa yake.
23Tikėjimu Mozė tris mėnesius buvo tėvų paslėptas, nes jie matė, koks kūdikis dailus, ir neišsigando karaliaus įsakymo.
23Kwa imani wazazi wa Mose walimficha huyo mtoto kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaliwa kwake. Walimwona kuwa ni mtoto mzuri, wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
24Tikėjimu Mozė užaugęs atsisakė vadintis faraono dukters sūnumi.
24Kwa imani Mose alipokuwa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti Farao.
25Jis verčiau pasirinko su Dievo tauta kęsti sunkumus negu laikinai džiaugtis nuodėmės malonumais.
25Aliona ni afadhali kuteseka pamoja na watu wa Mungu kuliko kufurahia raha ya dhambi kwa kitambo kidogo.
26Jis Kristaus paniekinimą laikė didesniu turtu negu Egipto brangenybes, nes jis žvelgė į atlygį.
26Alitambua kwamba kuteseka kwa ajili ya Masiha kuna faida kubwa zaidi kuliko utajiri wote wa nchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia tuzo la baadaye.
27Tikėjimu jis paliko Egiptą, neišsigandęs karaliaus rūstybės, nes liko nepajudinamas, tarsi regėtų Neregimąjį.
27Kwa imani Mose alihama kutoka nchi ya Misri bila kuogopa hasira ya mfalme; na wala hakurudi nyuma, kwani alikuwa kama mtu aliyemwona yule Mungu asiyeonekana.
28Tikėjimu jis įsteigė Paschą ir apšlakstymą krauju, kad naikintojas nepaliestų jų pirmagimių.
28Kwa imani aliadhimisha siku ya Pasaka, akaamuru damu inyunyizwe juu ya milango, ili yule Malaika Mwangamizi asiwaue wazaliwa wa kwanza wa Israeli.
29Tikėjimu jie perėjo per Raudonąją jūrą tartum per sausumą, o tai daryti mėginantys egiptiečiai prigėrė.
29Kwa imani watu wa Israeli walivuka bahari ya Shamu, kana kwamba ilikuwa nchi kavu; lakini Wamisri walipojaribu kufanya hivyo walikufa maji.
30Tikėjimu buvo sugriauti Jericho mūrai po septynių dienų žygiavimo aplinkui.
30Kwa imani kuta za mji wa Yeriko zilianguka watu wa Israeli walipokwisha zunguka kwa muda wa siku saba.
31Tikėjimu paleistuvė Rahaba nepražuvo kartu su neklusniaisiais; mat ji taikingai buvo priėmusi žvalgus.
31Kwa imani Rahabu aliyekuwa malaya hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wale wapelelezi.
32Ką dar pasakyti? Man neužtektų laiko, jeigu imčiau pasakoti apie Gedeoną, Baraką, Samsoną, Jeftę, Dovydą, Samuelį ir pranašus,
32Basi, niseme nini zaidi? Wakati hauniruhusu kueleza juu ya Gedeoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi, Samweli na manabii.
33kurie tikėjimu nugalėjo karalystes, vykdė teisumą, įgijo pažadus, užčiaupė liūtams nasrus,
33Kwa imani hawa wote walipigana vita na wafalme, wakashinda. Walitenda mambo adili, wakapokea yale aliyoahidi Mungu. Walifunga vinywa vya simba,
34užgesino ugnies karštį, paspruko nuo kalavijo ašmenų, sustiprėjo iš silpnumo, tapo galiūnais kovoje, privertė bėgti svetimųjų pulkus.
34Walizima mioto mikali, waliepuka kuuawa kwa upanga. Walikuwa dhaifu lakini walipata nguvu. Walikuwa hodari katika vita wakashinda majeshi ya kigeni.
35Moterys atgavo prikeltus savo mirusiuosius, kiti buvo kankinami ir atsisakė išlaisvinimo, kad gautų prakilnesnį prisikėlimą.
35Na, wanawake walioamini walirudishiwa wafu wao wakiwa wamefufuliwa. Baadhi yao walikataa kufunguliwa, wakateswa mpaka kufa ili wapate kufufuliwa na kuingia katika maisha bora zaidi.
36Dar kiti iškentė patyčias ir plakimus, taip pat pančius ir kalėjimą.
36Wengine walidhihakiwa na kupigwa mijeledi, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa gerezani.
37Jie buvo akmenimis užmušami, pjaustomi pusiau, gundomi, kardu žudomi, klajojo prisidengę avių ir ožkų kailiais, vargo, kentė priespaudą ir kankinimus.
37Walipigwa mawe, walipasuliwa vipandevipande, waliuawa kwa upanga. Walizungukazunguka wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi, walikuwa watu maskini, walioteswa na kudhulumiwa.
38Jie, kurių pasaulis nebuvo vertas, klajojo dykumose ir kalnuose, slapstėsi olose ir žemės plyšiuose.
38Ulimwengu haukustahili kuwa na watu hao. Walitangatanga jangwani na mlimani, wakaishi katika mashimo na mapango ya ardhi.
39Ir jie visi, per tikėjimą gavę gerą liudijimą, negavo to, kas buvo pažadėta,
39Watu hawa wote walionekana kuwa mashujaa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, hawakupokea yale ambayo Mungu aliwaahidia,
40nes Dievas geresnius dalykus buvo numatęs mums, kad jie ne be mūsų pasiektų tobulumą.
40maana Mungu alikuwa ameazimia mpango ulio bora zaidi kwa ajili yetu; yaani wao wangeufikia ukamilifu wakiwa pamoja nasi.