1Todėl ir mes, tokio didelio debesies liudytojų apsupti, nusimeskime visus apsunkinimus bei lengvai apraizgančią nuodėmę ir ištvermingai bėkime mums paskirtose lenktynėse,
1Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
2žiūrėdami į mūsų tikėjimo pradininką ir atbaigėją Jėzų. Jis vietoj sau priderančio džiaugsmo, nepaisydamas gėdos, iškentėjo kryžių ir atsisėdo Dievo sosto dešinėje.
2Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
3Apsvarstykite, kaip Jis iškentė nuo nusidėjėlių tokį priešiškumą, kad nepailstumėte ir nesuglebtumėte savo sielomis!
3Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
4Jums dar neteko priešintis iki kraujų, kovojant su nuodėme.
4Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
5Jūs pamiršote paraginimą, kuris sako jums kaip sūnums: “Mano sūnau, nepaniekink Viešpaties auklybos ir nenusimink Jo baramas:
5Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? "Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
6nes kurį Viešpats myli, tą griežtai auklėja, ir plaka kiekvieną sūnų, kurį priima”.
6Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae."
7Jeigu jūs pakenčiat drausmę, Dievas elgiasi su jumis kaip su sūnumis. O kurio gi sūnaus tėvas griežtai neauklėja?
7Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
8Bet jeigu jūs be drausmės, kuri visiems privaloma, vadinasi, jūs ne sūnūs, o pavainikiai.
8Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
9Jau mūsų kūno tėvai mus bausdavo, ir mes juos gerbėme. Tad argi nebūsime dar klusnesni dvasių Tėvui, kad gyventume?
9Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
10Juk anie savo nuožiūra mus drausmino neilgą laiką, o šis tai daro mūsų labui, kad taptume Jo šventumo dalininkais.
10Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
11Beje, kiekviena auklyba tam kartui atrodo ne linksma, o karti, bet vėliau ji atneša taikingų teisumo vaisių auklėtiniams.
11Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
12Todėl pakelkite nuleistas rankas, sustiprinkite linkstančius kelius
12Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
13ir ištiesinkite takus po savo kojomis, kad, kas luoša, neišnirtų, bet verčiau sugytų.
13Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
14Siekite santaikos su visais, siekite šventumo, be kurio niekas neregės Viešpaties.
14Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
15Žiūrėkite, kad kas neprarastų Dievo malonės, kad neišleistų daigų kokia karti šaknis ir nepadarytų vargo, suteršdama daugelį;
15Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
16kad neatsirastų ištvirkėlių ir bedievių kaip Ezavas, už valgio kąsnį pardavęs pirmagimio teises.
16Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
17Jūs žinote, kad jis ir paskui, norėdamas paveldėti palaiminimą, buvo atmestas, nes nerado progos atgailai, nors su ašaromis jos ieškojo.
17Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
18Jūs prisiartinote ne prie apčiuopiamo ir liepsnojančio ugnimi kalno ar prie tamsos, ar ūkanų, ar viesulo,
18Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
19ar trimito skardenimo, ar žodžių skambesio, kurį išgirdę žmonės meldė, kad daugiau nebūtų ištarta nė žodžio.
19mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
20Mat jie negalėjo pakelti įsakymo: “Net jeigu gyvulys paliestų kalną, jis privalo būti užmuštas akmenimis arba nušautas strėle”.
20kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: "Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe."
21Anas reginys buvo toks baisus, jog Mozė pasakė: “Labai išsigandau ir visas drebu!”
21Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, "Naogopa na kutetemeka."
22Bet jūs prisiartinote prie Siono kalno bei gyvojo Dievo miesto, dangiškosios Jeruzalės, prie nesuskaitomų tūkstančių angelų
22Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
23ir šventiško susirinkimo, prie danguje įrašytųjų pirmagimių bažnyčios, prie visų Teisėjo Dievo, prie ištobulintų teisiųjų dvasių
23Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
24ir prie Naujosios Sandoros Tarpininko Jėzaus bei prie apšlakstymo kraujo, kuris kalba apie geresnius dalykus negu Abelio kraujas.
24Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
25Žiūrėkite, kad neatstumtumėte kalbančiojo, nes jeigu anie neištrūko, kai atmetė Tą, kuris žemėje davė įspėjimų, tai juo labiau neištrūksime mes, nusigręžę nuo To, kuris kalba iš dangaus.
25Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
26Jo balsas anuomet drebino žemę, o dabar Jis pažadėjo, sakydamas: “Aš dar kartą sudrebinsiu ne tik žemę, bet ir dangų!”
26Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: "Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu."
27Žodžiai “dar kartą” rodo, kad iš sutvertųjų dalykų bus pašalinti sudrebinamieji, kad pasiliktų tai, kas nesudrebinama.
27Neno hili: "tena" linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
28Todėl, gaudami nesudrebinamą karalystę, tvirtai laikykimės malonės, kuria galime deramai tarnauti Dievui su pagarba ir baime,
28Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
29nes mūsų Dievas yra ryjanti ugnis.
29maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.