Lithuanian

Swahili: New Testament

Hebrews

13

1Teišsilaiko broliška meilė.
1Endeleeni kupendana kidugu.
2Nepamirškite svetingumo, nes per jį kai kurie, patys to nežinodami, priėmė viešnagėn angelus.
2Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3Prisiminkite kalinius, tarsi kartu būdami įkalinti, prisiminkite tuos, su kuriais piktai elgiamasi, nes patys tebesate kūne.
3Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4Tebūna visų gerbiama santuoka ir nesuteptas santuokos patalas. O ištvirkėlius ir svetimautojus teis Dievas.
4Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5Gyvenkite be godumo pinigams, būkite patenkinti tuo, ką turite, nes Jis pats yra pasakęs: “Niekad Aš tavęs nepaliksiu ir nepamiršiu”.
5Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa."
6Todėl galime su pasitikėjimu tarti: “Viešpats mano padėjėjas­aš nebijosiu! Ką gali padaryti man žmogus?”
6Ndiyo maana tunathubutu kusema: "Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?"
7Atsiminkite savo vadovus, kurie jums skelbė Dievo žodį. Įsižiūrėkite į jų gyvenimo vaisius, sekite jų tikėjimu.
7wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8Jėzus Kristus yra tas pats vakar, šiandien ir per amžius.
8Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
9Nesiduokite suklaidinami įvairių ir svetimų mokslų, nes gera, kai širdis sustiprinama malone, o ne valgiais, kurie nedavė naudos tiems, kurie jų laikėsi.
9Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10Mes turime aukurą, nuo kurio valgyti neturi teisės tie, kurie tarnauja palapinei.
10Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11Juk kūnai gyvulių, kurių kraujas vyriausiojo kunigo įnešamas į šventyklą už nuodėmes, sudeginami už stovyklos.
11Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12Todėl ir Jėzus, norėdamas savo krauju pašventinti tautą, kentėjo už vartų.
12Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13Taigi išeikime pas Jį už stovyklos, nešdami Jo paniekinimą.
13Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14Čia mes neturime išliekančio miesto, bet ieškome būsimojo.
14Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15Todėl per Jį visada aukokime Dievui šlovinimo auką, tai yra Jo vardą garbinančių lūpų vaisių.
15Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16Nepamirškite daryti gera ir dalintis su kitais, nes tokios aukos patinka Dievui.
16Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17Klausykite savo vadovų ir būkite jiems atsidavę, nes jie budi jūsų sielų labui, būdami atsakingi už jas; jie tai tedaro su džiaugsmu, o ne dūsaudami, nes tai nebūtų jums naudinga.
17Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18Melskite už mus, nes esame įsitikinę turį gerą sąžinę ir norį visame kame dorai elgtis.
18Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19Itin prašau melsti, kad būčiau greičiau jums sugrąžintas.
19Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20Ramybės Dievas, amžinosios Sandoros krauju išvedęs iš numirusių didįjį avių Ganytoją­mūsų Viešpatį Jėzų,
20Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele.
21teištobulina jus kiekvienam geram darbui, kad vykdytumėte Jo valią, Jam veikiant jumyse, kas Jo akims patinka per Jėzų Kristų. Jam šlovė per amžių amžius! Amen.
21Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.
22Aš maldauju jus, broliai, kantriai priimkite šį paraginimo žodį: juk parašiau jums trumpai.
22Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23Žinokite, kad mūsų brolis Timotiejus yra išleistas laisvėn. Jei jis greitai atvyks, ir aš su juo drauge pamatysiu jus.
23Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24Sveikinkite visus savo vadovus ir visus šventuosius. Jus sveikina broliai iš Italijos.
24Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25Malonė teesie su jumis visais! Amen.
25Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.