1Jokūbas, Dievo ir Viešpaties Jėzaus Kristaus tarnas, siunčia sveikinimus dvylikai pasklidusių giminių.
1Mimi Yakobo, mtumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, nawaandikia ninyi, makabila kumi na mawili, yaliyotawanyika ulimwenguni! Salaam!
2Mano broliai, laikykite didžiausiu džiaugsmu, kai patenkate į visokius išbandymus.
2Ndugu zangu, muwe na furaha mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
3Žinokite, kad jūsų tikėjimo išbandymas ugdo ištvermę,
3kwani mwajua kwamba imani yenu ikisha stahimili, itawapatieni uvumilivu.
4o ištvermė tesubręsta iki galo, kad būtumėte tobuli, subrendę ir nieko nestokotumėte.
4Muwe na hakika kwamba uvumilivu wenu utawategemeza mpaka mwisho, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu, bila kupungukiwa chochote.
5Jei kuriam iš jūsų trūksta išminties, teprašo Dievą, kuris visiems dosniai duoda ir nepriekaištauja, ir jam bus suteikta.
5Lakini kama mmoja wenu ametindikiwa hekima, basi, anapaswa kumwomba Mungu ambaye atampatia; kwani Mungu huwapa wote kwa wingi na kwa ukarimu.
6Bet tegul prašo tikėdamas, nė kiek neabejodamas, nes abejojantis panašus į jūros bangą, varinėjamą ir blaškomą vėjo.
6Lakini anapaswa kuomba kwa imani bila mashaka yoyote. Mtu aliye na mashaka ni kama mawimbi ya bahari ambayo husukumwa na kutupwatupwa na upepo.
7Toksai žmogus tenemano ką nors gausiąs iš Viešpaties,
7Mtu wa namna hiyo, mwenye nia mbili na asiye na msimamo katika mwenendo wake wote,
8toks svyruojantis, visuose savo keliuose nepastovus žmogus.
8asidhani ya kwamba atapata chochote kile kutoka kwa Bwana.
9Tesigiria pažemintas brolis savo išaukštinimu,
9Ndugu aliye maskini anapaswa kufurahi wakati Mungu anapomkweza,
10o turtuolis savo pažeminimu, nes jis išnyks kaip lauko gėlė.
10naye tajiri anapaswa kufurahi anaposhushwa na Mungu. Maana tajiri atatoweka kama ua la porini.
11Juk pakyla saulė, jos kaitra išdžiovina žolyną, ir jo žiedas nubyra, jo išvaizdos grožis pranyksta. Taip ir turtuolis sunyks savo keliuose.
11Jua huchomoza na kwa joto lake kali hukausha mimea, nayo maua yake huanguka, na uzuri wake wote huharibika. Vivyo hivyo, tajiri ataangamizwa katika shughuli zake.
12Palaimintas žmogus, kuris ištveria pagundymą, nes, kai bus išbandytas, jis gaus gyvenimo vainiką, kurį Viešpats pažadėjo Jį mylintiems.
12Heri mtu anayebaki mwaminifu katika majaribu, kwani akisha stahimili atapewa tuzo la uzima ambalo Mungu aliwaahidia wale wanaompenda.
13Nė vienas gundomas tenesako: “Esu Dievo gundomas”. Dievas negali būti gundomas blogiu ir pats nieko negundo.
13Kama mtu akijaribiwa, asiseme: "Ninajaribiwa na Mungu." Maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu yeyote.
14Kiekvienas yra gundomas, savo paties geismo pagrobtas ir suviliotas.
14Lakini mtu hujaribiwa anapovutwa na kunaswa na tamaa zake mbaya.
15Paskui užsimezgęs geismas pagimdo nuodėmę, o užbaigta nuodėmė gimdo mirtį.
15Tamaa ikiiva huzaa dhambi; nayo dhambi ikikomaa huzaa kifo.
16Neapsigaukite, mano mylimi broliai!
16Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike!
17Kiekvienas geras davinys ir kiekviena tobula dovana yra iš aukštybių, nužengia nuo šviesybių Tėvo, kuriame nėra permainų ir nė šešėlio keitimosi.
17Kila kipaji chema na kila zawadi kamilifu hutoka mbinguni; hutoka kwa Baba, Muumba wa mianga, ambaye habadiliki wala hana alama yoyote ya ugeugeu.
18Savo valia Jis pagimdė mus tiesos žodžiu, kad būtume tarsi Jo kūrinių pirmieji vaisiai.
18Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa kwa neno lake la ukweli, ili tuwe namna ya matunda ya kwanza miongoni mwa viumbe vyake.
19Žinokite, mano mylimi broliai: kiekvienas žmogus tebūna greitas klausyti, lėtas kalbėti, lėtas pykti.
19Ndugu zangu wapenzi, kumbukeni jambo hili! Kila mtu na awe mwepesi wa kusikia lakini asiwe mwepesi wa kusema wala mwepesi wa kukasirika.
20Žmogaus rūstybė nedaro Dievo teisumo.
20Mwenye hasira hawezi kutimiza matakwa ya Mungu yaliyo ya haki.
21Todėl, atmetę visą nešvarą bei piktybės gausą, su romumu priimkite įdiegtąjį žodį, kuris gali išgelbėti jūsų sielas.
21Kwa hiyo, tupilieni mbali mwenendo mchafu na tabia zote mbovu; jiwekeni chini ya Mungu na kupokea ule ujumbe uliopandwa mioyoni mwenu, ambao waweza kuziokoa nafsi zenu.
22Būkite žodžio vykdytojai, o ne vien klausytojai, apgaudinėjantys patys save.
22Msijidanganye wenyewe kwa kusikiliza tu neno lake, bali litekelezeni kwa vitendo.
23Jei kas tėra žodžio klausytojas, o ne vykdytojas, tai jis panašus į žmogų, kuris žiūri į savo gimtąjį veidą veidrodyje.
23Yeyote anayesikiliza hilo neno lakini halitekelezi, huyo ni kama mtu anayejiangalia sura yake mwenyewe katika kioo.
24Pasižiūrėjo į save ir nuėjo, ir bematant pamiršo, koks buvo.
24Hujiangalia mwenyewe, kisha huenda zake, na mara husahau jinsi alivyo.
25Bet kas įsižiūri į tobuląjį laisvės įstatymą ir jį vykdo, kas tampa nebe klausytojas užuomarša, bet darbo vykdytojas, tas bus palaimintas savo darbuose.
25Lakini mtu anayeangalia kwa makini sheria kamilifu ambayo huwapa watu uhuru, mtu anayeendelea kuizingatia, na si kuisikia tu na kuisahau baadaye, bali anaitekeleza, mtu huyo atabarikiwa katika kila kitu anachofanya.
26Jei kas iš jūsų mano esąs pamaldus ir nepažaboja savo liežuvio, bet apgaudinėja savo širdį, to pamaldumas tuščias.
26Kama mtu akijiona kuwa ni mtu mwenye dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, dini yake haifai kitu, na anajidanganya mwenyewe.
27Tyras ir nesuteptas pamaldumas prieš Dievą ir Tėvą yra: lankyti našlaičius ir našles jų sielvarte ir saugoti save nesuterštą šiuo pasauliu.
27Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.