Lithuanian

Swahili: New Testament

James

2

1Mano broliai, turėkite mūsų Jėzaus Kristaus, šlovės Viešpaties, tikėjimą, neatsižvelgdami į asmenis.
1Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.
2Štai į jūsų susirinkimą ateina žmogus su auksiniu žiedu, puikiais drabužiais, taip pat įžengia beturtis apskurusiu apdaru.
2Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.
3Jūs žiūrite į tą, kuris puikiai apsirengęs, ir sakote: “Atsisėsk čia į gerą vietą”, o beturčiui tariate: “Stovėk ten”, arba: “Sėskis prie mano kojų”.
3Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: "Keti hapa mahali pazuri," na kumwambia yule maskini: "Wewe, simama huko," au "Keti hapa sakafuni miguuni pangu,"
4Argi jūs nesate šališki, argi netampate piktais sumetimais besivadovaujantys teisėjai?
4je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?
5Paklausykite, mano mylimieji broliai: ar Dievas neišsirinko pasaulio vargšų, kad jie būtų turtingi tikėjimu ir paveldėtų karalystę, pažadėtą Jį mylintiems?
5Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.
6O jūs paniekinote beturtį! Argi ne turtuoliai jus spaudžia, ar ne jie tampo jus po teismus?
6Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?
7Ar ne jie niekina tą kilnų vardą, kuriuo jūs vadinatės?
7Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?
8Jeigu tik įvykdote karališkąjį įstatymą, kaip sako Raštas: “Mylėk savo artimą kaip save patį”, jūs gerai darote;
8Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: "Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", mtakuwa mnafanya vema kabisa.
9bet, jeigu atsižvelgiate į asmenis, darote nuodėmę ir esate įstatymo kaltinami kaip nusižengėliai.
9Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.
10Mat, kas laikosi viso įstatymo, bet nusižengia vienu dalyku, tas kaltas dėl visų.
10Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.
11Juk Tas, kuris pasakė: “Nesvetimauk!”, taip pat pasakė ir: “Nežudyk”. Tad jeigu tu nesvetimauji, bet žudai,­vis tiek esi įstatymo laužytojas.
11Maana yuleyule aliyesema: "Usizini," alisema pia "Usiue". Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.
12Taip kalbėkite ir taip darykite, kaip tie, kurie bus teisiami pagal laisvės įstatymą.
12Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.
13Teismas negailestingas tam, kuris neparodė gailestingumo. O gailestingumas triumfuoja prieš teismą.
13Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.
14Kokia nauda, mano broliai, jei kas sakosi turįs tikėjimą, bet neturi darbų? Ar gali jį išgelbėti toks tikėjimas?
14Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?
15Jei brolis ar sesuo neturi drabužių ir stokoja kasdienio maisto,
15Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.
16ir kas nors iš jūsų jiems tartų: “Eikite ramybėje, sušilkite ir pasisotinkite”, o neduotų, ko reikia jų kūnui,­kokia iš to nauda?
16Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: "Nendeni salama mkaote moto na kushiba," bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?
17Taip ir tikėjimas: jei neturi darbų, jis savyje miręs.
17Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.
18Bet kažkas pasakys: “Tu turi tikėjimą, o aš turiu darbus”. Parodyk man savo tikėjimą be darbų, o aš tau darbais parodysiu savo tikėjimą.
18Lakini mtu anaweza kusema: "Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!" Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19Tu tiki, kad yra vienas Dievas? Gerai darai. Ir demonai tiki ir dreba!
19Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.
20Ar nori žinoti, neišmintingas žmogau, kad tikėjimas be darbų miręs?
20Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?
21Argi ne darbais buvo išteisintas mūsų tėvas Abraomas, aukodamas savo sūnų Izaoką ant aukuro?
21Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.
22Ar matai, kad tikėjimas veikė kartu su jo darbais, ir darbais tikėjimas buvo atbaigtas?
22Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.
23Taip išsipildė Rašto žodžiai: “Abraomas patikėjo Dievu, ir tai buvo jam įskaityta teisumu”, o jis buvo pramintas Dievo draugu.
23Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: "Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu."
24Jūs matote, kad žmogus išteisinamas darbais, o ne vienu tikėjimu.
24Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.
25Taip pat ir paleistuvė Rahaba: argi ji ne darbais buvo išteisinta, kai priėmė pasiuntinius ir kitu keliu juos išleido?
25Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.
26Kaip kūnas be dvasios yra miręs, taip ir tikėjimas be darbų negyvas.
26Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.