Lithuanian

Swahili: New Testament

James

3

1Mano broliai, ne visi būkite mokytojais. Žinokite, kad mūsų laukia griežtesnis teismas.
1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe walimu. Kama mjuavyo, sisi walimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine.
2Juk mes visi daug kur nusižengiame. Kas nenusižengia žodžiu, tas yra tobulas žmogus; jis sugeba pažaboti ir visą kūną.
2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote.
3Jei mes įbrukame žąslus arkliams į nasrus, kad mums paklustų, mes suvaldome visą jų kūną.
3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka.
4Štai kad ir laivai: nors jie tokie dideli ir smarkių vėjų varomi, mažytis vairas juos pakreipia, kur nori vairininkas.
4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka.
5Taip pat ir liežuvis yra mažas narys, bet giriasi didžiais dalykais. Žiūrėkite, kokia maža ugnelė padega didžiausią girią;
5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana. Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa.
6ir liežuvis yra ugnis­nedorybės pasaulis. Liežuvis yra vienas iš mūsų narių, kuris suteršia visą kūną, padega gyvenimo eigą, pats pragaro padegtas.
6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe.
7Kiekviena žvėrių, paukščių, šliužų ir jūros gyvūnų veislė buvo sutramdyta ir yra sutramdoma žmogaus prigimties jėga.
7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote--wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini.
8O liežuvio joks žmogus nepajėgia suvaldyti; jis lieka nerimstanti blogybė, pilna mirtinų nuodų.
8Lakini hakuna mtu aliyeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua.
9Juo laiminame mūsų Dievą Tėvą ir juo keikiame žmones, kurie sutverti pagal Dievo atvaizdą.
9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huohuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
10Iš tų pačių lūpų plaukia ir laiminimas, ir prakeikimas. Bet taip, mano broliai, neturi būti!
10Maneno ya laana na ya kusifia hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo.
11Nejaugi šaltinis iš tos pačios versmės lieja saldų ir kartų vandenį?
11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja?
12Argi gali, mano broliai, figmedis išauginti alyvas, o vynmedis figas? Taip pat ir šaltinis negali duoti sūraus vandens ir saldaus.
12Ndugu zangu, je, mti wa mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13Kas tarp jūsų išmintingas ir sumanus? Teparodo geru elgesiu savo darbus su išmintingu romumu.
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aonyeshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima.
14Bet jeigu jūs savo širdyje puoselėjate kartų pavydą ir savanaudiškumą, tuomet nesigirkite ir nemeluokite tiesai.
14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli.
15Tai nėra išmintis, nužengusi iš aukštybių, bet žemiška, sielinė ir demoniška.
15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani.
16Kur pavydas ir savanaudiškumas, ten netvarka bei įvairūs pikti darbai.
16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi hapo pana fujo na kila aina ya uovu.
17Bet išmintis, kilusi iš aukštybių, pirmiausia yra tyra, paskui taikinga, švelni, klusni, pilna gailestingumo ir gerų vaisių, bešališka ir neveidmainiška.
17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki.
18O teisumo vaisius su ramybe sėjamas tų, kurie neša ramybę.
18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.