Lithuanian

Swahili: New Testament

James

4

1Iš kur tarp jūsų atsiranda karai ir kivirčai? Ar ne iš jūsų užgaidų, kurios nerimsta jūsų nariuose?
1Mapigano na magombano yote kati yenu yanatoka wapi? Hutoka katika tamaa zenu mbaya ambazo hupigana daima ndani yenu.
2Geidžiate ir neturite; žudote ir pavydite­ir negalite pasiekti; kovojate ir kariaujate; neturite, nes neprašote.
2Mnatamani vitu na kwa vile hamvipati mko tayari kuua; mwatamani sana kupata vitu, lakini hamvipati, hivyo mnagombana na kupigana. Hampati kile mnachotaka kwa sababu hamkiombi kwa Mungu.
3Jūs prašote ir negaunate, nes blogo prašote­savo užgaidoms išleisti.
3Tena, mnapoomba hampati kwa sababu mnaomba kwa nia mbaya; mnaomba ili mpate kutosheleza tamaa zenu.
4Paleistuviai ir paleistuvės! Ar nežinote, kad draugystė su pasauliu yra priešiškumas Dievui? Taigi kas nori būti pasaulio bičiulis, tas tampa Dievo priešu.
4Ninyi ni watu msio na uaminifu kama wazinzi. Je, hamjui kwamba kuwa rafiki wa ulimwengu ni kuwa adui wa Mungu? Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.
5Gal manote, kad Raštas veltui sako: “Pavydžiai trokšta Dvasia, kuri gyvena mumyse”.
5Msifikiri kwamba Maandiko Matakatifu yamesema maneno ya bure, yanaposema: "Roho ambaye Mungu amemweka ndani yetu ana wivu mkubwa."
6Bet Jis duoda dar didesnę malonę, ir todėl sako: “Dievas išdidiems priešinasi, o nuolankiesiems teikia malonę”.
6Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: "Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu."
7Todėl atsiduokite Dievui; priešinkitės velniui, ir jis bėgs nuo jūsų.
7Basi, jiwekeni chini ya Mungu; mpingeni Ibilisi naye atawakimbieni.
8Artinkitės prie Dievo, ir Jis artinsis prie jūsų. Nusiplaukite rankas, nusidėjėliai, nusivalykite širdis, dvejojantys.
8Mkaribieni Mungu, naye atakuja karibu nanyi. Osheni mikono yenu enyi wakosefu! Safisheni mioyo yenu enyi wanafiki!
9Dejuokite, liūdėkite ir raudokite! Jūsų juokas tepavirsta gedulu, o džiaugsmas­liūdesiu.
9Oneni huzuni, lieni na kuomboleza; kicheko chenu na kiwe kilio; na furaha yenu iwe huzuni kubwa.
10Nusižeminkite prieš Viešpatį, ir Jis jus išaukštins.
10Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
11Broliai, neapkalbinėkite vieni kitų! Kas apkalba ir teisia savo brolį, tas apkalba ir teisia įstatymą. O jeigu teisi įstatymą, vadinasi, nesi įstatymo vykdytojas, bet teisėjas.
11Ndugu, msilaumiane ninyi kwa ninyi. Anayemlaumu ndugu yake na kumhukumu, huyo huilaumu na kuihukumu Sheria. Kama ukiihukumu Sheria, basi, wewe huitii Sheria, bali waihukumu.
12Yra vienas įstatymo leidėjas, kuris gali išgelbėti ir pražudyti. O kas gi tu toks, kuris teisi kitą?
12Mungu peke yake ndiye mwenye kuweka Sheria na kuhukumu. Ni yeye peke yake anayeweza kuokoa na kuangamiza. Basi, wewe ni nani hata umhukumu binadamu mwenzako?
13Nagi jūs, kurie sakote: “Šiandien arba rytoj keliausime į tą ir tą miestą, tenai išbūsime metus, versimės prekyba ir pasipelnysime”,­
13Basi, sasa sikilizeni ninyi mnaosema: "Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani na kukaa huko mwaka mzima tukifanya biashara na kupata faida."
14jūs nežinote, kas atsitiks rytoj! Ir kas gi jūsų gyvybė? Garas, kuris trumpam pasirodo ir paskui išnyksta.
14Ninyi hamjui hata maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Ninyi ni kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi tu na kutoweka tena.
15Verčiau sakytumėte: “Jei Viešpats panorės, gyvensime ir darysime šį bei tą”.
15Mngalipaswa kusema: "Bwana akitujalia tutaishi na tutafanya hiki au kile."
16O dabar jūs giriatės iš savo pasipūtimo, ir kiekvienas toks gyrimasis yra blogas.
16Lakini sasa mwajivuna na kujigamba; majivuno ya namna hiyo ni mabaya.
17Kas moka daryti gera ir nedaro, tas nusideda.
17Basi, mtu ambaye hafanyi lile jambo jema analojua kwamba anapaswa kulifanya, anatenda dhambi.