1“Tenebūgštauja jūsų širdys! Tikite Dievątikėkite ir mane!
1Yesu aliwaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia.
2Mano Tėvo namuose daug buveinių. Jeigu taip nebūtų, būčiau jums pasakęs. Einu jums vietos paruošti.
2Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; la sivyo ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi.
3Kai nuėjęs paruošiu, vėl sugrįšiu ir jus pas save pasiimsiu, kad jūs būtumėte ten, kur ir Aš.
3Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi.
4Kur Aš einu, jūs žinote, ir kelią jūs žinote”.
4Mnajua njia ya kwenda huko ninakokwenda."
5Tomas Jam sako: “Viešpatie, mes nežinome, kur Tu eini, tai kaip žinosime kelią?”
5Thoma akamwuliza, "Bwana, hatujui unakokwenda, tutawezaje basi, kuijua hiyo njia?"
6Jėzus jam sako: “Aš esu kelias, tiesa ir gyvenimas. Niekas nenueina pas Tėvą kitaip, kaip tik per mane.
6Yesu akamjibu, "Mimi ni njia, na ukweli na uzima. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu.
7Jeigu pažinote mane, tai pažinsite ir mano Tėvą. Jau nuo šiol Jį pažįstate ir esate Jį matę”.
7Ikiwa mnanijua mimi mnamjua na Baba yangu pia. Na tangu sasa, mnamjua, tena mmekwisha mwona."
8Pilypas Jam sako: “Viešpatie, parodyk mums Tėvą, ir bus mums gana”.
8Filipo akamwambia, "Bwana, tuonyeshe Baba, nasi tutatosheka."
9Jėzus jam taria: “Jau tiek laiko esu su jumis, ir tu, Pilypai, vis dar manęs nepažįsti? Kas matė mane, matė Tėvą! Tad kaip gali sakyti: ‘Parodyk mums Tėvą’?
9Yesu akamwambia, "Filipo, nimekaa nanyi muda wote huu, nawe hujanijua? Aliyekwisha niona mimi amemwona Baba. Unawezaje basi, kusema: Tuonyeshe Baba?
10Nejaugi tu netiki, kad Aš esu Tėve ir Tėvas manyje? Žodžius, kuriuos jums kalbu, ne iš savęs kalbu; Tėvas, esantis manyjeJis daro darbus.
10Je, huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambieni nyote siyasemi kwa mamlaka yangu; Baba aliye ndani yangu anafanya kazi yake.
11Tikėkite manimi, kad Aš esu Tėve ir Tėvas manyje, arba tikėkite mane dėl pačių darbų!
11Mnapaswa kuniamini ninaposema kwamba mimi niko ndani ya Baba naye Baba yuko ndani yangu. Ama sivyo, aminini kwa sababu ya mambo ninayofanya.
12Iš tiesų, iš tiesų sakau jums: kas mane tiki, darys darbus, kuriuos Aš darau, ir dar už juos didesnių darys, nes Aš einu pas savo Tėvą.
12Kweli nawaambieni, anayeniamini atafanya mambo ninayofanya mimi; naam, atafanya hata makuu zaidi, maana nakwenda kwa Baba.
13Ir ko tik prašysite mano vardu, Aš padarysiu, kad Tėvas būtų pašlovintas Sūnuje.
13Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
14Ko tik prašysite mano vardu, Aš padarysiu.
14Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.
15Jei mylite mane, laikykitės mano įsakymų.
15"Mkinipenda mtazishika amri zangu.
16Ir Aš paprašysiu Tėvą, ir Jis duos jums kitą Guodėją, kad Jis liktų su jumis per amžius.
16Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele.
17Tiesos Dvasią, kurios pasaulis neįstengia priimti, nes Jos nemato ir nepažįsta. O jūs Ją pažįstate, nes Ji yra su jumis ir bus jumyse.
17Yeye ni Roho wa kweli. Ulimwengu hauwezi kumpokea kwa sababu hauwezi kumwona wala kumjua. Lakini ninyi mnamjua kwa sababu anabaki nanyi na yu ndani yenu.
18Nepaliksiu jūsų našlaičiais ateisiu pas jus.
18"Sitawaacha ninyi yatima; nitakuja tena kwenu.
19Dar valandėlė, ir pasaulis manęs nebematys. O jūs mane matysite, nes Aš gyvenu ir jūs gyvensite.
19Bado kidogo nao ulimwengu hautaniona tena, lakini ninyi mtaniona; na kwa kuwa mimi ni hai, nanyi pia mtakuwa hai.
20Tą dieną jūs suprasite, kad Aš esu savo Tėve, ir jūs manyje, ir Aš jumyse.
20Siku ile itakapofika mtajua kwamba mimi niko ndani ya Baba, nanyi mko ndani yangu, nami ndani yenu.
21Kas žino mano įsakymus ir jų laikosi, tas myli mane. O kas mane myli, tą mylės mano Tėvas, ir Aš jį mylėsiu ir pats jam apsireikšiu”.
21Azipokeaye amri zangu na kuzishika, yeye ndiye anipendaye. Naye anipendaye mimi atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake."
22Judasne Iskarijotaspaklausė: “Viešpatie, kas atsitiko, jog ketini apsireikšti mums, o ne pasauliui?”
22Yuda (si yule Iskarioti) akamwambia, "Bwana, itawezekanaje wewe kujidhihirisha kwetu na si kwa ulimwengu?"
23Jėzus jam atsakė: “Jei kas mane myli, laikysis mano žodžio ir mano Tėvas jį mylės; mes pas jį ateisime ir apsigyvensime.
23Yesu akamjibu, "Mtu akinipenda atashika neno langu, na Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake na kukaa naye.
24Kas manęs nemyli, mano žodžių nesilaiko. O žodis, kurį girdite, ne mano, bet Tėvo, kuris mane siuntė.
24Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno mlilosikia si langu, bali ni lake Baba aliyenituma.
25Aš jums tai pasakiau, būdamas su jumis,
25"Nimewaambieni mambo haya nikiwa bado pamoja nanyi
26o GuodėjasŠventoji Dvasia, kurią mano vardu Tėvas atsiųs, mokys jus visko ir viską primins, ką jums sakiau.
26lakini Msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisheni kila kitu na kuwakumbusheni yote niliyowaambieni.
27Aš palieku jums ramybę, duodu jums savo ramybę. Ne kaip pasaulis duoda, Aš jums duodu. Tenebūgštauja jūsų širdys ir teneišsigąsta.
27"Nawaachieni amani; nawapeni amani yangu. Siwapi ninyi kama vile ulimwengu ufanyavyo. Msiwe na wasiwasi, wala msifadhaike.
28Jūs girdėjote, kaip Aš pasakiau: ‘Aš išeinu ir vėl sugrįšiu pas jus!’ Jei mylėtumėte mane, džiaugtumėtės, kad pasakiau: ‘Einu pas Tėvą’, nes mano Tėvas už mane didesnis.
28Mlikwisha sikia nikiwaambieni: Ninakwenda zangu, kisha nitarudi tena kwenu. Kama mngalinipenda mngalifurahi kwa sababu ninakwenda kwa Baba, maana yeye ni mkuu kuliko mimi.
29Ir dabar, prieš įvykstant, jums tai pasakiau, kad tikėtumėte, kada tai įvyks.
29Nimewaambieni haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini.
30Jau nebedaug su jumis kalbėsiu, nes ateina šio pasaulio kunigaikštis, ir manyje jis neturi nieko.
30Sitasema nanyi tena mambo mengi, maana mtawala wa ulimwengu huu anakuja. Kwangu mimi hawezi kitu;
31Bet pasaulis turi pažinti, jog Aš myliu Tėvą ir darau taip, kaip Jis man įsakė.Kelkitės, eikime iš čia!”
31lakini ulimwengu unapaswa kujua kwamba nampenda Baba, na ndiyo maana nafanya kila kitu kama Baba alivyoniamuru. Simameni, tutoke hapa!"