1“Aš esu tikrasis vynmedis, o mano Tėvasvynininkas.
1"Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
2Kiekvieną šakelę manyje, neduodančią vaisiaus, Jis išpjauna, o kiekvieną šakelę, nešančią vaisių, apvalo, kad ji duotų daugiau vaisiaus.
2Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
3Jūs jau esate švarūs dėl žodžio, kurį jums kalbėjau.
3Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.
4Pasilikite manyje, ir Aš jumyse. Kaip šakelė negali duoti vaisiaus pati iš savęs, nepasilikdama vynmedyje,taip ir jūs, jei nepasiliksite manyje.
4Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
5Aš esu vynmedis, o jūs šakelės. Kas pasilieka manyje ir Aš jame, tas duoda daug vaisių; nes be manęs jūs negalite nieko nuveikti.
5"Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
6Kas nepasiliks manyje, bus išmestas laukan ir sudžius kaip šakelė. Paskui surinks šakeles, įmes į ugnį, ir jos sudegs.
6Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
7Jei pasiliksite manyje ir mano žodžiai pasiliks jumyse,jūs prašysite, ko tik norėsite, ir bus jums duota.
7Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
8Tuo bus pašlovintas mano Tėvas, kad duosite gausių vaisių ir būsite mano mokiniai.
8Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
9Kaip mane Tėvas pamilo, taip ir Aš jus pamilau. Pasilikite mano meilėje!
9Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.
10Jei laikysitės mano įsakymų, pasiliksite mano meilėje, kaip Aš kad vykdau savo Tėvo įsakymus ir pasilieku Jo meilėje.
10Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11Aš jums tai kalbėjau, kad jumyse liktų manasis džiaugsmas ir kad jūsų džiaugsmui nieko netrūktų.
11Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
12Tai yra mano įsakymas, kad mylėtumėte vienas kitą, kaip Aš jus pamilau.
12Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
13Niekas neturi didesnės meilės kaip tas, kuris savo gyvybę už draugus atiduoda.
13Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
14Jūs esate mano draugai, jei darote, ką jums įsakau.
14Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.
15Jau nebevadinu jūsų tarnais, nes tarnas nežino, ką veikia jo šeimininkas. Jus Aš draugais vadinu, nes jums viską paskelbiau, ką iš savo Tėvo girdėjau.
15Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.
16Ne jūs mane išsirinkote, bet Aš jus išsirinkau ir paskyriau, kad eitumėte, duotumėte vaisių ir jūsų vaisiai išliktų,kad ko tik prašytumėte Tėvą mano vardu, Jis jums duotų.
16Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.
17Aš jums tai įsakau: mylėkite vienas kitą!”
17Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.
18“Jei pasaulis jūsų nekenčia, žinokite, kad manęs jis nekentė pirmiau negu jūsų.
18"Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
19Jei jūs būtumėte pasaulio, jis mylėtų jus kaip savuosius. Kadangi jūsne pasaulio, bet Aš jus iš pasaulio išskyriau, todėl jis jūsų nekenčia.
19Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
20Atsiminkite žodžius, kuriuos jums sakiau: ‘Tarnas ne didesnis už savo šeimininką!’ Jei persekiojo mane, tai ir jus persekios; jeigu laikėsi mano žodžio, laikysis ir jūsų.
20Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.
21Bet visa tai jums darys dėl mano vardo, nes jie nepažįsta To, kuris mane siuntė.
21Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.
22Jei nebūčiau atėjęs ir jiems kalbėjęs, jie neturėtų nuodėmės. O dabar jie neturi kuo pateisinti savo nuodėmės.
22Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.
23Kas manęs nekenčia, nekenčia ir mano Tėvo.
23Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.
24Jeigu nebūčiau tarp jų padaręs darbų, kurių niekas kitas nedarė, jie neturėtų nuodėmės. O dabar jie matė, ir nekenčia ir manęs, ir mano Tėvo.
24Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.
25Bet kad išsipildytų užrašytas Įstatyme žodis: ‘Jie manęs nekentė be priežasties’.
25Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: Wamenichukia bure!
26Kai ateis Guodėjas, kurį jums atsiųsiu nuo Tėvo,Tiesos Dvasia, kuri eina iš Tėvo,Jis liudys apie mane.
26"Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.
27Ir jūs liudysite, nes nuo pradžios su manimi buvote”.
27Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.