1Jėzaus Kristaus, Dievo Sūnaus, Gerosios naujienos pradžia,
1Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
2kaip pranašų parašyta: “Štai Aš siunčiu pirma Tavęs savo pasiuntinį, kuris nuties Tau kelią.
2Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: "Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
3Dykumoje šaukiančiojo balsas: ‘Paruoškite Viešpačiui kelią! Ištiesinkite Jam takus!’ ”
3Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake."
4Jonas pasirodė dykumoje, krikštijo ir skelbė atgailos krikštą nuodėmėms atleisti.
4Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
5Pas jį traukė visa Judėjos šalis ir Jeruzalės gyventojai. Jie išpažindavo savo nuodėmes ir visi buvo krikštijami Jordano upėje.
5Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
6Jonas vilkėjo kupranugario vilnų apdaru, o strėnas buvo susijuosęs odiniu diržu. Jis maitinosi skėriais ir lauko medumi.
6Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
7Jis skelbė: “Po manęs ateina galingesnis už maneaš nevertas nusilenkęs atrišti Jo sandalų dirželio.
7Naye alihubiri akisema, "Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
8Aš jus krikštijau vandeniu, o Jis krikštys jus Šventąja Dvasia”.
8Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu."
9Tomis dienomis atėjo Jėzus iš Galilėjos Nazareto, ir Jonas pakrikštijo Jį Jordane.
9Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
10Vos tik išbridęs iš vandens, Jis pamatė prasiveriantį dangų ir Dvasią tarsi balandį, nusileidžiančią ant Jo.
10Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
11Ir iš dangaus pasigirdo balsas: “Tu esi mano mylimasis Sūnus, kuriuo Aš gėriuosi”.
11Sauti ikasikika kutoka mbinguni: "Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe."
12Ir tuojau Dvasia Jį nuvedė į dykumą.
12Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
13Jis praleido dykumoje keturiasdešimt dienų šėtono gundomas, buvo kartu su žvėrimis, ir angelai Jam tarnavo.
13akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
14Kai Jonas buvo suimtas, Jėzus atėjo į Galilėją ir skelbė Dievo karalystės Evangeliją:
14Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
15“Atėjo metas, prisiartino Dievo karalystė. Atgailaukite ir tikėkite Evangelija!”
15"Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!"
16Eidamas palei Galilėjos ežerą, Jėzus pamatė Simoną ir jo brolį Andriejų, metančius tinklą į ežerą; mat jie buvo žvejai.
16Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
17Jėzus jiems tarė: “Sekite paskui mane, ir Aš jus padarysiu žmonių žvejais”.
17Yesu akawaambia, "Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
18Ir tuojau, palikę tinklus, jie nusekė paskui Jį.
18Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
19Paėjęs truputį toliau, Jis pamatė Zebediejaus sūnų Jokūbą ir jo brolį Joną, valtyje betaisančius tinklus.
19Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
20Tuoj pat Jis pašaukė ir juos. Palikę savo tėvą Zebediejų valtyje su samdiniais, jie nusekė paskui Jį.
20Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
21Jie atėjo į Kafarnaumą, ir iškart, sabato dieną, Jis nuėjo į sinagogą ir ėmė mokyti.
21Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
22Žmonės stebėjosi Jo mokymu, nes Jis mokė kaip turintis valdžią, o ne kaip Rašto žinovai.
22Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
23Jų sinagogoje buvo žmogus, turintis netyrąją dvasią. Jis sušuko:
23Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
24“Palik mus! Ko Tau iš mūsų reikia, Jėzau Nazarieti? Gal atėjai mūsų pražudyti? Aš žinau, kas Tu esi: Dievo Šventasis!”
24akapaaza sauti, "Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!"
25Jėzus sudraudė jį: “Nutilk ir išeik iš jo!”
25Yesu akamkemea, "Nyamaza! Mtoke mtu huyu."
26Tada netyroji dvasia pradėjo jį tąsyti ir, baisiai šaukdama, išėjo iš jo.
26Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
27Visi apstulbo ir klausinėjo vienas kitą: “Kas tai? Koks čia naujas mokymas? Jis įsakinėja su valdžia net netyrosioms dvasioms, ir tos Jam paklūsta!”
27Watu wote wakashangaa, wakaulizana, "Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!"
28Garsas apie Jį kaipmat pasklido po visą Galilėjos kraštą.
28Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
29Išėję iš sinagogos, jie su Jokūbu ir Jonu atėjo į Simono ir Andriejaus namus.
29Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
30Simono uošvė gulėjo karščiuodama, ir jie tuojau apie tai Jam pasakė.
30Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
31Jis priėjęs paėmė ją už rankos ir pakėlė; karštis tučtuojau paliovė, ir ji galėjo jiems patarnauti.
31Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
32Vakare, saulei nusileidus, pas Jėzų sugabeno visus ligonius ir demonų apsėstuosius.
32Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
33Visas miestas buvo susirinkęs prie durų.
33Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
34Jis pagydė daug sergančių įvairiomis ligomis, išvarė daug demonų ir neleido demonams kalbėti, nes jie pažino Jį.
34Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
35Anksti rytą, gerokai prieš aušrą, Jėzus atsikėlęs nuėjo į nuošalią vietą ir ten meldėsi.
35Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
36Simonas ir buvę su juo nusekė iš paskos
36Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
37ir, suradę Jį, pasakė: “Visi Tavęs ieško”.
37Walipomwona wakamwambia, "Kila mtu anakutafuta."
38Jis atsakė: “Eikime kitur, į gretimus miestelius, kad ir ten pamokslaučiau, nes tam esu atėjęs”.
38Yesu akawaambia, "Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo."
39Ir Jis pamokslavo jų sinagogose po visą Galilėją ir išvarinėjo demonus.
39Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
40Pas Jį atėjo raupsuotasis ir atsiklaupęs maldavo: “Jeigu nori, gali mane padaryti švarų”.
40Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, "Ukitaka, waweza kunitakasa!"
41Jėzus, apimtas gailesčio, ištiesė ranką, palietė jį ir tarė: “Noriu, būk švarus!”
41Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, "Nataka, takasika!"
42Jam tai ištarus, raupsai iškart pranyko, ir jis tapo švarus.
42Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
43Jėzus liepė jam tuojau pasišalinti ir griežtai įspėjo:
43Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
44“Žiūrėk, kad niekam nieko nepasakotum! Eik, pasirodyk kunigui ir aukok už apvalymą Mozės įsakytą atnašą jiems paliudyti”.
44"Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona."
45Bet šis išėjęs pradėjo taip plačiai skelbti ir skleisti tą įvykį, jog Jėzus nebegalėjo viešai pasirodyti mieste. Jis laikėsi už miesto, negyvenamose vietose, bet žmonės iš visur rinkosi pas Jį.
45Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.