Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

28

1Sabatui pasibaigus, auštant pirmajai savaitės dienai, Marija Magdalietė ir kita Marija atėjo pažiūrėti kapo.
1Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
2Ir štai kilo smarkus žemės drebėjimas, nes Viešpaties angelas, nužengęs iš dangaus, atėjo, nurito akmenį nuo angos, ir atsisėdo ant jo.
2Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
3Jo išvaizda buvo tarsi žaibo, o drabužiai balti kaip sniegas.
3Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
4Išsigandę jo, sargybiniai ėmė drebėti ir sustingo lyg negyvi.
4Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
5O angelas tarė moterims: “Nebijokite! Aš žinau, kad ieškote Jėzaus, kuris buvo nukryžiuotas.
5Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, "Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
6Jo čia nėra! Jis prisikėlė, kaip buvo sakęs. Įeikite, apžiūrėkite vietą, kur Viešpats gulėjo.
6Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
7Ir skubiai duokite žinią Jo mokiniams: ‘Jis prisikėlė iš numirusių ir eina pirma jūsų į Galilėją; tenai Jį pamatysite’. Štai aš jums tai pasakiau”.
7Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni."
8Jos skubiai paliko kapą, apimtos išgąsčio bei didelio džiaugsmo, ir bėgo pranešti mokiniams.
8Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
9Joms beeinant pranešti Jo mokiniams, štai Jėzus sutiko jas ir tarė: “Sveikos!” Jos priėjo, apkabino Jo kojas ir pagarbino Jį.
9Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: "Salamu." Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
10Jėzus joms tarė: “Nebijokite! Eikite ir pasakykite mano broliams, kad keliautų į Galilėją; ten jie mane pamatys”.
10Kisha Yesu akawaambia, "Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona."
11Joms beeinant, keli sargybiniai atbėgo į miestą ir pranešė aukštiesiems kunigams, kas įvyko.
11Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
12Tie susitiko su vyresniaisiais, pasitarę davė kareiviams daug pinigų
12Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
13ir primokė: “Sakykite, kad, jums bemiegant, Jo mokiniai atėję naktį Jį pavogė.
13wakisema, "Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
14O jeigu apie tai išgirstų valdytojas, mes jį įtikinsime ir apsaugosime jus nuo nemalonumų”.
14Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo."
15Šie, paėmę pinigus, taip ir padarė, kaip buvo pamokyti. Šis žodis yra pasklidęs tarp žydų iki šios dienos.
15Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
16Vienuolika mokinių nuvyko į Galilėją, ant kalno, kurį jiems buvo nurodęs Jėzus.
16Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
17Jį pamatę, jie pagarbino Jį, tačiau kai kurie abejojo.
17Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
18Tuomet priėjęs Jėzus jiems pasakė: “Man duota visa valdžia danguje ir žemėje.
18Yesu akaja karibu, akawaambia, "Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19Todėl eikite ir padarykite mano mokiniais visų tautų žmones, krikštydami juos Tėvo ir Sūnaus, ir Šventosios Dvasios vardu,
19Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
20mokydami juos laikytis visko, ką tik esu jums įsakęs. Ir štai Aš esu su jumis per visas dienas iki pasaulio pabaigos. Amen”.
20Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati."