1Rytui išaušus, visi aukštieji kunigai ir tautos vyresnieji nusprendė, kad Jėzus turi būti nužudytas.
1Kulipopambazuka, makuhani wakuu wote na wazee wa watu walifanya mashauri juu ya Yesu wapate kumwua.
2Surišę nuvedė ir atidavė Jį valdytojui Poncijui Pilotui.
2Wakamfunga pingu, wakamchukua, wakamkabidhi kwa Pilato, mkuu wa mkoa.
3Pamatęs, jog Jėzus pasmerktas, išdavikas Judas gailėjosi ir nunešė atgal aukštiesiems kunigams ir vyresniesiems trisdešimt sidabrinių,
3Hapo, Yuda ambaye ndiye aliyemsaliti, alipoona kwamba wamekwisha mhukumu Yesu, akajuta, akawarudishia makuhani wakuu zile sarafu thelathini za fedha.
4sakydamas: “Nusidėjau, išduodamas nekaltą kraują”. Tie atsakė: “Kas mums darbo? Tu žinokis!”
4Akawaambia, "Nimekosa kwa kumtoa mtu asiye na hatia auawe." Lakini wao wakasema, "Yatuhusu nini sisi? Hilo ni shauri lako."
5Nusviedęs šventykloje pinigus, jis išbėgo ir pasikorė.
5Naye akazitupa zile fedha Hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.
6Aukštieji kunigai paėmė sidabrinius ir kalbėjo: “Jų negalima dėti į šventyklos iždą, nes tai užmokestis už kraują”.
6Makuhani wakuu wakazichukua zile fedha, wakasema, "Haifai kuziweka katika hazina ya Hekalu kwa maana ni fedha za damu."
7Jie pasitarė ir už juos nupirko puodžiaus dirvą ateiviams laidoti.
7Basi, wakashauriana, wakazitumia kununua shamba la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8Todėl ta dirva iki šios dienos vadinasi Kraujo dirva.
8Ndiyo maana mpaka leo shamba hilo linaitwa Shamba la Damu.
9Tuomet išsipildė, kas buvo parašyta per pranašą Jeremiją: “Ir paėmė trisdešimt sidabriniųįkainotojo kainą, už kurią buvo Jį suderėję iš Izraelio vaikų,
9Hivyo maneno ya nabii Yeremia yakatimia: "Walizichukua sarafu thelathini za fedha, thamani ya yule ambaye watu wa Israeli walipanga bei,
10ir atidavė juos už puodžiaus dirvą; taip man Viešpats buvo paskyręs”.
10wakanunua nazo shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza."
11O Jėzus stovėjo valdytojo akivaizdoje. Valdytojas Jį klausė: “Ar Tu esi žydų karalius?” Jėzus atsakė: “Taip yra, kaip sakai”.
11Yesu alisimamishwa mbele ya mkuu wa mkoa. Basi, mkuu wa mkoa akamwuliza, "Je, wewe ndiwe Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamwambia, "Wewe umesema."
12Aukštųjų kunigų ir vyresniųjų kaltinamas, Jis nieko neatsakė.
12Lakini makuhani wakuu na wazee walipokuwa wanamshtaki, hakujibu neno.
13Tada Pilotas klausė: “Ar negirdi, kiek daug jie prieš Tave liudija?”
13Hivyo Pilato akamwuliza, "Je, husikii mashtaka hayo yote wanayotoa juu yako?"
14Bet Jis neatsakė jam nė žodžio ir tuo labai nustebino valdytoją.
14Lakini Yesu hakumjibu hata neno moja; hata huyo mkuu wa mkoa akashangaa sana.
15Per šventę valdytojas buvo pratęs paleisti miniai vieną kalinį, kurio ji norėdavo.
15Ilikuwa kawaida wakati wa Sikukuu ya Pasaka mkuu wa mkoa kuwafungulia Wayahudi mfungwa mmoja waliyemtaka.
16Tuo metu jie turėjo pagarsėjusį kalinį, vardu Barabą.
16Wakati huo kulikuwa na mfungwa mmoja, jina lake Baraba.
17Todėl, žmonėms susirinkus, Pilotas klausė: “Kurį norite, kad jums paleisčiau: Barabą ar Jėzų, vadinamą Kristumi?”
17Hivyo, watu walipokusanyika pamoja, Pilato akawauliza, "Mwataka nimfungue yupi kati ya wawili hawa, Baraba ama Yesu aitwae Kristo?"
18Nes jis žinojo, kad Jėzų jie buvo išdavę iš pavydo.
18Alisema hivyo maana alijua wazi kwamba walimleta kwake kwa sababu ya wivu.
19Sėdinčiam teismo krėsle Pilotui žmona atsiuntė įspėjimą: “Nieko nedaryk šitam teisiajam, nes šiąnakt sapne labai dėl Jo kentėjau”.
19Pilato alipokuwa amekaa katika kiti cha hukumu, mke wake akampelekea ujumbe: "Usijitie katika shauri la mtu huyu mwema, maana leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake."
20Bet aukštieji kunigai ir vyresnieji įtikino minią, kad prašytų paleisti Barabą, o Jėzų pražudytų.
20Lakini makuhani wakuu na wazee wakawashawishi watu waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe.
21Tada valdytojas jiems tarė: “Kurį iš šių dviejų norite, kad jums paleisčiau?” Jie šaukė: “Barabą!”
21Mkuu wa mkoa akawauliza, "Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka nimfungue?" Wakamjibu, "Baraba!"
22Pilotas paklausė: “Ką gi man daryti su Jėzumi, kuris vadinamas Kristumi?” Jie visi rėkė: “Nukryžiuok Jį!”
22Pilato akawauliza, "Sasa, nifanye nini na Yesu aitwaye Kristo?" Wote wakasema, "Asulubiwe!"
23Jis klausė: “Ką bloga Jis padarė?” Bet jie dar garsiau šaukė: “Nukryžiuok Jį!”
23Pilato akauliza, "Kwa nini? Amefanya kosa gani?" Wao wakazidi kupaaza sauti: "Asulubiwe!"
24Pilotas, pamatęs, kad nieko nelaimi, o sąmyšis tik didėja, paėmė vandens, nusiplovė rankas minios akivaizdoje ir tarė: “Aš nekaltas dėl šio teisiojo kraujo. Jūs žinokitės!”
24Basi, Pilato alipotambua kwamba hafanikiwi chochote na kwamba maasi yalikuwa yanaanza, alichukua maji, akanawa mikono mbele ya ule umati wa watu, akasema, "Mimi sina lawama juu ya kifo cha mtu huyu; shauri lenu wenyewe."
25Visi žmonės šaukė: “Jo kraujas tekrinta ant mūsų ir ant mūsų vaikų!”
25Watu wote wakasema, "Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!"
26Tada jis paleido jiems Barabą, o Jėzų nuplakdinęs atidavė nukryžiuoti.
26Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, lakini akamtoa Yesu asulubiwe.
27Valdytojo kareiviai nusivedė Jėzų į pretorijų ir surinko aplink jį visą kuopą.
27Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.
28Jie išrengė Jį ir apsiautė raudonu apsiaustu.
28Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.
29Nupynę erškėčių vainiką, uždėjo Jam ant galvos, o į Jo dešinę įspraudė nendrę. Po to tyčiodamiesi klūpčiojo prieš Jį ir sakė: “Sveikas, žydų karaliau!”
29Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, "Shikamoo mfalme wa Wayahudi!"
30Spjaudydami Jį, stvėrė iš Jo nendrę ir čaižė per galvą.
30Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.
31Pasityčioję iš Jo, jie nusiautė apsiaustą, apvilko Jo paties drabužiais ir išsivedė nukryžiuoti.
31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
32Išeidami jie sutiko žmogų iš Kirėnės, vardu Simoną. Tą privertė nešti Jėzaus kryžių.
32Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.
33Atėję į vietą, vadinamą Golgota (tai yra: “Kaukolės vieta”),
33Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, "Mahali pa Fuvu la kichwa,"
34davė Jam gerti rūgštaus vyno, sumaišyto su tulžimi, bet Jėzus paragavęs negėrė.
34wakampa mchanganyiko wa divai na nyongo. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.
35Nukryžiavę Jį, pasidalijo Jo drabužius, mesdami burtą, kad išsipildytų, kas buvo per pranašą pasakyta: “Jie dalinosi mano drabužius ir dėl mano apdaro metė burtą”.
35Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
36Ir ten pat susėdę, saugojo Jį.
36Wakaketi, wakawa wanamchunga.
37Viršum Jo galvos jie prisegė užrašytą Jo kaltinimą: “Šitas yra Jėzus, žydų karalius”.
37Juu ya kichwa chake wakaweka shtaka dhidi yake lilioandikwa, "Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi."
38Kartu su Juo buvo nukryžiuoti du plėšikai, vienas iš dešinės, kitas iš kairės.
38Wanyang'anyi wawili walisulubishwa pia pamoja naye, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
39Einantys pro šalį užgauliojo Jėzų, kraipydami galvas
39Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana wakitikisa vichwa vyao na kusema,
40ir sakydami: “Še Tau, kuris sugriauni šventyklą ir per tris dienas atstatai; išgelbėk save! Jei esi Dievo Sūnus, nuženk nuo kryžiaus!”
40"Wewe! Si ulijidai kulivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu? Sasa jiokoe mwenyewe. Kama wewe ni Mwana wa Mungu, basi shuka msalabani!"
41Taip pat tyčiojosi aukštieji kunigai su Rašto žinovais ir vyresniaisiais, kalbėdami:
41Hali kadhalika na makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria na wazee walimdhihaki wakisema,
42“Kitus išgelbėdavo, o pats negali išsigelbėti. Jeigu Jis Izraelio karalius, tenužengia dabar nuo kryžiaus, ir mes Juo tikėsime.
42"Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi! Eti yeye ni mfalme wa Wayahudi! Basi, sasa na ashuke msalabani, nasi tutamwamini.
43Jis pasitikėjo Dievu, tad teišvaduoja Tas dabar Jį, jeigu Jam Jo reikia, nes Jis sakė: ‘Aš Dievo Sūnus’ ”.
43Alimtumainia Mungu na kusema eti yeye ni Mwana wa Mungu; basi, Mungu na amwokoe kama anamtaka."
44Taip pat Jį užgauliojo ir kartu nukryžiuoti plėšikai.
44Hali kadhalika na wale waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana.
45Nuo šeštos iki devintos valandos visą kraštą gaubė tamsa.
45Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa, nchi yote ikawa katika giza.
46O apie devintą valandą Jėzus sušuko garsiu balsu: “Elí, Elí, lemá sabachtáni?”, tai reiškia: “Mano Dieve, mano Dieve, kodėl mane palikai?!”
46Mnamo saa tisa Yesu akalia kwa sauti kubwa, "Eli, Eli, lema sabakthani?" Maana yake, "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?"
47Kai kurie iš ten stovėjusiųjų, tai išgirdę, sakė: “Jis šaukiasi Elijo”.
47Lakini wale waliosimama pale waliposikia hivyo wakasema, "Anamwita Eliya."
48Ir tuoj vienas iš jų pribėgęs paėmė kempinę, primirkė ją rūgštaus vyno, užmovė ant nendrės ir padavė Jam gerti.
48Mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo, akaichovya katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe.
49Kiti kalbėjo: “Liaukis! Pažiūrėsim, ar ateis Elijas Jo išgelbėti”.
49Wengine wakasema, "Acha tuone kama Eliya anakuja kumwokoa."
50Tada Jėzus, dar kartą sušukęs garsiu balsu, atidavė dvasią.
50Basi, Yesu akalia tena kwa sauti kubwa, akakata roho.
51Ir štai šventyklos uždanga perplyšo pusiau nuo viršaus iki apačios, ir žemė sudrebėjo, ir uolos ėmė skeldėti.
51Hapo pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili, toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
52Atsidarė kapai, ir daug užmigusių šventųjų kūnų prisikėlė.
52makaburi yakafunguka na watu wengi wa Mungu waliokufa wakafufuliwa;
53Išėję iš kapų po Jo prisikėlimo, jie atėjo į šventąjį miestą ir daug kam pasirodė.
53nao, baada ya kufufuka kwake, wakatoka makaburini, wakaingia katika Mji Mtakatifu, wakaonekana na watu wengi.
54Šimtininkas ir kiti su juo saugojantys Jėzų, pamatę žemės drebėjimą ir visa, kas dėjosi, labai išsigando ir sakė: “Tikrai šitas buvo Dievo Sūnus!”
54Basi, jemadari na wale waliokuwa wakimlinda Yesu walipoona tetemeko la ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, "Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu."
55Tenai buvo daug moterų, kurios žiūrėjo iš tolo. Jos sekė paskui Jėzų nuo Galilėjos, Jam tarnaudamos.
55Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia.
56Tarp jų buvo Marija Magdalietė, Jokūbo ir Jozės motina Marija ir Zebediejaus sūnų motina.
56Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo.
57Vakarui atėjus, atvyko vienas turtingas žmogus iš Arimatėjos, vardu Juozapas, kuris irgi buvo tapęs Jėzaus mokiniu.
57Ilipokuwa jioni, akaja mtu mmoja tajiri mwenyeji wa Armathaya, jina lake Yosefu. Yeye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58Jis nuėjo pas Pilotą ir paprašė Jėzaus kūno. Pilotas įsakė kūną atiduoti.
58Akamwendea Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. Basi, Pilato akaamuru apewe.
59Juozapas paėmė kūną, įvyniojo į švarią drobulę
59Yosefu akauchukua ule mwili akauzungushia sanda safi ya kitani,
60ir paguldė savo naujame kape, kurį buvo išsikaldinęs uoloje. Užritęs didelį akmenį ant kapo angos, nuėjo.
60akauweka ndani ya kaburi lake jipya alilokuwa amelichonga katika mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
61Ten buvo Marija Magdalietė ir kita Marija, kurios sėdėjo priešais kapą.
61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwa wameketi kulielekea kaburi.
62Kitą dieną, po Prisirengimo dienos, susirinko pas Pilotą aukštieji kunigai bei fariziejai
62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalio, makuhani wakuu na Mafarisayo walimwendea Pilato,
63ir kalbėjo: “Valdove, mes prisimename, jog tas suvedžiotojas, dar gyvas būdamas, sakė: ‘Po trijų dienų prisikelsiu’.
63Wakasema, "Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, Baada ya siku tatu nitafufuka.
64Įsakyk tad saugoti kapą iki trečios dienos, kad kartais nakčia atėję Jo mokiniai nepavogtų Jo ir nepaskelbtų žmonėms: ‘Jis prisikėlė iš numirusių’. Pastaroji apgavystė būtų blogesnė už pirmąją”.
64Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa awali."
65Pilotas jiems atsakė: “Štai jums sargybaeikite ir saugokite, kaip išmanote”.
65Pilato akawaambia, "Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo."
66Jie nuėjo, pastatė prie kapo sargybą ir paženklino antspaudu akmenį.
66Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.